Dar: Polisi waua watu wawili wakamatwa, wamekamata risasi zaidi ya 162

Kazi nzuri pongezi kwa polisi lakini je kama huyo Shafi ni lini alitoroka gerezani? Kwanini raia hatukutahadharishwa?
 
1. Hivi inakuwaje kila majambazi wakikamatwa wanafariki wakiwa njiani kuelekea hospitali?
Mkuu kama kuna msela unamjua mtu wa matukio mshauri aache,siku hizi hawaruhusu jambazi apelekwe hospitalini au mahakamani,tangu walipouwawa polisi wenzao wakishakuchukua maelezo wanakumalizia njiani wakiwa wanakupeleka hospitalini,huko nyuma jambazi alikuwa anafungwa baadae anakata rufaa anatoka halafu anaanza kusumbua mtaani tena,mambo ya upelelezi bado haujakamilika kwa majambazi hakuna tena.Na wanapukutika kweli,itafika wakati ujambazi utabaki 1% kama sio kuisha kabisa.
 
Wale waliovamia IMMMA wamekimbia kusikojulikana nn mbona hawakamatwi?
 
Hiiiv....siku zoote hawa majambaz wao hufa wakati wakiwa wanakimbizwa hospital?? Hakuna hata siku moja kwamba polisi walipiga risasi akafa hapo hapo???
 

MLETA TAARIFA SIJAELEWA INA MAANA HUYU ANAETUMIKIA KIFUNGO CHA MIAKA 30 AKAKAMATWA NA UJAMBAZI .

HEBU WEKA TAARIFA YAKO VIZULI ISIJE UKAWA UMEJITUNGIA TUU
 
~~~>>>Kwa siku 3 tu Pesa za tozo zilizopatikana ni Tsh. 424,620,000/=......


Na hii ni kwa Daslam tu.....
 
Nilichokiamini kwenye hizi porojo za Mambo Kesho ni Tozo tu mengine yote ni soga za kujisifia ili kupoteza lengo.

Hatutaondoka kwenye sakata la Lissu mpaka wahusika watakapokamatwa.
Bado mnataka FBI? Kwa hiyo Tundulissu ni damu zaidi kuliko wanaCCM walioawa Kibiti au polisi waliouawa Sitakishari?
 
porojo tu hakuna kingine, yaani majambazi mmewasimamisha wakagundua ni polisi katika kufyatuliana risasi(asa sijui walishuka kwenye gari) maana kama hawakushuka wangetoroka na aliye toroka na gari.

hawa wameingia studia kutengeneza movie, wiki majambazi waliovunja ofisi ya mawakili hawajagawana pesa japo wamefanikiwa kulikata sanduku la mkwanja

hollywood
 
Namna hiyo kazi nzuri. Ila nauliz majambazi wa siku hizi mbona wote hufia njiani wakipelekwa hospitali?
 

Sasa mkuu kama wanaoenda kufanya kazi jeshi la polisi ni form four wenye division four, unatarajia wakitunga script zao zinakuwa na tofauti na bongo movie? Story ina maswali mengi sana
 
Ni mazoea lakini si sahihi kusema " polisi wamefanikiwa kuua ......" Hii inamaanisha polisi walikuwa na kusudio la kuuwa
they've that right of killing under when the situation is uneven secured!!
 
Kuna mijitu kazi yao ni kuponda tu, sijui ilipewa semina kwamba chochote mtakachoona pondeni tu,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…