Chibudee
JF-Expert Member
- Dec 28, 2016
- 1,775
- 2,397
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemuhoji Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima kwa tuhuma za kusambaza kipeperushi na sauti kwa lugha ya Kisukuma zenye lengo la kuhamasisha watu kuunda kikundi cha kikabila nchini. Kipeperushi kilikuwa na picha ya Rais Magufuli.
Sent using Jamii Forums mobile app
=====
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemuhoji Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, kwa tuhuma za kusambaza kipeperushi na sauti kwa lugha ya kisukuma, zenye lengo la kuhamasisha watu kuunda kikundi cha kikabila nchini.
Taarifa hiyo imetolewa leo Machi 3, 2020, na Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, SACP Camillius Wambura, na kusema kuwa kutokana na jumbe hizo kuonekana kuhamasisha vitendo vya kikabila,Jeshi hilo limempa onyo kali la kuacha mara moja vitendo vya kuligawa Taifa.
"Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemuonya vikali Askofu Gwajima kuacha mara moja, vitendo vya kuligawa Taifa kwa kutumia vigezo vya ukabila na kutoa onyo kwa wote wenye nia ya kutaka kuligawa Taifa kwa njia ya ukabila, udini ama ukanda" amesema SACP Wambura.
Aidha Kamanda Wambura ameongeza kuwa, "Katika ujumbe huo wa sauti Askofu Gwajima pia, amewataka wasukuma matajiri kuungana kwa pamoja kwa lengo la kuwasaidia wasukuma maskini ili kuondoa dhana ya kwamba wasukuma ni maskini na ni washamba".
Sent using Jamii Forums mobile app
=====
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemuhoji Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, kwa tuhuma za kusambaza kipeperushi na sauti kwa lugha ya kisukuma, zenye lengo la kuhamasisha watu kuunda kikundi cha kikabila nchini.
Taarifa hiyo imetolewa leo Machi 3, 2020, na Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, SACP Camillius Wambura, na kusema kuwa kutokana na jumbe hizo kuonekana kuhamasisha vitendo vya kikabila,Jeshi hilo limempa onyo kali la kuacha mara moja vitendo vya kuligawa Taifa.
"Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemuonya vikali Askofu Gwajima kuacha mara moja, vitendo vya kuligawa Taifa kwa kutumia vigezo vya ukabila na kutoa onyo kwa wote wenye nia ya kutaka kuligawa Taifa kwa njia ya ukabila, udini ama ukanda" amesema SACP Wambura.
Aidha Kamanda Wambura ameongeza kuwa, "Katika ujumbe huo wa sauti Askofu Gwajima pia, amewataka wasukuma matajiri kuungana kwa pamoja kwa lengo la kuwasaidia wasukuma maskini ili kuondoa dhana ya kwamba wasukuma ni maskini na ni washamba".