Raimundo
JF-Expert Member
- May 23, 2009
- 13,415
- 12,622
Nakupa version rahisi, ambayo unaweza kuitumia kutongozea.
Kama huwa unakutana naye na ynamsalimia ni vizuri, mwombe namba yake ya simu yeye mwenyewe, mweleze kiutani tu kwamba kuna mida unatakaga kumsalimia ila humwoni, hivyo ni vema uwe na namba unaweza kumjulia hali bila hata kuonana (ni badala ya kusema huwa una m-miss).
Akikupa namba, mpigie asubuhi kumsalimia (unaweza kuanza hata kumuuliza kama amekunywa chai, hii ya chai isiwe haraka), mchana (lunch) na usiku kulala kama mdau Faabroz alivyosema post no 22. Kila siku piga simu kusalimia muda fixed (usiharibu ratiba).
Baada ya wiki anza kutuma SMS pia za goodnight, hii ni baada ya kuwe mmeongea labda kama saa 3 usiku, saa 5 tuma SMS. Anaweza akaanza kuwa anajibu, hapa itakurahisishia.
Baada ya kama wiki mbili za kupiga simu kila siku, acha kupiga siku mbili uone je atakuulizia? Akikaa kimya halafu siku ukipiga akawa hajakuuliza kwa nini hukupiga ujue hii stratege imefeli, rudi nikupe nyingine.
Ila akikuuliza tu kwa nini hukupiga au akikupigia yeye, ujue yuko nyavuni tayari. Hapo sasa unaanza ratiba za kuonana naye lunch, pengine dinner etc, huhitaji kutongoza, from there utajua maana mtashitukia mapenzi yameanza.
Kwenye simu siku akikwambia hajisikii vizuri unajifanya kuonyesha unajali, unauliza kama ameenda hospital, kwa kufuata ratiba unauliza anaendeleaje, akisema amepona unasema nimefurahi kusikia umepona, unavaa uhusika wa kusikitika hasa (hata kama ni zuga).
NOTE: Sio lazima ziwe siku zote hizo, mwingine anaweza kuanza kutoa ushirikiano mapema tu mkaanza kuwa mnatoka weeend hata kutembea, movie, beach etc.
NB: 1. Unaweza pia kucheki profile yake ya FB itakupa mwanga ni mtu wa maisha gani, so unaweza kupata njia nyingine rahisi sana ya kumapproach.
2. Ungekuwa na gari haya yote tusingeya-discuss, gari inatongoza ndani ya siku 3 tu na usingehangaika hata na simu simu hizi. Labda kama na yeye ana gari.
Kama huwa unakutana naye na ynamsalimia ni vizuri, mwombe namba yake ya simu yeye mwenyewe, mweleze kiutani tu kwamba kuna mida unatakaga kumsalimia ila humwoni, hivyo ni vema uwe na namba unaweza kumjulia hali bila hata kuonana (ni badala ya kusema huwa una m-miss).
Akikupa namba, mpigie asubuhi kumsalimia (unaweza kuanza hata kumuuliza kama amekunywa chai, hii ya chai isiwe haraka), mchana (lunch) na usiku kulala kama mdau Faabroz alivyosema post no 22. Kila siku piga simu kusalimia muda fixed (usiharibu ratiba).
Baada ya wiki anza kutuma SMS pia za goodnight, hii ni baada ya kuwe mmeongea labda kama saa 3 usiku, saa 5 tuma SMS. Anaweza akaanza kuwa anajibu, hapa itakurahisishia.
Baada ya kama wiki mbili za kupiga simu kila siku, acha kupiga siku mbili uone je atakuulizia? Akikaa kimya halafu siku ukipiga akawa hajakuuliza kwa nini hukupiga ujue hii stratege imefeli, rudi nikupe nyingine.
Ila akikuuliza tu kwa nini hukupiga au akikupigia yeye, ujue yuko nyavuni tayari. Hapo sasa unaanza ratiba za kuonana naye lunch, pengine dinner etc, huhitaji kutongoza, from there utajua maana mtashitukia mapenzi yameanza.
Kwenye simu siku akikwambia hajisikii vizuri unajifanya kuonyesha unajali, unauliza kama ameenda hospital, kwa kufuata ratiba unauliza anaendeleaje, akisema amepona unasema nimefurahi kusikia umepona, unavaa uhusika wa kusikitika hasa (hata kama ni zuga).
NOTE: Sio lazima ziwe siku zote hizo, mwingine anaweza kuanza kutoa ushirikiano mapema tu mkaanza kuwa mnatoka weeend hata kutembea, movie, beach etc.
NB: 1. Unaweza pia kucheki profile yake ya FB itakupa mwanga ni mtu wa maisha gani, so unaweza kupata njia nyingine rahisi sana ya kumapproach.
2. Ungekuwa na gari haya yote tusingeya-discuss, gari inatongoza ndani ya siku 3 tu na usingehangaika hata na simu simu hizi. Labda kama na yeye ana gari.