Dada wa kazi anapaswa kulipwa mshahara kiasi gani kwa mwezi?

Melki Wamatukio

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,839
10,070
Nafahamu fika naingilia makubariano ya watu, ila kwa jambo kama hili si sawa!

Anapika chakula, anafua nguo za watoto, baba na mama mwenye nyumba, kila siku kibarazani kunyoosha hizo nguo, usafi kuzunguka nyumba, kuteka maji maili mia zaidi ya ndoo kumi na tano kwa siku (na huo mpando), kuwapeleka na kuwafuata watoto shuleni, bado kuhudumia mkuyenge wa mdogo wake mama mwenye nyumba! Na mikazi mingine kibao!

Alfajiri ninapoamka asubuhi na mapema namkuta nje, usiku kwenye saa sita ndo muda wake wa kulala (alivyonieleza)

Bado mke wa boss amsurubishe kwa mabao, mangumi na mateke pindi atokapo kazini na hasira zake especially akute wanae hawajaoga! Au kitoto kimchongee mdomo kwa mama yake! Mchana kutwa, jua kali anaelekea sokoni kuemea!


Alivyonisimulia haya yote nimejikuta namwaga chozi!

Yote tisa:
Mshahara 30,000 kwa mwezi! Halafu 10,000 ni makato kwenda kwa dada yake aliyemtafutia kazi! Halafu ni ndugu wa damu eti!

Mtakufa kifo kibaya ninyi wahusika!

Nashindwa niwachukulie hatua gani!
Na ngoja nipate mahali sahihi pa kumpeleka akapata kazi ya maana, Nitamtorosha!
 
Nimemrudisha kwao bhana aache ujinga ,,,mtoto kiburi,jeuri,haambiliki,,kupika anapika wife,nguo zangu anafua wife ,,kufungua nguo za mtoto anasaidiwa,,narudi job mtoto hajambadilisha nguo yaan toka asubuhi yupo vilevile ,,ukimuuliza anajibu kiufupi ,,sijui,,,,watoto wote ndani ya nyumba wanahaki sawa kuanzia yaya mpk wanangu lkn huyu hapana,,wacha aende kwao..40k nyingi sana
 
Aise huyo mdada kampata ,Kuna ndugu yangu Ana mdada hawezi kuwahi kuamka kufanya maandalizi ya watoto shule,watoto wanaandaliwa na boss ikiwa Ni pamoja na kusimamiwa kula kabla hawajaenda shule,chakula Cha family kinapikwa na mama mwenye nyumba japo naye Ni mtu na mishe zake Ila akirudi lazima apike chukula Cha usk,nguo za baba na mama zinafuliwa na mama mwenye nyumba muda mwingine mpaka za watoto zinafuliwa na mama,malipo ya huyo mfanyakazi Ni 50000 hiyo 30000 kwa majukumu yote hayo Ni ndogo sn
 
Nafahamu fika naingilia makubariano ya watu, ila kwa jambo kama hili si sawa!

Anapika chakula, anafua nguo za watoto, baba na mama mwenye nyumba, kila siku kibarazani kunyoosha hizo nguo, usafi kuzunguka nyumba, kuteka maji maili mia zaidi ya ndoo kumi na tano kwa siku (na huo mpando), kuwapeleka na kuwafuata watoto shuleni, bado kuhudumia mkuyenge wa mdogo wake mama mwenye nyumba! Na mikazi mingine kibao!

Alfajiri ninapoamka asubuhi na mapema namkuta nje, usiku kwenye saa sita ndo muda wake wa kulala (alivyonieleza)

Bado mke wa boss amsurubishe kwa mabao, mangumi na mateke pindi atokapo kazini na hasira zake especially akute wanae hawajaoga! Au kitoto kimchongee mdomo kwa mama yake! Mchana kutwa, jua kali anaelekea sokoni kuemea!


Alivyonisimulia haya yote nimejikuta namwaga chozi!

Yote tisa:
Mshahara 30,000 kwa mwezi! Halafu 10,000 ni makato kwenda kwa dada yake aliyemtafutia kazi! Halafu ni ndugu wa damu eti!

Mtakufa kifo kibaya ninyi wahusika!

Nashindwa niwachukulie hatua gani!
Na ngoja nipate mahali sahihi pa kumpeleka akapata kazi ya maana, Nitamtorosha!
TZS 300,000 kabla ya ongezeko la 23.3%
 
Nao wanafanya kazi
Sawa lkn kupika hawez kupika yaya
Wala nguo zangu hawez kupas yaya na kutua pia hawez kufua yaya...tuwe serious baba mwenye nyumba kuruhusu chakula Cha familia kipikwe na yaya Ni uzembe..labda km hakuna option nyingne
 
Nimemrudisha kwao bhana aache ujinga ,,,mtoto kiburi,jeuri,haambiliki,,kupika anapika wife,nguo zangu anafua wife ,,kufungua nguo za mtoto anasaidiwa,,narudi job mtoto hajambadilisha nguo yaan toka asubuhi yupo vilevile ,,ukimuuliza anajibu kiufupi ,,sijui,,,,watoto wote ndani ya nyumba wanahaki sawa kuanzia yaya mpk wanangu lkn huyu hapana,,wacha aende kwao..40k nyingi sana
Pole ndugu naona umekereka mpaka basi
 
Back
Top Bottom