Uchaguzi 2020 Dalili zote zinaonesha anga limeikataa CCM

Lusungo

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
27,124
39,337
Wahenga walisema dalili ya mvua ni mawingu na mwanzo wa ngoma ni lele!

Kuelekea Oktoba 28 dalili zote zinaonesha CCM kukataliwa na anga la Tanzania.

Kutakua na matukio mengi mfululizo kuelekea Oktoba 28 na kuendelea huko mbele hata kama Magufuli atashinda ambayo yatabadili kabisa mwelekeo na upepo wa CCM dhidi ya upinzani.

CCM imeishiwa pumzi kabisa na kwa wataalamu wa alama za nyota tunaweza thibitisha hili kwamba upepo si mzuri kwa CCM na ile 'hewa' imeondoka kwenye paa la CCM!

Siuoni uhai wa CCM kunanzia 2020 na kuendelea ni suala la muda tuu huu uzi utakua kama rejea.

Namba hazikubali kwa CCM na kwa mazingira haya Tanzania inakwenda kuandika historia mpya!

Mungu awabariki.
 
Mkuu, hata mfanya mazingaombwe huwa anaishiwa tricks ... na hapo ndipo panakuwa mwisho wa maonyesho.

Kwa kweli CCM is running out of tricks. New tricks are required for them to survive in this game. This time around naamini watashinda kwa ubabe ... lakini by 2025 haitawezekana. I can imagine wagombea wa CCM 2025 ..... Mwigulu, Kigwa, January, Makonda, Tulia, Polepole, Bashiru, Kabudi .... Tuombee Corona isituchafulie hewa!!
 
Haya ndio matokeo ya kufanya research kupitia coment za hapa jf na kwenye magroup ya chadema!

Tz ni kubwa jamani hawa walioko huku mitandaoni ni tone tu!

Kingine nmeona kwenye post za BBC kule facebook kuhusu Lisu, coment za raia wengi wa kule upepo haupo kwa Lisu kabisa.
 
Haya ndio matokeo ya kufanya research kupitia coment za hapa jf na kwenye magroup ya chadema!

Tz ni kubwa jamani hawa walioko huku mitandaoni ni tone tu!

Kingine nmeona kwenye post za BBC kule facebook kuhusu Lisu, coment za raia wengi wa kule upepo haupo kwa Lisu kabisa.
Huku kwetu nderemo na vifijo vilitamalaki jana. Japo hakuna aliyeona habari za Lissu kwenye TV lakini watu walirushiana clips kwenye simu.

Bia zilikwisha grocery ilitulazimu kulala saa saba usiku.
 
Ccm inabebwa na vyombo vya dola, ccm bila kubebwa kwisha

Vyombo vya Dola badala ya nchi - Urais (soma hayo maandishi kwenye mkoba husika). Vyomb vya dola ni sehemu ya Urais, lakini Urais ni mpango mzima. Sasa iweje kuwania kuongoza vyomb vya dola badala ya nchi? Lakini, wa Zanzibar ni Urais! (tazama chini)

1596535903939.png


1596536049771.png
 
Huku kwetu nderemo na vifijo vilitamalaki jana. Japo hakuna aliyeona habari za Lissu kwenye TV lakini watu waliruahiana clips kwenye simu.

Biazilikwisha grocery ilitulazimu kulala saa saba usiku.
Kwenu wapi mkuu? Mbona huku kwetu hamna kitu? Na ndio wapiga kura walikojaa?
 
Back
Top Bottom