Dada yangu Sophia Simba, chagua moja. Nchimbi atasema punde!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Dada yangu na kada mwenzangu mwandamizi wa zamani wa CCM, Sophia Simba unapaswa kufanya uamuzi. Uamuzi wa kuchagua moja: kuomba msamaha na kurejea CCM au kuhamia chama kingine au kubaki kimya bila chama.

Nimesikia na kusoma mahali kuwa umesema utakuwa mkereketwa mwaminifu wa CCM. Ukereketwa ni nini? Unabakije kuwa mkereketwa wa chama kilichokufukuza uanachama kwa kukisaliti (kuonesha kukosoa maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu)? Msaliti anabaki vipi?

Dada Sophia Simba, nakujua na naijua historia yako ya kichama. Nakujua tangu enzi zile ulipokuwa Katibu Muktasi (Secretary) huko Dar es Salaam. Najua jinsi ulivyojijenga taratibu hadi kufika ulipofukuziwa. Najua kuwa UWT umeitangaza na kuiimarisha. Hupaswi kubaki bila kuamua.

Ninazo taarifa kuwa Balozi Emmanuel Nchimbi atasema neno hivi karibuni. Kwa misimamo yake, hulka yake na 'ungoni' wake, Nchimbi ataweka wazi msimamo wake juu ya kubaki au kutoka CCM. Hawezi kubaki vuguvugu kama wewe. Najua umeumia kuona unafukuzwa na kiongozi wako Nchimbi akipewa onyo kali.

Dada Sophia Simba, ni ima uombe msamaha na usubiri miaka miwili kurejeshwa chamani-CCM au uamue kujiunga na wengine au ukae kimya bila 'ukereketwa' wowote. Kwa level uliyofikia ndani ya CCM (kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu), hupaswi kubaki huelewekieleweki.

Mwafaaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha kumchagua Lissu kuwa Rais wa TLS)
 
Kwani lazima awe ccm?ahame,maisha sio ccm tu,chama chenyew kipo ukingoni,kimefika mwisho hicho
 
Huyu mama yupo pamoja na great thinkers na majabali ya siasa hapa Tz. Sina shaka na uamuzi wake. Naamini hakuna jipya litakalofanywa na CCM bila team mamvi kupata updates. The only solution I suggest, CCM waache kutumia majengo yote ambayo Lowasa alikuwa akitumia hapo awali maana hata kuta bado zinampenda. Pili, wote waliojifanya wana imani na mtu yule wapukutishwe bila kujali nafasi walizonazo.

Chama kipo katika wakati mgumu wa kushindwa kutunza siri na mipango. Adui yupo kila kona yapasa kuondoa kila aina ya hofu.
 
Nchimbi kasha kula shavu, sidhani kama ataongea tofauti na kile alichotwambia Pole pole akifanye; nina hakika ataomba msamaha tu. Kwani si kuna mtandao mmoja umemripoti kwamba nae anafanyaga biashara ya sembe? Sasa ajifanye jeuri ili anyang'anywe ubalozi halafu arudishwe bongo and then aunganishwe na kundi la kina Wema? Sidhani kaka Tupatupa, huyo ataomba msamaha tu.
Nakuunga mkono hapo kwa dada Sophia
 
Dada yangu na kada mwenzangu mwandamizi wa zamani wa CCM, Sophia Simba unapaswa kufanya uamuzi. Uamuzi wa kuchagua moja: kuomba msamaha na kurejea CCM au kuhamia chama kingine au kubaki kimya bila chama.

Nimesikia na kusoma mahali kuwa umesema utakuwa mkereketwa mwaminifu wa CCM. Ukereketwa ni nini? Unabakije kuwa mkereketwa wa chama kilichokufukuza uanachama kwa kukisaliti (kuonesha kukosoa maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu)? Msaliti anabaki vipi?

Dada Sophia Simba, nakujua na naijua historia yako ya kichama. Nakujua tangu enzi zile ulipokuwa Katibu Muktasi (Secretary) huko Dar es Salaam. Najua jinsi ulivyojijenga taratibu hadi kufika ulipofukuziwa. Najua kuwa UWT umeitangaza na kuiimarisha. Hupaswi kubaki bila kuamua.

Ninazo taarifa kuwa Balozi Emmanuel Nchimbi atasema neno hivi karibuni. Kwa misimamo yake, hulka yake na 'ungoni' wake, Nchimbi ataweka wazi msimamo wake juu ya kubaki au kutoka CCM. Hawezi kubaki vuguvugu kama wewe. Najua umeumia kuona unafukuzwa na kiongozi wako Nchimbi akipewa onyo kali.

Dada Sophia Simba, ni ima uombe msamaha na usubiri miaka miwili kurejeshwa chamani-CCM au uamue kujiunga na wengine au ukae kimya bila 'ukereketwa' wowote. Kwa level uliyofikia ndani ya CCM (kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu), hupaswi kubaki huelewekieleweki.

Mwafaaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha kumchagua Lissu kuwa Rais wa TLS)
Wewe kwani ni wakili?
 
Namsubiri Nchimbi tu, maana ndio aliyeongea hawali. Huyo mama alibaki kupigwa picha tu.
 
Nchimbi alishatepeta. Huyu aliwah mapema kwenda kujikabidhi kwa mh na kumlamba miguu
 
Nchimbi alishatepeta. Huyu aliwah mapema kwenda kujikabidhi kwa mh na kumlamba miguu
 
Kwa umri wake apumzike tu siasa lasivyo ngonjera na vijembe vitakuwa fadhila yake.
 
Sofia Simba mfia ccm aliyetoswa akizinduka atabadili kauli.
Tupa Tupa tukutane Arusha kumchagua TL kwa ajili ya Tanganyika tuipendayo; Fair, Just and Progressive. Mungu ibariki Tanzania
 
c681a940d750ece744b4df33806fe83e.jpg
 
Back
Top Bottom