MCHUMIPESA
JF-Expert Member
- Mar 11, 2012
- 2,088
- 257
Kumemua na mkanganyiko na unyongwaji wa haki ya kupiga kura hasa kwa vijana wanaotimiza umri wa kupiga kura hapa tanzania,vijana walio wengi hadi sasa wanakosa haki yao ya msingi ya kupiga kura katika chaguzi kuu na hata hizi chaguzi ndogondogo(by-elections) kama katiba ya nchi na sheria mama ya uchaguzi inayonena kuwa kila mtu ana haki haki ya kuchagua(kupiga kura) au kuchaguliwa kwa mujibu wa sheria.katika hali isiyokuwa na utata ni kwamba imekuwa ni mbinu na njama chafu inayotumiwa na chama tawala katika kujipatia kura kiulaini kwa kuwatenga vijana waliofikisha huo umri wa kupiga kura na wanaotaka mabadiliko kama sasa na badala yake inaanza kuchakachua kura na kujipatia ushindi wenye utata. My take.tunaomba tume ya taifa ya uchaguzi kupitia serikali iliyoko madarakani waweke utaratibu na mchakato mahususi wa kufanya juu chini katika kurekebisha hili daftari la wapiga kura ili na hawa vijana ambao wamefikisha umri wa kupiga kura waweze kushiriki kikamilifu katika suala zima la kupiga kurahapa nchini.kwa heshima na taathima naomba kuwasilisha.