DAR LUX yadhalilisha abiria wake

DAR LUX yadhalilisha abiria wake

PrinceNsabho

Member
Joined
Oct 27, 2015
Posts
34
Reaction score
27
Mabasi ya DAR LUX yafanyayo safari zake ktk baadhi ya mikoa hapa nchini imejikuta ikidhalilisha abiria wake baada yakuonekana inapendwa na abiria wengi. Uongozi wa kampuni hiyo umejikuta unaingiwa tamaa na kujikuta inalazimisha madereva wake kufika na kugeuza siku hiyo hiyo bila kujali umbali wa safari anayoenda ( yaani go and return) bila kupumzika kwa kuwa wapo wawili ktk kila gari.

Hali hiyo leo imesababisha Dereva kusinzia mpaka saa moja kasorobo na kuibua taharuki kubwa kwa abiria wa gari Na.2 la Dar-Mza.Hizo ni taarifa nilizozipata kwa mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo ambaye chonde ameomba kuhifadhi jina lake. Kwa mujibu wa bwana huyo ameongeza kusema hata ujira wa madereva wake hauendani na umbali wa safari za Mza tena kwa kwenda nakugeuza.

Tuwaombe mamlaka zinazohusika na safari za mabasi kuchunguza hilo swala kwa kuwa ni la hatari kwa usalama wa abiria na madereva wake
 
Hujaeleweka
Dereva kusinzia mpaka saa moja kasoro robo, ina maana akiwa katika usukani au ofisini kwao?
aliyekuletea habari hdizo muambie awasiliane na namba za SUMATRA zipo katika kila Basi la abiria kioo cha pili toka kiti cha ereva,
Au awasiliane na Chama cha abiria CHAKUA wapo Stand ya Ubungo, Msamvu, Stabd ya Mkoa Dodoma, hata huko Mwanza hawa CHAKUA simu zao zinawasiliana na Traffic Makao Makuu, Traffi wa barabarani wote mikoani, na SUMATRA pia wana Whatsapp/
Kama Basi linageuza na Madereva wanabadilishana, sioni tatizo ila kama Basi ni bovu au kujaza abiria na kuwasimamisha waripoti
 
Sijaelewa, nitarudi baadaye!
Sijaelewa ni kwa mazingira yapi ya udhalilishaji wa abiria? Isipokuwa nimeona kama watumishi wa kampuni ndio hawana mazingira mazuri ya kazi (May be)
 
Hebu fafanua vizuri Dar-Mwanza wanaenda nakugeuza? Unajua umbali wa kutoka Dar-Mwanza? Au umemaanisha madereva hawabadilishani/hawapokezani ruti zao?


mtoa mada anamaanisha basi linapofika mwanza au dar linatakiwa lianze safari siku inayofuata ambapo ni kinyume na sumatra. kila kampuni inatakiwa kuwa na basi moja stand by katika mkoa husika ambapo basi linalofika leo linatakiwa kuondoka kesho kutwa. nadhani sumatra pamoja na askari wa barabarani wangetilia mkazo katika hili kwani limesaidia sana kupunguza ajali. pamoja na aliyosema mtoa mada bado dar lux wanajitahidi sana katika kutoa huduma nzuri ndani ya mabasi yao kwa wateja.
 
Cyo kwenda nakugeuza kwa maana ya mchana mmoja, nikwamba mfano gari linatoka Mza asbh j'mosi linafika dar saa saba usiku afu kesho yake asbh gari hilo hilo lirudi Mza huko ndiko namaanisha, lkn pia muda wa mabasi kuondoka stendi ni saa 12 kamili na abiria wanakuwa hapo saa moja kabla ya muda, hivyo kukaa mpaka saa moja kasoro unaweza kuiona taharuki niliyosema
 
Sijaelewa, nitarudi baadaye!
Sijaelewa ni kwa mazingira yapi ya udhalilishaji wa abiria? Isipokuwa nimeona kama watumishi wa kampuni ndio hawana mazingira mazuri ya kazi (May be)

sikupingi ila kweli kichwa cha habari pamoja na habari havioani. katika habari nzima thima iko katika haki za madereva pamoja na usalama wa abiria na mali zao. nadhani mleta mada angebadilisha kidogo, vile vile naona uzembe wa sumatra na traffic kwani wao hawawezi kuona basi lenye namba za jana leo pia linapita na madereva wale wale wa jana
 
mtoa mada anamaanisha basi linapofika mwanza au dar linatakiwa lianze safari siku inayofuata ambapo ni kinyume na sumatra. kila kampuni inatakiwa kuwa na basi moja stand by katika mkoa husika ambapo basi linalofika leo linatakiwa kuondoka kesho kutwa. nadhani sumatra pamoja na askari wa barabarani wangetilia mkazo katika hili kwani limesaidia sana kupunguza ajali. pamoja na aliyosema mtoa mada bado dar lux wanajitahidi sana katika kutoa huduma nzuri ndani ya mabasi yao kwa wateja.
Hapa naona umetumia Biology na chemistry kwenye hitimisho lako.
Yaani gari ikipumzika siku moja halafu ndio ifanye safari inaondoa uwezekano wa kuanguka!?
Physics inakataa!!!!!
 
mtoa mada anamaanisha basi linapofika mwanza au dar linatakiwa lianze safari siku inayofuata ambapo ni kinyume na sumatra. kila kampuni inatakiwa kuwa na basi moja stand by katika mkoa husika ambapo basi linalofika leo linatakiwa kuondoka kesho kutwa. nadhani sumatra pamoja na askari wa barabarani wangetilia mkazo katika hili kwani limesaidia sana kupunguza ajali. pamoja na aliyosema mtoa mada bado dar lux wanajitahidi sana katika kutoa huduma nzuri ndani ya mabasi yao kwa wateja.
Basi alitakiwa aseme hivyo mana alikuwa anakitu cha muhimu ila uwasilishaji ndo kachemka...ila Dar Lux wapo vizuri lakini kuna mikokoteni kama Najimunisa,Green Star(sijui bado lipo)..haya si ya kujiroga kupanda safari ya Mwanza
 
Mabasi ya DAR LUX yafanyayo safari zake ktk baadhi ya mikoa hapa nchini imejikuta ikidharirisha abiria wake baada yakuonekana inapendwa na abiria wengi. Uongozi wa compuni hiyo umejikuta unaingiwa tamaa nakujikuta inalazimisha madereva wake kufika nakugeuza siku hiyo hiyo bila kujali umbali wa safari anayoenda ( yaani go and return) bila kupumzika kwakuwa wapo wawili ktk kila gari. Hali hiyo leo imesababisha Dereva kusinzia mpaka saa moja kasorobo nakuibua taharuki kubwa kwa abiria wa gari Na.2 la Dar-Mza.Hizo ni taarifa nilizozipata kwa mmoja wa wafanyakazi wakampuni hiyo ambae chonde ameomba kuhifadhi jina lake. Kwa mujibu wa bwana huyo ameongeza kusema hata ujira wa madereva wake hauendani na umbali wa safari za Mza tena kwa kwenda nakugeuza.Tuwaombe mamlaka zinazohusika na safari za mabasi kuchunguza hilo swala kwakuwa ni la hatari kwa usalama wa abiria na madereva wake
Wenzako hulipia fedha kwa ajili ya kujifunza uandishi wa habari, wewe naona unadandia kiberenge.
 
Cyo kwenda nakugeuza kwa maana ya mchana mmoja, nikwamba mfano gari linatoka Mza asbh j'mosi linafika dar saa saba usiku afu kesho yake asbh gari hilo hilo lirudi Mza huko ndiko namaanisha, lkn pia muda wa mabasi kuondoka stendi ni saa 12 kamili na abiria wanakuwa hapo saa moja kabla ya muda, hivyo kukaa mpaka saa moja kasoro unaweza kuiona taharuki niliyosema


kuhusu abiria kuwahi hilo umeongeza chumvi. mabasi yote ya mikoani yanaanza kuruhusiwa saa 12 na katika mabasi kwenye tiketi yamewaelekeza abiria kufika ofisini/ kituo cha basi kuanzia nusu saa kabla ya muda wa kuondoka ili kuondoa adha, hapo kuondoka saa moja kasoro siyo tatizo la dar lux ila ni kutokana na foleni ya mabasi kutoka, au unataka wapae? mbona kwenye ndege unatakiwa masaa mawili kabla? au umetumwa kuharibu biashara ya watu? acha chuki
 
Mabasi ya DAR LUX yafanyayo safari zake ktk baadhi ya mikoa hapa nchini imejikuta ikidharirisha abiria wake baada yakuonekana inapendwa na abiria wengi. Uongozi wa compuni hiyo umejikuta unaingiwa tamaa nakujikuta inalazimisha madereva wake kufika nakugeuza siku hiyo hiyo bila kujali umbali wa safari anayoenda ( yaani go and return) bila kupumzika kwakuwa wapo wawili ktk kila gari. Hali hiyo leo imesababisha Dereva kusinzia mpaka saa moja kasorobo nakuibua taharuki kubwa kwa abiria wa gari Na.2 la Dar-Mza.Hizo ni taarifa nilizozipata kwa mmoja wa wafanyakazi wakampuni hiyo ambae chonde ameomba kuhifadhi jina lake. Kwa mujibu wa bwana huyo ameongeza kusema hata ujira wa madereva wake hauendani na umbali wa safari za Mza tena kwa kwenda nakugeuza.Tuwaombe mamlaka zinazohusika na safari za mabasi kuchunguza hilo swala kwakuwa ni la hatari kwa usalama wa abiria na madereva wake
Nawasiwasi na wewe si mtu utakuwa umetumwa jini wewe
 
Najimunisa DUME LA MBEGU. Barabara toka ikiwa ya vumbi kampuni ilitupenda na kutupa huduma safi mpaka imewekwa lami nayo imeendelea kutoa huduma!!
Hatutatupa mbachao kwa msala upitao.
Ya nini kutema BigG kwa karanga za kuonjeshwa?
Basi alitakiwa aseme hivyo mana alikuwa anakitu cha muhimu ila uwasilishaji ndo kachemka...ila Dar Lux wapo vizuri lakini kuna mikokoteni kama Najimunisa,Green Star(sijui bado lipo)..haya si ya kujiroga kupanda safari ya Mwanza
 
Hapa naona umetumia Biology na chemistry kwenye hitimisho lako.
Yaani gari ikipumzika siku moja halafu ndio ifanye safari inaondoa uwezekano wa kuanguka!?
Physics inakataa!!!!!
Nafikiri alimaanisha madereva wapate muda wa kupumzika
 
Basi alitakiwa aseme hivyo mana alikuwa anakitu cha muhimu ila uwasilishaji ndo kachemka...ila Dar Lux wapo vizuri lakini kuna mikokoteni kama Najimunisa,Green Star(sijui bado lipo)..haya si ya kujiroga kupanda safari ya Mwanza

kweli kabisa kak, dar lux wako vizuri na wanautaratibi mzuri. nadhani huyu mtoa mada atakuwa katumwa kuwachafua maana njia ya mwanza lazima basi moja liwe mwanza la stand by au kama yeye ni dereva aseme kuwa hawalipwi vizuri. maana mfano ukitoka mwanza ukaingia morogoro saa nne kasoro usiku hamruhusiwi tena kuendelea kuja dar hadi kesho yake saa 12 asubuhi. je huyo dereva atageuza saa ngapi?
 
Back
Top Bottom