JoJiPoJi
JF-Expert Member
- Aug 8, 2009
- 2,907
- 3,261
na Lucy Ngowi
MBUNGE wa Viti Maalum, Janeth Massaburi (CCM), amebainisha kuwa mkoa wa Dar es Salaam, unaongoza kwa rushwa ya ngono hasa kipindi cha uchaguzi au mtu anapotaka uongozi.
Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es salaam kwenye semina ya ukimwi iliyoendeshwa na taasisi ya Engender Health kwa wabunge wa Kamati ya Bunge inayohusika na masuala ya ukimwi.
Massaburi alisema, mtu anayetaka nafasi ya kuongoza kwenye uchaguzi, kampuni binafsi na serikalini, ngono imekuwa ni sehemu ya kigezo cha kupata nafasi hizo.
Umaskini unasababisha rushwa ya ngono, mtu anapotaka nafasi yoyote ya kuongoza ili ajulikane, iwe ni kwenye kampuni binafsi, serikalini au katika kipindi cha uchaguzi anatakiwa atoe rushwa ya ngono.
Wasiwasi wangu watu wanafanya hivyo ili kupata cheo, hasa kwenye jimbo langu la Dar es Salaam ambalo nimeona hali hiyo ikijitokeza mara kwa mara, alisema Massaburi.
Aliongeza kuwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wamekuwa wakijidanganya kuwa wana uelewa mkubwa wa ugonjwa huo wakati ukweli si huo.
Alishauri Engender Health iwatumie wabunge wa majimbo, viti maalumu na madiwani ili waweze kuwafikia wananchi kwa urahisi na kuwaelewesha kuhusu athari za ugonjwa wa ukimwi.
Naye mbunge wa Jimbo la Bukene, Teddy Kasella-Bantu (CCM), alisema katika jimbo lake ngoma na ulinzi wa sungusungu vinachangia kuwepo kwa ongezeko la ukimwi kwa kuwa wananchi hawana elimu ya kutosha.
Katika jimbo langu kuna kitu kama ngoma, ambazo zinakuwepo kwa wingi sana. Sasa baada ya ngoma hiyo kinachofuata ni maambukizi ya ukimwi. Pia kwenye makundi yoyote hasa ya sungusungu maambukizo haya yanakuwepo, alisema.
Aliongeza kuwa katika jimbo lake, hakuna suala la uzazi wa mpango na hivyo wananchi hao wanahitaji kupata zaidi elimu kuhusu suala hilo.
Mbunge wa Konde, Kaskazini- Pemba (CUF), Dk. Ali Tarab Ali, alisema kuwa katika jimbo lake kuna tatizo kubwa la vifo vya kina mama na watoto kutokana na ukosefu wa vituo vya afya.
Awali, Naibu Mkurugenzi wa Engender Health, Dk. Dunstan Bishanga, alisema kuwa baadhi ya tabia hatarishi zinazofanywa na wanaume zinachangia kuwepo kwa virusi vya ukimwi, ambapo athari kubwa zinawapata wanawake. Alisema wabunge wanatakiwa kuwa wakala wa mabadiliko katika masuala yahusuyo ukimwi na maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto.
Source
http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=14323
MBUNGE wa Viti Maalum, Janeth Massaburi (CCM), amebainisha kuwa mkoa wa Dar es Salaam, unaongoza kwa rushwa ya ngono hasa kipindi cha uchaguzi au mtu anapotaka uongozi.
Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es salaam kwenye semina ya ukimwi iliyoendeshwa na taasisi ya Engender Health kwa wabunge wa Kamati ya Bunge inayohusika na masuala ya ukimwi.
Massaburi alisema, mtu anayetaka nafasi ya kuongoza kwenye uchaguzi, kampuni binafsi na serikalini, ngono imekuwa ni sehemu ya kigezo cha kupata nafasi hizo.
Umaskini unasababisha rushwa ya ngono, mtu anapotaka nafasi yoyote ya kuongoza ili ajulikane, iwe ni kwenye kampuni binafsi, serikalini au katika kipindi cha uchaguzi anatakiwa atoe rushwa ya ngono.
Wasiwasi wangu watu wanafanya hivyo ili kupata cheo, hasa kwenye jimbo langu la Dar es Salaam ambalo nimeona hali hiyo ikijitokeza mara kwa mara, alisema Massaburi.
Aliongeza kuwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, wamekuwa wakijidanganya kuwa wana uelewa mkubwa wa ugonjwa huo wakati ukweli si huo.
Alishauri Engender Health iwatumie wabunge wa majimbo, viti maalumu na madiwani ili waweze kuwafikia wananchi kwa urahisi na kuwaelewesha kuhusu athari za ugonjwa wa ukimwi.
Naye mbunge wa Jimbo la Bukene, Teddy Kasella-Bantu (CCM), alisema katika jimbo lake ngoma na ulinzi wa sungusungu vinachangia kuwepo kwa ongezeko la ukimwi kwa kuwa wananchi hawana elimu ya kutosha.
Katika jimbo langu kuna kitu kama ngoma, ambazo zinakuwepo kwa wingi sana. Sasa baada ya ngoma hiyo kinachofuata ni maambukizi ya ukimwi. Pia kwenye makundi yoyote hasa ya sungusungu maambukizo haya yanakuwepo, alisema.
Aliongeza kuwa katika jimbo lake, hakuna suala la uzazi wa mpango na hivyo wananchi hao wanahitaji kupata zaidi elimu kuhusu suala hilo.
Mbunge wa Konde, Kaskazini- Pemba (CUF), Dk. Ali Tarab Ali, alisema kuwa katika jimbo lake kuna tatizo kubwa la vifo vya kina mama na watoto kutokana na ukosefu wa vituo vya afya.
Awali, Naibu Mkurugenzi wa Engender Health, Dk. Dunstan Bishanga, alisema kuwa baadhi ya tabia hatarishi zinazofanywa na wanaume zinachangia kuwepo kwa virusi vya ukimwi, ambapo athari kubwa zinawapata wanawake. Alisema wabunge wanatakiwa kuwa wakala wa mabadiliko katika masuala yahusuyo ukimwi na maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto.
Source
http://freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=14323