Dada zangu naombeni mnishauri cha kufanya

Dada zangu naombeni mnishauri cha kufanya

mimi49 na Heaven on earth,
Kuna watu wa kupoteza muda kuwashauri ila sio huyo jamaa Nduka . . .
Ndo zake kila mara anahangaika na nyumba ndogo zake. (refer threads zake alizowahi kupost)

Lijamaa linajaza seva tu!!

aisee asante kwa taarifa Avemaria....kumbe huyu Nduka....ndo alivyo

uzuri hamna alomshauri kapata Makavu live tu toka kwa wadau

hebu nivute shuka nilale mie...ucku mwema dia
 
Last edited by a moderator:
Yani uoni hata aibu eti mapenzi yamenoga,the way nnavyoimagine wewe sio mume mwema na ndio maana umefanya yote hayo,ni mbinafsi mno na hapo hautamuumiza mkeo peke yake even your mistress hataumia pia.. Mwanaume wa kweli ni yule muaminifu katika mahusiano yake na sio kufungua zipu to everywoman anayepita katika macho yako,fanya maamuzi sahihi tell your mistress to over your illegal relationship.. #ni hayo tu..!!
 
Nilijua wajutia dhambi yako na kuacha kabisa.....lakin wewe unaogopa wanadamu watasema nini????Kazi ipo sana aiseeee
si ajabu yeye kwa mke wa marehemu kafata mali,mtu hadi anataja idadi ya magari inaonyesha interest yake ni mali.na si ajabu marehemu walifanya kumchanganyia arsenic kwenye food.
 
Mimi nimeoa, yapata mwaka sasa nimekuwa na mahusiano na mdada ambae alikuwa mke wa shemeji yangu ambae familia zetu zilikuwa karibu sana. Wote tunaishi hapa hapa dar. Kwa bahati mbaya rafiki/ndugu yangu yule alifariki. Nilihusika sana katika kumuuguza mpaka mauti ilipomkuta.

Mahusiano na familia ya marehemu yaliendelea vizuri na nilijitahidi sana kutoa msaada pale ambapo niliweza. Kibaya ni kwamba tumekuja kuwa na mahusiano na kimapenzi na huyu shemeji yangu.hakika wote tunapendana sana. Mapenzi yamenoga ambapo mpaka naona ni hatari mke wangu akija kujuwa. Naomba muelewe shemeji huyu hana matatizo kwani mume kamuachia nyumba, magari kama matano ya biashara, maduka mawili hapa mjini na yeye mwenyewe pia ni msomi ana mba.

Swali: Mimi nina wazo niongee na huyu shemeji yangu tusimamishe uhusiano wetu kabla mke wangu hajafahamu. Kuna baadhi ya marafiki zangu tayari wanafahamu. Je madada zangu mnadhani huyu mama atalichukulia vipi? Au kuna approach nyingine ninaweza kuitumia?

Naomba ushauri.

Fanya kama unamuuliza yesu halafu piga picha atakujibu nini.
 
Ushindwe kuwaza mkeo akijua atajisikiaje....how deep will you hurt her feelings...

unamuwazia huyo mwanamke....

hivi huwa mnakosa nini kwa wake zenu jamani.........
umeona eeh anamuwazia wa nje badala ya mkewe afu ndo kwanza mwaka wa kwanza kama wanaume wa saiv ndo kama wewe bora kuwa single kuliko kufa kwa stress
 
Hivi mbona JF hakuna msaada? mwenzenu nimebanwa nahitaji msaada wenu mnipe techs za kuchomoka kwa shemeji bila kuwa na mazara jamani.
 
aisee asante kwa taarifa Avemaria....kumbe huyu Nduka....ndo alivyo

uzuri hamna alomshauri kapata Makavu live tu toka kwa wadau

hebu nivute shuka nilale mie...ucku mwema dia

Lala mpendwa wangu.

Huyo Nduka michosho tu. Ningekuwa naweza ningekuwekea link ya threads zake usome . . . bahati mbaya mie si mtaalam. Labda nimuombe watu8 anigawie hayo maujuzi
 
Last edited by a moderator:
Vipi kuhusu afya zenu? Mmepata walau nafasi ya kupima?

Nikipata jibu ninaweza nikaanza kukushauri Nduka original
 
Duh!
Ukiona konnie kashangaa, ujue umej.amba haitebo.
 
Dini gani wewe? Ongeza huyo awe mke wa pili
 
Hapa hata sina ushauri wowote bora ungewaomba wanaume wenzio sisi wadada tunaumia kwa unachomfanyia mwenzetu afu unatuomba ushauri atiii. uwiiiiiiiii uwiiiiiiiii.
 
endelea kumgegeda tuu...ndio raha ya dunia. wee ata mke akijua ishakula kwake...atalia ila atabaki.
 
kiongozi sema unamendea pesa za huyo mama!!!acha umario tafuta zako ili uleee familia yako vizuri,,sio ulee familia yako kwa jasho la mwanaume mwenzio
 
Back
Top Bottom