Mimi nimeoa, yapata mwaka sasa nimekuwa na mahusiano na mdada ambae alikuwa mke wa shemeji yangu ambae familia zetu zilikuwa karibu sana. Wote tunaishi hapa hapa dar. Kwa bahati mbaya rafiki/ndugu yangu yule alifariki. Nilihusika sana katika kumuuguza mpaka mauti ilipomkuta.
Mahusiano na familia ya marehemu yaliendelea vizuri na nilijitahidi sana kutoa msaada pale ambapo niliweza. Kibaya ni kwamba tumekuja kuwa na mahusiano na kimapenzi na huyu shemeji yangu.hakika wote tunapendana sana. Mapenzi yamenoga ambapo mpaka naona ni hatari mke wangu akija kujuwa. Naomba muelewe shemeji huyu hana matatizo kwani mume kamuachia nyumba, magari kama matano ya biashara, maduka mawili hapa mjini na yeye mwenyewe pia ni msomi ana mba.
Swali: Mimi nina wazo niongee na huyu shemeji yangu tusimamishe uhusiano wetu kabla mke wangu hajafahamu. Kuna baadhi ya marafiki zangu tayari wanafahamu. Je madada zangu mnadhani huyu mama atalichukulia vipi? Au kuna approach nyingine ninaweza kuitumia?
Naomba ushauri.