Dar es Salaam ibadilishwe jina

Dar es Salaam ibadilishwe jina

kiwiko

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2014
Posts
1,341
Reaction score
2,218
Habari wakuu,

Hili jina ni la jiji kubwa kuliko yote nchini cha kushangaza ni la Kiarabu wakati nchi ni ya kiafrika tena wabantu.

Kwakweli ili kulinda utambulisho wetu napendekeza jina libadilishwe liwe la kibantu kama mikoa mingine tena la kizaramo kabisa.

Haiingii akilini kuwa na jina la Kiarabu kwa mji wetu huu wa kibiashara.
 
Unasahau hata kiswahili unachokizungumza kina percent ya lugha ya kiarabu so km vp ungekuwa unaongea "kibantu" cha kwenu tu maana ndo utakuwa unatunza mila zenu.
Ni kweli ila kiswahili kimetohoa hayo maneno hivo hayapo kama yalivo kwa kiarabu yanatamkwa kibantu. Dar es Salaam imabaki kiarabu kabisa tofauti na maneno ya kiswahili yenye asili ya kiarabu.
 
Ni kweli ila kiswahili kimetohoa hayo maneno hivo hayapo kama yalivo kwa kiarabu yanatamkwa kibantu. Dar es Salaam imabaki kiarabu kabisa tofauti na maneno ya kiswahili yenye asili ya kiarabu.
Bro kasome vizuri historia ya kiswahili na historia ya neno "dar es salaam" kwa kifupi kwenye kiarabu hakuna kitu "es" kuna "el" sasa ukisema dar es salaam ni kiarabu pure utakuwa umewapoteza wandugu humu.
 
Habari wakuu. Hili jina ni la jiji kubwa kuliko yote nchini chakushangaza ni la kiarabu wakati nchi ni ya kiafrika tena wabantu.
Kwakweli ili kulinda utambulisho wetu napendekeza jina libadirishwe liwe la kibantu kama mikoa mingine tena la kizaramo kabisa.
Haiingiii akilini kuwa na jina la kiarabu kwa mji wetu huu wa kibiashara.
Lingekua Washington usinge sema libadirishwe kinacho kusumbua hapo ni roho mbaya ya ugalatia unashindwa kuangalia nini maana ya jina la dar es laaam sema sasa na ikulu ivunjwe kwa sababu imejengwa na waarabu
 
Bro kasome vizuri historia ya kiswahili na historia ya neno "dar es salaam" kwa kifupi kwenye kiarabu hakuna kitu "es" kuna "el" sasa ukisema dar es salaam ni kiarabu pure utakuwa umewapoteza wandugu humu.
Labda utueleze why kuna es badala ya el?? Why tupate mikanganyiko isiyo ya lazma
 
Lingekua Washington usinge sema libadirishwe kinacho kusumbua hapo ni roho mbaya ya ugalatia unashindwa kuangalia nini maana ya jina la dar es laaam sema sasa na ikulu ivunjwe kwa sababu imejengwa na waarabu
Ndugu yangu sio vizuri kuingiza udini kwenye hii mada. By the way wakati wa utawala wa wajerumani baadhi ya mikoa ilikua ina majina ya kijerumani ila baadae ilikuja kubadirishwa
 
Ndugu yangu sio vizuri kuingiza udini kwenye hii mada. By the way wakati wa utawala wa wajerumani baadhi ya mikoa ilikua ina majina ya kijerumani ila baadae ilikuja kubadirishwa
Huyu mtoa mada anachuki kashindwa tu kufunguka
 
Habari wakuu. Hili jina ni la jiji kubwa kuliko yote nchini chakushangaza ni la kiarabu wakati nchi ni ya kiafrika tena wabantu.
Kwakweli ili kulinda utambulisho wetu napendekeza jina libadirishwe liwe la kibantu kama mikoa mingine tena la kizaramo kabisa.
Haiingiii akilini kuwa na jina la kiarabu kwa mji wetu huu wa kibiashara.
Kwan ww unaitwa nan kwann usianze we kubadililako mbaguzi mkubwa
 
Lingekua Washington usinge sema libadirishwe kinacho kusumbua hapo ni roho mbaya ya ugalatia unashindwa kuangalia nini maana ya jina la dar es laaam sema sasa na ikulu ivunjwe kwa sababu imejengwa na waarabu
ikulu haijajengwa na waarabu, kisha uarabu si uislamu binafsi sipendi kabisa kubadilishwa hilo jina.

Na hata kubadilisha majengo ningependa yakarabatiwe tu, mji mpya ujengwe sehemu nyingine na kuitwa hayo majina yao.

Japo nalipenda jina MZIZIMA.
 
Back
Top Bottom