MamaBeata
JF-Expert Member
- Apr 15, 2013
- 325
- 112
Wadau samahani kama nitamkwaza mtu lakini binafsi sijapendezwa na zawadi zinazotolewa na shindano la dance 100 linaloendeshwa na channel 5 east Africa television.
Hebu fikiria washiriki wanatakiwa kuwa kundi la watu kuanzia 5-8. Mshindi anapata zawadi ya sh za kitanzania milioni tano. Wakigawana kila mmoja kwa kundi la watu watano kila mtu atachukua milioni moja. Na kama wako wengi zaidi kiasi kitapungua zaidi.
Nafikiri hii zawadi haiendani na effort iliotumika kwa washiriki. Kuna mazoezi yanayotakiwa kufanyika na pia gharama za sare nakadhalika. Yote hii uishie kupata milioni tano? Tena sio ya peke yako?
Najua watu wengine watasema kuwa group pia linapata faida nyingine ikiwemo promo ya kuwafanya wajulikane na wadau. Lakini bado washiriki hawatendewi haki. Mbona mashindano kama Bongo star search inatoa zawadi zinazoweza kubadilisha maisha ya Mshindi? Kwanini dance 100 watoe zawadi kiduchu wakati juhudi kubwa inahitahitajika ili ushinde?
Hebu fikiria washiriki wanatakiwa kuwa kundi la watu kuanzia 5-8. Mshindi anapata zawadi ya sh za kitanzania milioni tano. Wakigawana kila mmoja kwa kundi la watu watano kila mtu atachukua milioni moja. Na kama wako wengi zaidi kiasi kitapungua zaidi.
Nafikiri hii zawadi haiendani na effort iliotumika kwa washiriki. Kuna mazoezi yanayotakiwa kufanyika na pia gharama za sare nakadhalika. Yote hii uishie kupata milioni tano? Tena sio ya peke yako?
Najua watu wengine watasema kuwa group pia linapata faida nyingine ikiwemo promo ya kuwafanya wajulikane na wadau. Lakini bado washiriki hawatendewi haki. Mbona mashindano kama Bongo star search inatoa zawadi zinazoweza kubadilisha maisha ya Mshindi? Kwanini dance 100 watoe zawadi kiduchu wakati juhudi kubwa inahitahitajika ili ushinde?