Dar mnatuangusha sana wana UKAWA

Dar mnatuangusha sana wana UKAWA

Nilishasema humu wakazi wengi wa Dar ni waswahili (hawajaelimika, wavivu, wacheza vigodoro) wakifuatiwa na wezi wa maofisini (wanaogopa ukiwa kinyume na CCM unapelekwa Namanyere), malaya/mashangingi, mateja/wapiga debe, wapambe na wafanyabiashara wakwepa kodi (pinga CCM ukione) so kumuondoa huyu mdudu CCM kazi ipo!
Ukikaa nyuma ya meza ya mfalme harufu ya jipilau hutaikosa na pia vijifupa vya miguu ya kuku anavyotupa chini mfalme wanaviokota; Dar ni sehemu ya ufisadi uliokomaa nchini na wapo tayari kuulinda kwa kutojali
 
Nashukuru kwa kutukumbusha na nakuhakikishia 2015 hatuwaangushi,mfano huku segerea no wazi Mahanga kama sio majanga lazima aachie wadhifa.
 
Mleta uzi hana uchambuzi wa maana.Nani ka gain katika uchaguzi huu?vilikuwepo vitongoji vichache sana Dar lakini sasa kata nzimanzima zina ongozwa na wapinzani.hata ukuwa uliza ccm makini wanajua na wanatafakari kasi ya kupoteza mitaa.Ina maana tukirudia kama kasi ndiyo hii na mapingamizi ya sipokuwepo ccm kita kuwa chama cha upinzani,jambo ambalo litafanya wajinyonge
 
Mleta uzi hana uchambuzi wa maana.Nani ka gain katika uchaguzi huu?vilikuwepo vitongoji vichache sana Dar lakini sasa kata nzimanzima zina ongozwa na wapinzani.hata ukuwa uliza ccm makini wanajua na wanatafakari kasi ya kupoteza mitaa.Ina maana tukirudia kama kasi ndiyo hii na mapingamizi ya sipokuwepo ccm kita kuwa chama cha upinzani,jambo ambalo litafanya wajinyonge

Chama Cha Mapingamizi-CCM, maana bila mapingamizi na hila hawawezi kushinda kama ilivyofanyika Kilindi
 
Bora samaki samakinchanga umesema, huwa nawafikiria sana hao ndugu zangu wa hapo jijini dar.
kuna kitu kinamis somewhere ila nahisi wengi wamekua wazoefu wa shida(mabingwa wa tabu) hawajali tena bora liende.
Kuna namna ya kufanya kuwakomboa kwa kuwaonyesha mifano venye sisi tunafanya.
 
UKAWA imeanguka Tanzania nzima si Dar pekee.

Fananisha 80% na 20% halafu bado mna kauli?
 
Ukiona dar wamepata hzo asilimia ujue vijijini wanainchi ambako hawajui escrow nin ,UKAWA wamepata 10%
 
Wasomi wengi dar hawapigi kura. Na pia si wahamasishaji wazuri. Hii itatugharimu sana 2015 tusipokuwa makini.
 
Samaki mchanga wape bigup wana Dar es salaam ....wana ukawa wamepata 25% ccm 75% lakini unajua kuwa serikali nzima inaishi Dar? usalama wote wanaishi Dar ....wakuu wote wa majeshi wako Dar .......wajuaji wote ...wasoma magazeti wote ..much know wote wanashi Dar......Samaki mchanga vita ni kali kuliko mikoani ....sasa unadhani ccm hapa Dar ndipo ikulu ipo ....ghafla tu wakubali wapokwe Dar .....taratibu ndiyo mwendo tutaelewana tu ni jambo la Muda
comment yako imenipa hope walau kidogo, ila pamoja na hayo makundi yaliyotawala hapo dar kama ulivyoyataja , bado ni % kubwa mno ya wakazi wa hapo ni masikini wa kiwango wa kushindia mlo miwili per day lakini hawajigusi, vichwa viko chini kama kondoo hawaonyeshi nia ya kuchukizwa na umasikini wala hawana hata muda wa kujua chanzo cha umasikini wao,
yaani wamemuachia mungu ilimradi kukuche.
Watu wa taabu ya namna hii inayotokana na system waliyoiweka kwa ridhaa yao wenyewe wanastahili kuwa front kumpazia sauti mtawala waliomkabithi mamlaka ya kuwatawala na kudai haki yao na kuchochea mabadiliko ya mfumo kujikomboa.
Dar wamachinga pekee ndio mmewaacha wanajitokeza peke yao hawana back up ya watu wa kada zingine wakiwa front kwenye kusimamia haki na mabadiliko.
Imagine ile kada ya vijana unaopishana nao hapo posta na bahasha za cv's zilizolowa jasho kwa kuzunguka kila kukicha kutafuta ajira hewa, kada hii ingekuwa inanawapa back up hao wamachinga wetu walau hata kuhamasisha na kuwa front kwenye vote ballot walau ili sura za wenye kuhitaji mabadiliko zisiwe zile-zile za wamachinga wa kila siku,
Hapo Dar tuna kada kubwa mno ya vijana smart wenye taabu zitokanazo na system na taabu hizo ni kubwa kuliko za wamachinga ila huwa wanajifungia ndani wanaposikia sauti ya mabadiliko ikirindima huko nje na kuwaachia wamachinga pekee wapambane, na kutokana na hulka ya wamachinga obviously inakuwa easy kuwapa wanamabadiliko hawa picha ya wahuni kutokana na nature ya ajira ya wataka mabadiliko mliowaachia jukumu la kuwasaidia kudai haki na mabadiliko.
Kenya Mtawala anabehave na anajali watawaliwa kwasabau anajua aki-disturb rights za watawaliwa yeye kama mtawala atapata challenge kubwa kwasababu wanaotoka front kupaza sauti kudai haki na mabadiliko ya system ni watu wa maana: kada za wasomi, wamachinga, wafanyakazi, wasio na ajira n.k.
Hakuna mjinga Nairobi, Bunge likifanya maamuzi ya kipuuzi raiya wote bila kujali kada watachonga majeneza ya wabunge na majina yao na kuja nayo nje ya bunge kuwapinga watawala na challenge dhidi ya mtawala inaonekana wazi kwasababu watawaliwa wa kila kada wamejielewa na wamejitokeza kwa pamoja kudai na kusimamia haki inayokiukwa na mtawala na mwisho wa siku mtawala nasurrender na ananyooka.
Misri chanzo cha harakati zote za mabadiliko zilianzishwa na Mmachinga aliyejipa ajira hiyo ya umachinga baada ya kumaliza chuo kikuu na kukosa ajira, mmachinga aliyejimwagia petrol na kujiwasha moto hadi kufa kupinga uonevu wa askari wa jiji.
Hapa kwetu mtoto anamaliza mpaka masters na anakosa ajira, hajiajiri, ana miaka 40 anakula na kulala kwa wazazi hajigusi hadi kifo chake kitakapomkuta.
Shule ni muhimu sana, binafsi kupenda kujisomea ni silaha pekee ya kumuinua mnyonge.
Shule ni muhimu sana jamani, shule sio kwa ajili ya kupata ajira , bali kujua wewe ni nani, na unastahili nini na unastahili kufanya nini kupata unachostahili.
 
Bahati waliyonayo watu wa Dar ni kuwa wapiga deals za siasa wote wapo dar, wana shinda kwenye vijiwe wa Kahawa na bia, na mipango yao ya matukio wanaijua na sababu zake. Kudanganyika watu kama hao ni ngumu ndiyo maana maeneo yote ya watoto wa mjini inakuwa ngumu.
 
Siku za kujiandikisha iwe miezi 2.pana foleni sana dar,huwezi wahi kabla ya saa 12 tunaipenda sana ukawa.
 
UKAWA imeanguka Tanzania nzima si Dar pekee.Fananisha 80% na 20% halafu bado mna kauli?
Dada......Subiri hautaamini 2015.../ ni jambo la nuda ...najua unaipenda ccm .....na kwa bahati mbaya leo nikiyaweka matokeo halisi jinsi UKAWA walivyo fanya vizuri utashika kichwa .........................wewe jiulize Dar UKAWA wamepata 25% how about mwz...mby...arsh...morog....and other party in our country? ........Faizafoxy.......kuna kitu natamani ukijue ...kwamba 2015 UKAWA watakuwa wamoja kuliko leo ... .plus ile migogoro ya ccm ....plus makundi ....dada hamtaamini kitachotokea ....ni jambo la 6 miezi ....ama UKAWA AU CCM
 
Back
Top Bottom