Dagaa wa Kigoma, What happened?

Nipo Kigoma mda huu,juzi nilikutana na Mkongo mmoja nilimuuliza kuhusu mazao ya ziwa victoria,kwanini huku Kigoma Dagaa ghari,akaniambia Dagaa na migebuka wengi wanaenda Burundi na Rwanda,ila ukiendwa Rukwa-Katavi dagaa na Migebuka ni Rahisi sana kuliko Kigoma,ila wakongo wanavyombo sana,upande wao dagaa na Migebuka ni wengi
 
Tena umekuta ni msimu, nakuambia dagaa wa Kigoma kuna kipindi pale Kariakoo sokoni wanashuti mpaka 27,000 kwa kilo moja,by the way maisha yamepanda galama sana kwa hiyo kuliko mtu anunue kuku kwa shilingi 15,000 halafu akamla kwa siku moja ama mbili ni bora anunua dagaa kwa 27000 halafu awatwange wiki nzima akitaka atakaanga, atarosti atapika chuku chuku lakini wanakuwa nafuu kuliko kununua kuku
 
wa Mwanza mchanga mtupu nani anataka. Halafu ukumbuke 'zamani' unayoizungumzia soko halikuwa kubwa. Sasa hivi watu wanavua na kuuza kila pembe ya nchi na hata nje ya nchi.
Kwa DRC sijui.
Halafu hao kuku wa elfu tano ni wepi kwanza?
VodaFasta Chickens!!
 


Miaka mitatu iliyopita kuna jamaa yangu alikuwa kikazi huko Kigoma ziwani kabisa. Nikamwemba aninunulie dagaa hao, lakini ikawa ngumu. Sababu aliyonipa ni kuwa wafanya biashara kutoka Kongo wamepandisha bei ya dagaa. Kwamba wakifika mwaloni huuliza bei ya sokoni wakati huo halafu wao wananunua kwa bei ya juu zaidi ili wachukue mzigo wote. Alinitajia mfanyabiashara mmoja maarufu toka Kongo aliyejulikana kama Mkasai, akifika tu hufunga soko mpaka yeye apate kwanza kiasi anachihitaji ndio hohe hahe wengine wanunue.

 
rafiki unanichokoza......
 
siku hizi dagaa wanakula wenye nazo
yaani hata kuku hawawafikii dagaa hawa wa kigoma
very strange kwa kweli
rafiki unanichekesha unavyoendelea kusisitiza bei ya dagaa wa kigoma ni kubwa kuliko ya kuku.......
kwa familia ya watu wa5 kuku anaisha kwa mlo mmoja tu, ila kilo ya dagaa mnaweza kula milo zaidi ya minne....
umelizingatia hilo rafiki?
all in all nakubaliana nawe kabisa kuwa mfumuko wa bei kwenye dagaa wa kigoma inashangaza.
huwa naagiziaga dagaa toka kigoma ziwani kabisaaaaa....(eti sitaki kununua wa kwenye magunia kule kariakoo), kwa sasa naona nafilisika tu, maana bei ya dagaa ziwani ni kubwa kuliko wa kwenye magunia ya kariakoo, inatisha sana.
 
Ushatekwa weye!!! Shurti kwa furushi la dagaa wa Kigoma na mawese... Chezeya utamu wake weye!!! 🙂🙂
hilo sikubishii kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.....
ila nainjoije sasa!!!!!!!
 
Reactions: BAK

Chanzo ni Dokta Ndodi
 
Kwa raha zako rafiki, halafu uzuri wake ni kwamba idara ya kukaangiza pia unaiweza vizuri sana, hivyo wanatoka watamu utadhani wamekaangizwa ujiji lol!!!!

hilo sikubishii kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.....
ila nainjoije sasa!!!!!!!
 
Kwa raha zako rafiki, halafu uzuri wake ni kwamba idara ya kukaangiza pia unaiweza vizuri sana, hivyo wanatoka watamu utadhani wamekaangizwa ujiji lol!!!!
ha haaa, usinijazie wageni nyumbani kwangu rafiki
 
nilishawahi fika kigoma na hasa katika bandari na kukuta shehena kubwa ya dagaa na samaki wakipakiwa kwenda kongo..kulisha watu wafanyao kazi migodini,jamaa hawachagui bei yeyote wao wananunua usijekuta ndio chanzo cha bei kuruka kiasi hicho
 

Siku hizi unaweza kupandisha bei ya kitu chochote ukiongea "in CAPITAL letters" na vyombo vya habari na "wataalamu" wa nyanja zinazoibuka kama vile tiba mbadala, etc. Fursa zinatengenezwa jamani, hazijileti.

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:

meaning.......?????
 


yaani hawa dagaa jinsi walivyo panda bei inahitajika research ya kitaalamu
otherwise five years to ten years from now dagaa watakuwa sawa na keki za birthday
 
Ziwa Tanganyika lina kina kirefu sana nadhani hilo mnalifahamu, wavuvi wetu huku kigoma wanavua kwa kutumia nyenzo duni sana ndo maana dagaa hawapatikani kwa wingi (Demand is higher than supply ) pia msimu ambapo mwezi unakuwepo usiku dagaa hua hawapatikani kabisa. nipo Kigoma hapa penyewe ikifika saa 8 ukienda kwenye mgahawa ukiulizia dagaa huwapati
 
nina sangara ,kuhe na migebuka kilo 6000-8000 atakaehitaji anjulishe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…