Dan Alves wa Barca awajibu wabaguzi wa rangi kwa kula ndizi waliomrushia uwanjani

mwacheni77

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
763
209
Katika mechi ya Villarreal na Barca,mashabik wa Villarreal walionesha kitendo cha kibaguzi kwa kumtupia ndizi beki wa Barca, Dan Alves.

Ujasiri alioufanya alichukua ile ndizi akaimenya na kuila akapiga kona bahati nzuri ikamgusa beki wa Villarreal na kuwa goli.

Nimefurah maana kitendo hicho hakijamtoa mood ya mchezo.

==========
Daniel%20Alves_full.jpg

Beki wa pembeni kutoka nchini Brazil na klabu ya Barcelona, Dani Alves ameushangaza ulimwengu wa soka, kufuatia shukrani alizozitoa dhidi ya mashabiki wa klabu ya Villareal waliomtupia ndizi akiwa uwanjani usiku wa kumkia hii leo huko El Madriga.

Katika hali isiyotarajiwa Daniel Alvesa alifanya hivyo mara baada ya mchezo kati ya Barcelona na Villareal kumalizika huku Barca wakipata ushindi wa mabao matatu kwa mawili.

Alves, amesema kurushiwa ndizi akiwa uwanjani kwake anakichukulia kitendo hicho ni cha kawaida na anaamini wanaofanya hivyo ni mashabiki wenye upeo mdogo wa kufikiria ambao bado wanahitaji usaidizi wa kubadilishwa kimawazo.

Amesema ameishi nchini Hispania kwa miaka 11 na mara kadhaa wachezaji wenye asili ya bara la Afrika wamekua wakikutana na vitimbi kama hivyo, ambavyo vinaashiria ubaguzi wa rangi hali ambayo amesisitiza ameshaizoea.

Hata hivyo beki huyo mwenye umri wa miaka 30, kwa kuonyesha hajali masuala ya ubaguzi wa rangi, alidiriki kukata kipande cha ndizi aliyorushiwa uwanjani na kukila huku sehemu iliyo baki akiitupa pembezoni mwa uwanja wakati akijitayarisha kupiga mpira wa kona.

video hii hapa chini.

<strong>
 
Last edited by a moderator:
Dah Mkuu nimeipenda
ile ka risk maisha mpaka wamemtupia wangeweZa kumqekea simu kwenenye ndizi mwambie
 
Dawa ya jeuri ni kiburi.
Ndio manake umepatia siku nyingi nilikuwa nawaambia watu mtu akirusha ndizi chukua kula na ikiwezekana mngate kabisa mkono mkienda mahakamani sema mie si Monkey? Sie watu weusi asilimia kubwa hatuna roho za ubaguzi tungekuwa nazo tulikuwa tunauwezo wa kuita wengine nguruwe ila hatufanyi hivyo... Watu wenye kutenda zile tabia inakuwa wao ndio roho inaumia, wanataka mtu ukasirike sasa dawa ni kama alivyofanya Dani Alves alikuwa na uwezo hata wa kuwarushia ganda lao ila sababu mstaarabu katupia pembeni. Spain hutosikia Fine yoyote zaidi ya timu itapigwa fine Dola 2000 tu.
 
Duuuuuuuuuh wazungu noma sana na tabia hizi za kibaguzi lakini mbona sisi waafrika hatuna tabia hizi au na sisi tunakbali kuwa wazungu ni wazuri???? mbona wapo wazungu ambao ukiwaangalia sura zao kama nguruwe mfano yule mchezaji wa man united cjui anaitwa ruuuuuuuuuuuuuni.........
 
Huo ndio ukomavu kisaikolojia kwa wachezaji, sio sie kukimbilia kutoa taulo la kipa golini kusingizia kuzuia goli lisiingie!!!!!!!!!
 
Hahahaa kk unatafuta ugomvi na wenye timu yao.
Mkuu, huu ndio ukweli tupu uliopo, TUMEONA na si kusimuliwa na mtangazaji. Ni aibu sana na bahati mbaya sijasikia tamko lolote toka TFF japo kukikemea tu kitendo hicho. Hatuwezi kuwa na wachezaji wenye imani ya uchawi ili kuhalalisha uzembe wao uwanjani.
 
Ndio manake umepatia siku nyingi nilikuwa nawaambia watu mtu akirusha ndizi chukua kula na ikiwezekana mngate kabisa mkono mkienda mahakamani sema mie si Monkey? Sie watu weusi asilimia kubwa hatuna roho za ubaguzi tungekuwa nazo tulikuwa tunauwezo wa kuita wengine nguruwe ila hatufanyi hivyo... Watu wenye kutenda zile tabia inakuwa wao ndio roho inaumia, wanataka mtu ukasirike sasa dawa ni kama alivyofanya Dani Alves alikuwa na uwezo hata wa kuwarushia ganda lao ila sababu mstaarabu katupia pembeni. Spain hutosikia Fine yoyote zaidi ya timu itapigwa fine Dola 2000 tu.


waSpanish m.a.n.i.n.a zaoo...wao ndio watu watu wa kwanza duniani kupeleka watumwa bara lingine Americas..personally
I hate them,their league,their national team na team zao..ni msakini wa jabu Ulaya,wavivu,wainga
ila wanajidai...natamani ningewemwagia mitusi hapa but naogopa ban

Kudos Alves..
 
Daniel%20Alves_full.jpg
Beki wa pembeni kutoka nchini Brazil na klabu ya Barcelona, Dani Alves ameushangaza ulimwengu wa soka, kufuatia shukrani alizozitoa dhidi ya mashabiki wa klabu ya Villareal waliomtupia ndizi akiwa uwanjani usiku wa kumkia hii leo huko El Madriga.

Katika hali isiyotarajiwa Daniel Alvesa alifanya hivyo mara baada ya mchezo kati ya Barcelona na Villareal kumalizika huku Barca wakipata ushindi wa mabao matatu kwa mawili.

Alves, amesema kurushiwa ndizi akiwa uwanjani kwake anakichukulia kitendo hicho ni cha kawaida na anaamini wanaofanya hivyo ni mashabiki wenye upeo mdogo wa kufikiria ambao bado wanahitaji usaidizi wa kubadilishwa kimawazo.

Amesema ameishi nchini Hispania kwa miaka 11 na mara kadhaa wachezaji wenye asili ya bara la Afrika wamekua wakikutana na vitimbi kama hivyo, ambavyo vinaashiria ubaguzi wa rangi hali ambayo amesisitiza ameshaizoea.

Hata hivyo beki huyo mwenye umri wa miaka 30, kwa kuonyesha hajali masuala ya ubaguzi wa rangi, alidiriki kukata kipande cha ndizi aliyorushiwa uwanjani na kukila huku sehemu iliyo baki akiitupa pembezoni mwa uwanja wakati akijitayarisha kupiga mpira wa kona.

video hii hapa chini.

<strong>
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom