Dalili kuwa mtoto wako anatumika kingono

Dalili kuwa mtoto wako anatumika kingono

snowhite

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
18,422
Reaction score
25,322
child.png

WATOTO WANATUMIKA KINGONO!
Inaumiza lakini ndio uhalisia! sio kitu kinapendeza machoni wala akili lakini ndio ukweli!

Watoto wetu hawako salama!

Hawako salama sio kwa watu tunaoamini sio salama.

Watoto hawako salama kwa watu tunaoamini wako salama!

Kuna vitu tu lazima kama jamii tuambiane na tuinue sauti kuvizungumza!

Unyanyasaji kingono miongoni mwa watoto ni jambo ambalo lipo, linafanyika, linatendeka under our very noses!

Ni vile tu hatuamini na tunafikiri wapo salama! ni vile tu tunaamini sio kitu kinaweza kutokea kwa wanetu! ni vile tu tunaamini wapo watoto aina fulani wa kufanyiwa hayo!

Sio kweli!

Sio kweli!

Sio kweli!

Leo hebu tushirikishane dalili ambazo zinaweza kuwa taarifa kuwa mtoto anatumika kingono.

Unyanyasaji kingono umekuwa ni sehemu ya historia za maisha ya baadhi yetu.

Matukio yote unayokumbuka ulifanyiwa ukiwa mdogo ambayo leo ukiwa mtu mzima unaweza kuyahusisha na matukio ya kingono na hukusema ndiyo hayo yanaweza kuwa yanamtokea mtoto sasa na hasemi.

nyingine ni

  1. Mtoto anapata shida kukaa au kutembea (2 - 10yrs)
  2. Anaogopa kupita kiasi baadhi ya watu, mahali au vitu (0-5yrs)
  3. Anapenda kujishika sehemu za siri kiasi cha kujisahau mpk kulala akiwa anajishika.
  4. Anakaa chooni muda mrefu au kuhitaji kujisaidia mara kwa mara.(0-5yrs)
  5. Anaweweseka usiku (0-5yrs)
  6. Anakataa/kusumbua kula au kutapika bila ugonjwa mahsusi. (0-5yrs)
  7. Analia sana (0-3yrs )
  8. Anaona aibu na kujitenga (umri wote)
  9. Anashindwa kuzuia haja kubwa (4-7yrs)
  10. Anakuwa mkimya isivyo kawaida (umri wa balehe)
  11. Anashuka kielimu (6-17)
  12. Anakuwa na kiburi, maamuzi ya kukinzana na maagizo( umri wa balehe)
  13. Mimba (11-17)
  14. Majaribio ya kujiua (8- 17)
  15. Anakimbia nyumbani mara kwa mara (8-17)
  16. Msongo wa mawazo (8-17)
  17. Anakataa kushiriki shughuli za nyumbani, za shule, za kiroho. (7-17)
Ongeza zingine na tushauriane cha kufanya!

Hali sio nzuri!

Sio nzuri kabisa!

cc sema tanzania
 
Nakumbuka nikiwa kama 4-5 yrs hivi nilishaanza kulalana na binti mmoja hivi anaitwa mariam alikua chumba cha jirani,,tulikua tunavizia mama zetu wakitoka kwenda sokoni au clinic na mchezo ulikua mtamu hasa,,,,,baadae tulijahama na hatujaonana ten 27+ yrs now na hata simkumbuki sura tena ila alikua mtam sana
 
nkumbuka nikiwa kama 4-5 yrs hivi nilishaanza kulalana na binti mmoja hivi anaitwa mariam alikua chumba cha jirani,,tulikua tunavizia mama zetu wakitoka kwenda sokoni au clinic na mchezo ulikua mtamu hasa,,,,,baadae tulijahama na hatujaonana ten 27+ yrs now na hata simkumbuki sura tena ila alikua mtam sana
hahaha asante kwa kuchangia hahaa
 
Sexual abuse kwa watoto ina lasting effects.

Mimi natoka nje ya mada.

R Kelly ni matunda ya sexual abuse.

Ndoa nyingi kutetereka kwake ni sexual abuse.

Mahusiano na mtu aliyeexperience sexual abuse hua hayana afya, haswa kama hakuna tiba aliyoipata.

Pia effects zake hua complicated.
Mfano kuna babu alikua anawaabuse sexually wajukuu zake wawili. Mmoja akawa anamuingilia mwingine hamuingilii.

Akili ya kawaida inasema ambaye kaingiliwa ndiyo inabidi akumbwe na effects kubwa zaidi lakini katika kesi hii ambaye hakuingiliwa ndiyo alikua na effects kubwa kuliko.
Kutoingiliwa kulimfanya ajihisi hatoshi, hafai na mchafu hivyo aliishi maisha yake akijaribu kucompensate kwa kujirahisisha kwa wanaume na kufanya ngono na kila mwanaume kutokana na hiyo perception.

Tuwasaidie.
 
Ahaaa, aliyesema mudy kaleta hayo amekosea.
Hajakosea " kwa sababu kuna Theory zinasema kuwa alimuoa bi aisha akiwa na umri wa miaka 9....

Sasa hauoni kuwa kama ni kweli basi baadhi ya Wafuasi wake nao wapo katika mkumbo wa kuiga hilo !!? Nadhani unaijua nguvu aliyonayo Public figure yeyote yule kwa wafuasi wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiukweli watoto wetu hawako salama sio wa kike sio wa kiume, hali inatisha jamani inahitajika nguvu ya ziada mnooo ,leo kuna mama mmoja anatuuziaga ndizi hapa kazini, alipotea almost mwezi mzima leo kaja tukamuuliza vp huonekani anasema mtoto wake wa 5 yrs amebakwa na baba mtu mzima tena mwenye familia na watoto juu.anaongea hadi analia, mtoto kaharibiwa hafai, niliwaza, nkajikuta nalia ,unajiuliza baba mtu mzima anabaka mtoto mdogo anapata hamu gani, ni wap yule mtoto anaweza mtamanisha,yaani ahaa basi tu
 
Sexual abuse kwa watoto ina lasting effects.

Mimi natoka nje ya mada.

R Kelly ni matunda ya sexual abuse.

Ndoa nyingi kutetereka kwake ni sexual abuse.

Mahusiano na mtu aliyeexperience sexual abuse hua hayana afya, haswa kama hakuna tiba aliyoipata.

Pia effects zake hua complicated.
Mfano kuna babu alikua anawaabuse sexually wajukuu zake wawili. Mmoja akawa anamuingilia mwingine hamuingilii.

Akili ya kawaida inasema ambaye kaingiliwa ndiyo inabidi akumbwe na effects kubwa zaidi lakini katika kesi hii ambaye hakuingiliwa ndiyo alikua na effects kubwa kuliko.
Kutoingiliwa kulimfanya ajihisi hatoshi, hafai na mchafu hivyo aliishi maisha yake akijaribu kucompensate kwa kujirahisisha kwa wanaume na kufanya ngono na kila mwanaume kutokana na hiyo perception.

Tuwasaidie.
Hujatoka nje ya mada mkwe!
ahsante sana kwa kushare umenipe perspective nyingine sikuwahi ifikiria aisee!
 
Back
Top Bottom