Uchaguzi 2020 Dalili ya mvua ni mawingu. Vyama vya upinzani vimekubali kushindwa kabla ya mtanange kupigwa

You are very corrupt at the chronic level
Wahenga walisema ukiona wingu zito limetanda angani ujue kuna mvua kubwa inakuja kunyesha hivyo chukua tahadhari na tafuta mahala salama ujikinge. Siku zinazidi kuyoyoma na wapinzani wa CCM ndio wanazidi kunywea maana wanajua kwenye uchaguzi wanaenda kukutana na kichapo cha ukweli.

Ninajua wanajiuliza majukwaani watanadi sera gani? Wanakosa majibu. Wanajiuliza tukisimamisha wagombea wa ubunge wanakosa majibu nani atafaaa au nani atarudi tena. Wamekuwa wa baridi na hatusikii hata dalili za watia nia wao maana kila jimbo ni kama kuna shoti ya umeme na wanaogopa kuweka mkono.

Lakini nini hasa sababu ya haya yote? Ni uadilifu, uchapakazi na uzalendo wa JPM ndio umeipa nguvu na kiburi CCM na sasa ina uhakika wa kuchukua kiti cha ubunge au udiwani katika eneo lolote. Maana ni ndani ya miaka minne tu, watu wameshuhudia mabadiliko makubwa sana.

Sekta ya afya, elimu, miundombinu na ulinzi na usalama zote zimeimalishwa. Wapinzani uchwara wanaona aibu tu kukubali na kukaa kando. Lakini wangekuwa na busara wangetulia na kukaa kando.
 
Kwasababu siko kwenye njia unayoiamini, basi unataka kuharibu haiba yangu, ili ionekane naongozwa na hisia na ushabiki wa kisiasa. Ninajitambua vya kutosha, na wala sitoki nje ya ukweli. Ww unaweza kuamini au kutetea unachoamini, kwakuwa una maslahi binafsi na utawala huu, lakini akija mtu akasimamia ukweli, bado majibu yake yatakuwa kama ninavyokuambia.
Sina maslahi yoyote naeleza ukweli wa mambo ambao kila mtu anauona.
 
Hayo ya tume ya uchaguzi na marufuku ya siasa ni uongo tu. Tume ipo huru na huwa inafuata taratibu na sheria za nchi. Kufanya siasa mliruhusiwa ngazi za majimbo msilete mtafaruku kitaifa.
wee bwege taja mmoja kwenye tume ya uchaguzi ambae sio kada wa CCM just one
 
Sio kweli mahakama zipo huru. Wewe uwe na ushahidi na uthibitisho utafanikiwa tu.
mzee wacha bangi sio nzuri kwa afya yako hivi wewe bwege kiasi gani huoni wale masheikh leo ni mwaka 6 eti ushahidi haujakamilika ivi engekuwa kuna jaji waamaana si keshaifutiliyua mbali kesi hiyo kama mahkama ni huru.
 
Onghwise , mapenzi mabaya sana .

Mbona mshindanaji mwenyewe kashika kipenga, mpira anao na golini anafunga mwenyewe ?!. Unataka ushindani wa sera na wagombea, basi uwanja uwe leveled na wote wawe na haki Sawa mbele za wananchi . Siyo hii ya sasa moja anabebwa na vyombo, wakati wengine wanadhalilishwa na vyombo hivyo hivyo.

Wewe ni mwenyeji wa kanda yetu . Unaweza kuniambia kuna nini kipya tofauti na awamu zilizopita ?!. Labda kidogo wilaya fulani kule geita. Vinginevyo nothing
 
Na huyu anayeimbwa na wasanii wote , unadhani yeye anafanya nini ?!. Mbona ukweli unaukataa
 
Onghwise , mapenzi mabaya sana .

Mbona mshindanaji mwenyewe kashika kipenga, mpira anao na golini anafunga mwenyewe ?!. Unataka ushindani wa sera na wagombea, basi uwanja uwe leveled na wote wawe na haki Sawa mbele za wananchi . Siyo hii ya sasa moja anabebwa na vyombo, wakati wengine wanadhalilishwa na vyombo hivyo hivyo.

Wewe ni mwenyeji wa kanda yetu . Unaweza kuniambia kuna nini kipya tofauti na awamu zilizopita ?!. Labda kidogo wilaya fulani kule geita. Vinginevyo nothing
Jaduong habari za kusingizia kuminywa kwa demokrasia ni uongo tu. Watanzania wanaangalia nini Ccm imefanya chini ya JPM na maendeleo yamesambazwa Tanzania nzima bila upendeleo. Ndio maana ile hospital ya mkoa wa Mara kule kwenu imekamilika baada ya miaka zaidi ya 30. Kwa hiyo unastahili upongeze.
 
Onghwise , mapenzi mabaya sana .

Mbona mshindanaji mwenyewe kashika kipenga, mpira anao na golini anafunga mwenyewe ?!. Unataka ushindani wa sera na wagombea, basi uwanja uwe leveled na wote wawe na haki Sawa mbele za wananchi . Siyo hii ya sasa moja anabebwa na vyombo, wakati wengine wanadhalilishwa na vyombo hivyo hivyo.

Wewe ni mwenyeji wa kanda yetu . Unaweza kuniambia kuna nini kipya tofauti na awamu zilizopita ?!. Labda kidogo wilaya fulani kule geita. Vinginevyo nothing
Juzi karudisha fomu akiwa na msafara wa kufa mtu,vyombo vyote vya serikali ndiyo vilikuwa vinaratibu na kuhakikisha lengo linatimia.Naye bila kukosea akapiga kampeni yake rasmi na kuruhusu wengine waanze michakato ya ndani ya chama.Sikumbuki lini fomu za chama zimeanza kutolewa kwa vipindi tofauti yaani za Urais,Ubunge na Udiwani.Huu nao ni utaratibu wa CCM Mpya?
 
Hayo ya tume ya uchaguzi na marufuku ya siasa ni uongo tu. Tume ipo huru na huwa inafuata taratibu na sheria za nchi. Kufanya siasa mliruhusiwa ngazi za majimbo msilete mtafaruku kitaifa.
Tume inayoongozwa na makada wa CCM inawezaje kuteñda uadilifu?
Just imagine jinsi CUF ilivyohujumiwa na tume ya jecha miaka ya nyuma afu Jecha huyo huyo anasimama kama mtia nia wa ÇCM.
Kama hujaelewa somo rudi shule kaka/dada
 
Juzi karudisha fomu akiwa na msafara wa kufa mtu,vyombo vyote vya serikali ndiyo vilikuwa vinaratibu na kuhakikisha lengo linatimia.Naye bila kukosea akapiga kampeni yake rasmi na kuruhusu wengine waanze michakato ya ndani ya chama.Sikumbuki lini fomu za chama zimeanza kutolewa kwa vipindi tofauti yaani za Urais,Ubunge na Udiwani.Huu nao ni utaratibu wa CCM Mpya?
Kuna CCM MPYA, CCM ASILI NA CCM MASALIA....
Wote wamo kwenye kapu moja la samaki wabovu!!
 
Back
Top Bottom