Dalili kumi za msichana anaye kucheat

Dalili kumi za msichana anaye kucheat

tutafikatu

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2011
Posts
3,425
Reaction score
4,773
1. Anaficha hisia zake:
Anaweza akakwambia kila kitu, lakini asikwambie jinsi siku yake ilivyokuwa, hapo kuna uwezekano mkubwa huwa anamweleza mwanaume mwingine. Kama hakuambii kuhusu masahibu yanayomuudhi, furaha zake na huzuni, una sababu ya kuwa na hasira.

2. Hayuko wazi:
Tuwe wakweli, wanawake wako wazi zaidi ya wanaume. Lakini ukikuta mwanamke katulia kama mtungi na mara chache anachukizwa na wewe, uwe na hofu asije akawa mahusiano ya kimwili au emotional na mwanaume mwingine.

3. Anaficha au kufunika simu au kutoa mlio wa sauti muda wote:
Mtu huyu ukimuuliza, atakwambia kwani yako ninashikaga? Atadai watu wanaopendana wanaaminiana. Wasiopendana hawaaminiani.

4. Hazungumzii mengi ya makusanyiko ya watu alipoenda:
Labda anapenda kwenda sana harusinu, akikuacha wewe, hatokueleza kilichotokea huko maana labda kuna mtu anaongozana naye, au anakuwa amepata muda wa kuwa na mawasiliano na huyo ampendaye.

5. Huwa hawi na 'mudi':
kama katika mahusiano yenu wewe ndio umekuwa waanza kuomba tendo la ndoa mara zote ujue umeliwa. Kama hukumbuki lini mlifanya mapenzi na wala yeye hajali una haki kuwa na wasiwasi naye.Mwanamke anapokuwa amepunguza hamu ya tendo la ndoa au kuonana ana kwa ana ujue mapenzi yake yapo sehemu nyingine.

6. Ghafla kabadiri mwonekano wa nje: Japo ni kitu cha kawaida kujipamba kimavazi, nywele, viatu n.k. Lakini kuna mabadiriko yasiyo ya kawaida ambayo yanaweza yakawa dalili za yeye kuanzisha mahusiano mapya.

7. Anadhani hujiamini: Mwanamke akiwa na hisia za wewe kutojiamini una haki ya kuwa na shaka kwamba ana mahusiano na mwanaume mwingine.

8. Hajali matokeo ya kile anachojibu:
Mwanamke ambaye ana majibu yasiyo ya kuridhisha na mafupi mara nyingi anaonesha kutojali. Hisia zake zinaweza zikawa sehemu nyingine. Mfano anakujibu amini utakalo.

9. Hataki um follow kwenye social media kama facebook, Instagram, Twitter: Maana kuna vitu anaficha.

10. Anashinda Whatsapp au Viber huku aki ignore text zako. Na ama anatuma sana sms kwenda kusikifahamika hata mkiwa pamoja.
 
Tutafikatu,upo sawa kabisa mkuu na nimekupata vizuri tu.
 
Dah Mbona kila mwanamke ninae kuwa nae anakuwa na hizi tabia,kumbe wote ni wazabizabina tu sijui kwa nini sasa
 
Mkuu umeongea kweli kabisa nilikua na mpenzi wangu ambae nilikua nimesha enda kwao kujitambulisha na process nyingine nilikua nimesha fanya ilikua imebaki mahali tu

mabadiliko yakaanza mara nyingi sana alikua akinibana kufanya mapenzi pindi anapo kuwa na ham tu alikua ananipigia simu mfurulizo siku ambyo nimepata muda wa kushinda nyumbani lazima aje vilevile sms zangu kwenye simu alikua hafuti hata mimi nilikua sifuti sms zake

Ghafla akawa si mtu wa kunibana kama mwanzo mpaka mimi niamwambie aje wakati mwengine mpaka nianze kumbembeleza mara nkikagua simu yake sehemu ya sms nakuta empty nikanza kua na wasiwasi nikaanza kumfuatilia taratibu bila yeye kujua mwisho wa siku nikagundua ana cheat na nikapata habari zake zote kutoka kwa rafiki yake wa karibu.

Kipindi chote cha mwaka mmoja na nusu kwenye mahusiano yetu alikua hana mtu ndo mana alikua karibu sana na mimi ila mara tu alipoa anzisha uhusiano na mwanaume mwengine ndo mabadiliko yakaanza nilicho fanya nilimuita nyumbani nikamuambia mambo yake yote ndo ikawa mwisho wa uchumba wetu.

Baadae rafiki yake akaniambia jamaa kamtema kipindi hicho alianza kunisumbua akitaka turudiane nae ukiwa kwenye mahusiano kunavitu inabdi uvifuatilie ukiona mabadiliko chukua hatua mapema
 
Uko sahihi ukiona hizo dalili toka nduki.
 
tutafikatu

Huwa ha-appreciate! Hata umfanyie nini bado malalamiko yatakuwepo tu!! Yaan kifupi akiwa anakucheat hawezi kuridhishwa na lolote lile utalomfanyia!!
 
Last edited by a moderator:
Sijui mi ndo nakaribia kushinda vita yake ya mapenzi mbona kama dalili zote hana,au niendelee kumchunguza mambo yakibadilika nakuja nami kuongezea.
 
Back
Top Bottom