Dalili kwamba umenenepa

Dalili kwamba umenenepa

Author

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2014
Posts
1,745
Reaction score
8,222
Wakati huu wa mapumziko watu tuleeee... tunywe... Ila tukumbumbushane mambo kadhaa... Dalili ambazo zitakusaidia kufahamu kuwa unaongezeka uzito/unene ni;

1. Kula sana zaidi ya kiasi ulichokuwa unakula kipindi cha nyuma kutokana na kuwa na njaa mara kwa mara.

2. Nguo kubana; yaani hapa unajaribisha nguo kama zote kabla hujaamua ipi ya kuvaa wakati wa kutoka.

3. Kujamba sana na mara kwa mara (hata ukiwa umelala)

4. Watu wa karibu nawe au wanaokufahamu kuamza kukuita bonge.

5. Ngozi kung'aa; hapa ni kutokana na mwili kuongezeka.

Nyingine wadau muongezee wenyewe....
 
Sili mchana siku hizi kukwepa maneno ya Mbona umenenepa sana..Kila ninaekutana nae hakuna kipya zaidi ya hilo swali
 
Hamna siyo kivile mkuu shida nipo uswahilini so ukitoka shavu kidogo tuu unaitwa umenenepa ili. Utwasikia wakisema " Naona mambo so mabaya...tupeane michongo...." Ukisema sina issue anakwambia hakuna mwili unaokuja bila kula vizuri...hahaaaaaa....
 
Kuanza kuhisi uchovu na mwili kuwa mzito,kupenda kulala lala,ukipiga kimoja ukigeukia ukuta kuamka ni Kesho saa mbili tena Kwa msaada wa alarm
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom