Dah! Huyu mtia nia ni muongo!

Dah! Huyu mtia nia ni muongo!

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
4,289
Reaction score
2,472
Bila kuuma uma ni Lowassa, nimemsikia hapa ITV muda si mrefu akikamilisha safari ya kutafuta wadhamini ambapo kavuna malaki ya wadhamini. Kilichonigutusha ni ahadi zake. Kwanza kazungumzia viwanda vya Moro na kusema vilikuwepo viwanda ila vimekufa, akasema akiwa rais jambo la kwanza ni kushughulikia ufufuaji wa viwanda vya Moro.

Mara tena akagusia wakulima na wafugaji na kusikitishwa jinsi wanavyopigana kama kuku. Akasema akiwa rais jambo la kwanza ni kushughulikia migogoro ya wakulima na wafugaji wa Moro.

Najiuliza, kaweka ahadi ngapi huko alikopita? Hivi kweli hawa Moro wa mwisho kero zao ndio zitakuwa za kwanza? Maana haijajulikana itaanza ya viwanda au wakulima na wafugaji.

Wandugu kazi ipo, kweli naona dalili za Lowassa kuikimbia CCM kwa kutopitishwa kama ahadi tu ndio inakuwa hivi. Naona mkanganyiko kati ya sera zake na ilani yao. Mnaomsapoti Lowassa mmeliwa
 
mm mambo ya lowasa sichangii nangojea cc itakapo kaa na mengi kuhusu lowasa
 
Alisema pia JAMBO LA KWANZA itakuwa kushughulikia foleni dar "foleni dar itakuwa historia ndani ya miezi 12"
 
Kwani wewe ulikuwa hujui kuwa watia nia wa Sisiemu ni miongoni ya wasema uongo wakubwa hapa nchini kwetu?

Hebu tujikumbushe baadhi ya kauli za uongo zilizoahidiwa na watia nia hao.

Tuanze na huyo huyo Lowassa.

Alipokuwa Dar aliwaahidi wakazi wa jiji hilo kuwa 'akibahatika' kuingia Ikulu atahakikisha ndani ya miezi 6 tatizo la foleni ya magari itaisha kabisa na litageuka kuwa historia!

Tuje kwa Membe.

Alipokuwa Kigoma alisema iwapo 'ngekewa' itamdondokea na kuwa Rais, atakuwa Rais bora ambaye dunia hii haijawahi kupata!

Ailiyetia fora kwa uongo ni Profesa Muhongo.

Alipokuwa akitangaza nia kule Musoma, aliahidi kuwa iwapo 'neema' itamshukia na kutinga Ikulu, atahakikisha kila nyumba ya mwananchi wa TZ inakuwa na mabomba mawili, moja ni bomba la maji yanayotoka masaa 24 na lingine la gesi kwa ajili ya jiko la kupikia!

Baada ya kusikiliza ahadi nyingi sana za watia nia hao wanazowaahidi waTz, ambapo naamini hata nafsi zao 'zinawasuta' kwa uongo huo wa kutupa, nimeanza kuliona 'group' hilo la watia nia kutoka Sisiemu, kama kikundi fulani cha The Comedians, ambacho hakina tofauti sana na vile vikundi maarufu vya Komedi vya akina Joti na kile kingine cha kina Bambo!
 
Eh tuambie dada, ahadi za yupi unaona zinakuvutia sana ? Naona umetumwa na mtu sio bure. Ule umati unaojitokeza kumlaki na kumsapot EL kila anapokwenda unafikiri unajua zaidi kuliko ule umati. Hadi sasa amedhaminiwa na watu laki nane. Kumbuka hajatembelea kwenye wilaya ni mikoa tu. weka kata mpaka vijiji angedhaminiwa na wangapi ?
Mwambie mtia nia aliyekutuma hizo hela zake alizoiba azitumie vzr na akutafutie maneno ya kuandika siku nyengine.
 
Membe alipokuwa Mbeya alisema ikiwa yeye ataenguliwa basi atamuunga mkono Mwandosya. Membe huyo huyo alipokuwa Rukwa akasema ikiwa ataenguliwa basi atamuunga mkono Pinda. Kama si kinyonga ni nani huyo?
 
Kama mtu mwenye akili timamu na uwezo wa kuchambua mambo na unataka kumpigia kura huyu jamaa Lowassa nakuonea huruma at the same time nakudharau kwasababu inaonyesha wazi kuwa sio mzalendo na ni mmoja wa wahuni wanaosubiria kuiumiza nchi zaidi kupitia mgongo wake. CCM wameshindwa kutatua tatizo la foleni ndani ya miaka 10 huyu "Jesus wanna be" atawezaje? Kama alikuwa na solution kwanini kaikalia kimya miaka kumi anajidai tumpe nchi afanye kazi wakati anataka kurudisha hela aliyoinvest kwenye kampeni zake? Acheni kuwa kama vishuzi upepo ukipuliza mnakwenda tumieni busara zenu kuchagua kiongozi sio ushabiki wa kijinga kijinga sijui team nani mara team nyau. Tuweni wazalendo na tuanze sisi kuonyesha mfano.
 
Nani amemruhusu kufanya Kampeni? Kwanini asichukuliwe hatua? Kama akiendelea hivi bila kuchukuliwa hatua nitaamini kuwa yeye ndiye mgombea pendekezwa wa CCM.
 
Kila MTU anamtazamo wake kwa yule ampendae sasa tunguje kipenga.......…
 
Eh tuambie dada, ahadi za yupi unaona zinakuvutia sana ? Naona umetumwa na mtu sio bure. Ule umati unaojitokeza kumlaki na kumsapot EL kila anapokwenda unafikiri unajua zaidi kuliko ule umati. Hadi sasa amedhaminiwa na watu laki nane. Kumbuka hajatembelea kwenye wilaya ni mikoa tu. weka kata mpaka vijiji angedhaminiwa na wangapi ?
Mwambie mtia nia aliyekutuma hizo hela zake alizoiba azitumie vzr na akutafutie maneno ya kuandika siku nyengine.

Hata mimi nimemshangaa sana huyu mtoa mada kumuita EL muongo,sijui nani mkweli kwake ktk hao watia nia? Tena kwa usalama wa ccm ni bora wakampitisha EL,wakijichanganya tu wakamuacha ndo mwisho wa ccm na inaenda kuzikwa rasmi,asiyeamini asubiri kuamini,nani sasa wa kusimama kwa ccm? Membe? Membe ataligawa taifa vipande vipande,anataka TZ iungane na OIC ya waislamu na ndo ndoto zake kubwa,taifa lisilo na dini kuja kuingiziwa udini,itatugharimu sana.
 
Hii team naiogopa kama shetani vile. Maana yeye plus walio nyuma yake naishia kutetemeka. Maana haka ka nchi naona katakavyokuwa kanyonge zaidi ya sasa. Shida sie wa tz tuna akili za kuku.
 
Hapo hakuna tatizo mbona, au mkuu wewe umeshawahi ona mahali serikali ikashughulika na jambo moja tuuuuu hadi liishe ndio wahamie lingine? Mfano akiingia ikulu na kum-assign waziri wa ardhi ashughulikie migogoro ya ardhi na waziri wa viwanda ashughulikie viwanda moro kwa wakati mmoja kuna tatizo?????
 
Eh tuambie dada, ahadi za yupi unaona zinakuvutia sana ? Naona umetumwa na mtu sio bure. Ule umati unaojitokeza kumlaki na kumsapot EL kila anapokwenda unafikiri unajua zaidi kuliko ule umati. Hadi sasa amedhaminiwa na watu laki nane. Kumbuka hajatembelea kwenye wilaya ni mikoa tu. weka kata mpaka vijiji angedhaminiwa na wangapi ?
Mwambie mtia nia aliyekutuma hizo hela zake alizoiba azitumie vzr na akutafutie maneno ya kuandika siku nyengine.

tumekusikia dada. mpitisheni tu huko ccm maana atasambaratisha chama chenu. na akishapita akaja kwa wananchi ataongezewa tu kura laki mbili zifike milioni. hapo chama chenu kitanusurika kupasuka ila mjiandae kisaikolojia kama alivyosema jk
 
Mwaka huu wana ccm mtadanganyika tena kama miaka mengine ee
 
Back
Top Bottom