Daktari Mgiriki auawa Tanzania

Daktari Mgiriki auawa Tanzania

taarifa nilizonazo, tena za uhakika ni kuwa vibaka wanaofanya wizi wa aina hii ni watoto wa vigogo wa serikali ya sasa.

Inawezekana kabisa, cha msingi ni kuhakikisha wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
 
yes, i am, fuatilia hata vijana hodari wa kuiba magari na vitu vilivyoko ndani ya magari pale mlimani city ni watoto wa vogogo. Kuna mob ambayo ukijiuliza kwa hali ya kawaida utadhni ni rahisi kuwakamata, bali jeshi la polisi halihangaiki nalo. Jiulize, moja ya maeneo yaliyoanza muda mrefu kuwa na uharifu wa aina hii ni pembezoni mwa IKULU NA KIJITONYAMA, karibu kabisa na makazi ya maofisa wa usalama wa taifa. Polisi hawathubutu kuwabugudhi.



Duh! Basi tumekwisha mkuu!
 
Watanzania wangapi wanawauwa kule ugiriki mbona si kioja au ni pale anapokufa mzungu? hii mijamaa mibaguzi wameshawatoa roho ndugu zetu wengi bila sababu.... nadhani watz sasa waliowai kuishi ugiriki wanahaki ya kulipiza,,,

Naomba utoe data hapa za waliouawa kibaguzi, sina shaka ni wazamiaji ( na japo I don't support it ) ila najua mabaharia hurusha wazamiaji majini na wote wanajua wakidakwa ndio hivyo..

Huyu amekuja kama doctor wa kujitolea ametumia taaluma yake vizuri na hata angekuwa mtalii au missiontown ana haki ya kuishi

Tuache mambo ya jino kwa jino
 
Maeneo ya city centre hasa ocean road ukipita usiku ni hatari sana.Uwe kwa miguu au kwa gari ni hatari sana.Kinachoshangaza ni kwamba kituo cha polisi kipo jirani lakini hawa waharifu hata hawashughulikiwi.Kwa nini kusiwe na doria maeneo yote hatari??Na huu uporaji wa kutumia magari upo sana hapa mjini.Kuna tukio kama hilo la wanafunzi wawili wa IFM kwa nyakati tofauti waliporwa laptop zao na kuburuzwa kwenye barabara pindi tu wanapotoka getini.Swali,je hili tatizo la waporaji wa kutumia magari na wale wa kukaba watu maeneo ya ocean road,daraja la sallender na maeneo mengine city centre utaisha lini???
Mi kuna jamaa yangu alipata pancha daraja la salenda aliposhuka wakatokea watu vichakani wakamtwanga shoka la goti ukifikiria mita chache kuna kituo cha polisi labda kuipa uzito hiyo habari itawaamsha watu wengine maana polisi wetu wanaonyesha ukakamavu pale tu wanapodhibiti maandamano ya kisiasa
 
Sasa polisi wanasemaje? Au walikuwa busy kudhibiti mikutano ya CDM?
 
Watanzania wangapi wanawauwa kule ugiriki mbona si kioja au ni pale anapokufa mzungu? hii mijamaa mibaguzi wameshawatoa roho ndugu zetu wengi bila sababu.... nadhani watz sasa waliowai kuishi ugiriki wanahaki ya kulipiza,,,
it is very sad mkuu, lakini je dini zinatufundisha kisasi??

maswali mengine bora niweke pembeni usije kusema i am insensitive
 
Hapa ni tatizo la nchi kugeuka ya vibaka. Mibaka inaiba huko juu kiasi cha kutengeneza vibaka wengine ambapo hawachukuliwi sheria kutokana na kwamba wote ni vibaka. Angalia hata tunavyojenga majumba yetu mikuta kibao badala ya kuondoa umaskini na kuleta uwajibikaji. Leo jitu linaiba kesho linajiita milionea na hakuna anayeliuliza lilivyochuma hiyo pesa. Matokeo yake kila mtu anatafuta njia ya kupata pesa ili aheshimike. Heri aliyeuawa angekuwa mke au binti wa mkubwa nadhani wangetia akili.

siyo sehemu ya kucheka,ila uliposema mibaka ya huko juu inatengeneza vibaka!,nmejikuta nacheka. Rip marehemu
 
Nimevuta pumzi kwa uchungu mkubwa sana, INNA LILLAH ...sote sisi ni wa Mwenye ez Mungu na kwake ndio marejeo yetu ... pole sana kwa familia naye alie juu awafariji Amin.
 
swts huo ndiyo ukweli ingwa ni mchungu. Leo utasikia rais akisema kuwa Andrew Chenge kwa mfano si fisadi. Kesho unasikia mke wake ametapeli watu. Leo tuna Edward Lowassa anayeendelea kulipwa pesa ya kustaafu kama waziri mkuu wakati hakustaafu zaidi ya kuliingiza taifa kwenye kiza. Kwa vile ni mshirika wa Kikwete kwenye mazabe yao nani atamgusa? Unategemea nini toka kwenye serikali iliyoingia madarakani kwa pesa ya ujambazi wa EPA na ikaingia kwa mara ya pili kupitia ujambazi wa Richmond na uchakachuaji?
 
Aibu, aibu, shame. Hao wazungu watatoa taarifa gani kuhusu Tanzania? Ni aibu sana.
 
Umenena vyema Nsiande, tuache mambo ya jino kwa jino, huyu ametumia taaluma yake kutusaidia, kumbuka bado ratio ya doctor😛atient Tanzania ni 1:25,000. Mungu amlaze pema peponi

Naomba utoe data hapa za waliouawa kibaguzi, sina shaka ni wazamiaji ( na japo I don't support it ) ila najua mabaharia hurusha wazamiaji majini na wote wanajua wakidakwa ndio hivyo..

Huyu amekuja kama doctor wa kujitolea ametumia taaluma yake vizuri na hata angekuwa mtalii au missiontown ana haki ya kuishi

Tuache mambo ya jino kwa jino
 
Last edited by a moderator:
Greek Official Dies in Tanzania After Attack

Hatzipadazi1.jpeg


A Greek doctor who was working for the Greek Ministry of Foreign Affairs in Tanzania died following an attack by unknown men who tried to steal her hand bag, officials said. Petroula Hatzipantazi passed away on Sept. 25 from her injuries.

Authorities said that the unknown perpetrators were driving a car when they attacked Hatzipantazi and in their attempt to take her bag caused her serious injuries. She was immediately transported to a hospital but doctors could not keep her alive.

According to the official announcement of the Greek Ministry, Hatzipantazi was on a special mission of the Patriarchate of Alexandria in Tanzania.

Her colleagues and the Ministry described her as a professional official who offered her knowledge on hygiene and support to her co-workers as a doctor. The Ministry and her colleagues expressed their condolences to Hatzipantazi's family.


Source: greekreporter
 
Back
Top Bottom