Daftari la kudumu la Wapiga Kura: Kuna sababu ya msingi ya kutoboreshwa?

Tume ya uchaguzi hufanya kazi kwa kuifurahisha CCM. CCM wanafahamu fika vijana waliotimiza miaka kumi na nane wote ni wafuasi wa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani. Hivyo hiyo ni janja ya kuibeba CCM.
 
Tume ya uchaguzi hufanya kazi kwa kuifurahisha CCM. CCM wanafahamu fika vijana waliotimiza miaka kumi na nane wote ni wafuasi wa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani. Hivyo hiyo ni janja ya kuibeba CCM.

Nadhani unaongea kwa ushabiki tu. Tume ya Uchaguzi hufanya kazi kufuatana na sheria za uchaguzi. Uboreshaji wa Daftari la wapiga Kura nalo linalindwa na sheria zake. Kwa sasa sheria inawataka kuboresha mara mbili tu kwa kipindi cha miaka mitano, yaani kutoka uchaguzi mwingine hadi unaofuata. Sheria haisemi kuboresha wakati wa uchaguzi mdogo. Sasa hilo sio kosa la Tume labda useme sheria ni mbovu tu.
 
Je ikiwa ni sheria, hamuoni kuwa wataalamu wa sheria ndani ya serikali aidha ni wajinga katika suala hili au hawana uzalendo
na haki za watanzania. Kwanini wenyewe wasiwe wa kwanza kuliona hili?
 
Nadhani unaongea kwa ushabiki tu. Tume ya Uchaguzi hufanya kazi kufuatana na sheria za uchaguzi. Uboreshaji wa Daftari la wapiga Kura nalo linalindwa na sheria zake. Kwa sasa sheria inawataka kuboresha mara mbili tu kwa kipindi cha miaka mitano, yaani kutoka uchaguzi mwingine hadi unaofuata. Sheria haisemi kuboresha wakati wa uchaguzi mdogo. Sasa hilo sio kosa la Tume labda useme sheria ni mbovu tu.

mkuu wangu lazima utambue kwamba ktk nchi hii sheria zinatengenezwa kusaidia watawala wabakie madarakani.
 
mkuu wangu lazima utambue kwamba ktk nchi hii sheria zinatengenezwa kusaidia watawala wabakie madarakani.

Nadhani ni kazi ya Jamii nzima sasa kupigia kelele sheria hii. Lakini watu tukiendelea kuisema Tume kwa jambo hili haitasaidia kitu. Tume iko kutekeleza kilichopo na endapo kitabadilishwa itakuwa ni wajibu wake kutekelezwa vile vile. Kumbuka kuwa sheria inayoibeba serikali, serikali yenyewe haiwezi kuiondoa mpaka jamii ije juu. refer mabadiliko ya Katiba, wanaharakati wamefanya kazi kubwa mpka serikali kukubali.
 
Je ikiwa ni sheria, hamuoni kuwa wataalamu wa sheria ndani ya serikali aidha ni wajinga katika suala hili au hawana uzalendo
na haki za watanzania. Kwanini wenyewe wasiwe wa kwanza kuliona hili?

Unataka wao walione wakati waliitengeneza kwa manufaa yao! Lini wajichinje? Tuache kulalamikia Tume. chukueni hatua, pigeni kelele basi.
 
Mnalalamika kama wageni wa nchi hii. Mmeshaambiwa nchi haina hela sasa gharama za kuboreshea watazikuta wapi? Waandikie pencel na majani ya migomba? Ndo maana watasigizia sheria ambayo hata wenyewe wanajua ni mbovu.
 
Naskia anataka kujitoa anaogopa kulishwa sumu
Na Rorya pia wafanye hivyo hivyo haraka iwezekanavyo kwani tumemchoka mbunge yule ambaye hata siku moja hajawahi kukohoa bungeni!
Na hizi kata tatu tunapiga kura 02/10/11
1. Nyahongo
2. Mkoma na
3. Nyamtinga.
 
Source tbccm taarifa ya habari usikuo

Mwenyekiti wa uchaguzi jaji Lubuva anadai vituo havitabadilika ila watawatoa wale wote waliojiandikisha mara mbili.

Hivi hawa tume wanataka kuwafuta kina nani?
 
Nimefuatilia kwa makini jinsi chaguzi mbali mbali zinazo endelea hapa nchini na kuona ipo haja sasa kwa tume ya uchguzi kuboresha upya daftari la wapiga kura hasa ukizingatia mambo yanayo jitokeza kuhusu idadi ya wapiga kura inapunguwa kila wakati ..wasiwasi wangu ni kuwa labda watu wamekufa wengi au wamehama kama wamasai na wasukuma na baadhi ya wakulima kwa ajili ya kutafuta malisho na sehemu nzuri za kulima ..hao ni wamashambani je hawa wa mijini nao inakuweje idadi inapunguwa ...? mfano arumeru.
 
Kama ni swala la kuboresha ili linaweza kufanyika hata bila kutuhusisha wananchi, NEC inatakiwa iondoe maghost voters wote kwenye Daftari.

Hao unaosema wachache ndio wapiga kura halisi waliojiandikisha mkuu, NEC iliongeza wapipa kura hewa ili kupenyeza mabox ya kura pale CCM inapozidiwa, udhibiti wa wizi wa kura unawaumbua sasa.
 
Mojawapo ya njia na njama chafu ya chama cha magama aka ccm wanazozitumia kuweza kujipatia kura kiulani na kusababisha wapinzani kukosa kura ni hili daftari la kudumu la wapiga kura.Nasema hivyo nikiwa na maana kuwa idadi kubwa ya vijana imeshindwa kushiriki chaguzi mbali mbali hata hizi by elections kwa sababu hawana vitambulisho vya kupigia kura wakati umri wao umeshafka kupiga kura kikatiba!!

Vijana walio wengi hapa Tanzania wanataka mabadiliko katika jamii zao na majority of them wapo mijini na hasa vijijini na wengi wao wamechoshwa na uongozi wa kitapeli na kifedhuli wa magamba wanataka mabadiliko kupitia sanduku la kura kama haki yao ya msingi!

My take:Daftari la kudumu la wapiga kura lifanyiwe marekebisho kila mwaka maana wananchi wanafikisha umri wa kupiga kura kila mwaka.Naomba kuwasilisha kwa heshima zote.
 
tunachohitaji ni NEC kuwa na wafanyakazi wake wa kudumu iliyowaajiri yenyewe ambao watafanya kazi tajwa usiku na mchana na waache kutegemea serikali za mitaa ambako mashinikizo ni kulinda uozo uliopo.......
 
Mi'sidhani kama bado hatuwez ku'computerize this system, inauma sana jins ambavyo m2 ananyimwa haki yake kwa kukusudia, mi'najua ilikua mikakati ya dhat kupunguz kas ya waleta mabadikiko, mwisho wa mwaka huu 2naingia ktk mfumo wa kidigital lkn ikiwa mifumo yetu mingi bado ipo ktk analog na manual co mbaya! lkn inamaana ulimwengu unatuburuza. Mi'nawasihi sana mnaopenda maendeleo kuiamsha jamii iliyolala. Daftar la mpiga kura halipo ktk hali nzuri lirekebishwe haraka na zaidi liwe ktk mfumo wa kikomputa kwamba kila raia awepo ndan watt na wakubwa, zpo software zinazo weza kublock under18 kupiga kura na ku unblock alietimia kupiga kura na kublock pia marehemu kutokupiga kura ya just simple kumanage system ila najua hawataki
 
Ni vyema ili kutoafura kwa watanzania wengi kupiga kura jambo ambalo litatoa ukweli na uhalisia wa matakwa ya Wananchi walio wengi.
 
Ninaunga mkono hoja. Fikiria katika uchaguzi mdogo wa Arumeru - idadi ya wapiga kura katika daftari inaonesha kuwa 120,000 lakini waliopiga kura ni 60,000 (kwa mujibu wa msimamizi wa uchaguzi). Hapa kuna matatu: 1) hiyo idadi inakuwa inflated ili walioshika mpini waweze kupenyeza wanachoweza iwapo fursa itatokea; 2) washika mpini wamenunua shahada hata za wapiga kura wao kutokana na njaa kali waliosababishia wapiga kura. Shahada zinanunuliwa ili kuzuia wahusika wasipige kura. 3) wapiga kura hawana msukumo au hamasa ya kushiriki katika zoezi la kutimiza haki yao ya kikatiba kutokana kukatishwa tamaa ya democrazy ya bongo (wizi wa kura).
 
Kumemua na mkanganyiko na unyongwaji wa haki ya kupiga kura hasa kwa vijana wanaotimiza umri wa kupiga kura hapa tanzania,vijana walio wengi hadi sasa wanakosa haki yao ya msingi ya kupiga kura katika chaguzi kuu na hata hizi chaguzi ndogondogo(by-elections) kama katiba ya nchi na sheria mama ya uchaguzi inayonena kuwa kila mtu ana haki haki ya kuchagua(kupiga kura) au kuchaguliwa kwa mujibu wa sheria.katika hali isiyokuwa na utata ni kwamba imekuwa ni mbinu na njama chafu inayotumiwa na chama tawala katika kujipatia kura kiulaini kwa kuwatenga vijana waliofikisha huo umri wa kupiga kura na wanaotaka mabadiliko kama sasa na badala yake inaanza kuchakachua kura na kujipatia ushindi wenye utata. My take.tunaomba tume ya taifa ya uchaguzi kupitia serikali iliyoko madarakani waweke utaratibu na mchakato mahususi wa kufanya juu chini katika kurekebisha hili daftari la wapiga kura ili na hawa vijana ambao wamefikisha umri wa kupiga kura waweze kushiriki kikamilifu katika suala zima la kupiga kurahapa nchini.kwa heshima na taathima naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom