Kama bado hujajua kwamba Yesu ni Mungu, soma uzi huu:
1. Ushahidi wa Kibiblia Yohana 1:1 – "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu." Tito 2:13 – "Tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Mungu mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo." Yesu mwenyewe alikiri kuwa ni Mungu: Yohana 10:30 – "Mimi...
www.jamiiforums.com
Hebu tumia akili basi, bibilia yenu inasema; Mwanzo alikuwa Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, na Mungu alikuwa Neno.
Sawa hebu tutumie akili na hoja hapa.
Neno alikuwa pamoja na Mungu
Sawa sasa tunaye Yesu Pamoja na Mungu.
Kwa hiyo Yesu sasa yupo Pamoja na Mungu ambayo inaonyesha wazi hawafanani hapa kati ya hao wawili.
Sasa Yesu ametuambia kuwa Baba yake alikuwa Mungu wake.
Ninapaa kwenda kwa Baba yangu na Baba yenu; na kwa Mungu wangu, na Mungu wenu. Yohana 20:17
Kwa hiyo sasa tunaye Yesu pamoja na Baba yake.
Naye Neno alikuwa Mungu.
Kwa hivyo hii ni kusema kwamba Yesu alikuwa Baba yake? Bila shaka sivyo.
Sasa kwa kusema Neno lilikuwa (A) Mungu angekuwa na maana kama Yesu alivyoitwa Mungu Mwenye Nguvu kwenye Isaya 9:6
yeye hapo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Yohana 1:2
Sasa angalia neno Pamoja na limetumika tena kwa Yesu alikuwa (Pamoja)Mungu akionyesha kwa uwazi hawa wawili (Tofauti)