comte
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 8,222
- 5,946
Rosemary Kweka
1tSpons5faohrendfg ·Nikiwa kama Mgeni rasmi wa Mahafali ya 10 Shule ya Sekondari Kiloleli October 31/2020. Ni heshima ambayo inakuja na majukumu.
💁Unaambiwa mafanikio na changamoto za shule. Na hutoi tu ahadi kama wanasiasa, unatakiwa kuzitatua hizo changamoto.
💁Nashukuruni kwa heshima na nilifanya wajibu wangu. Nilichangia Meza ya Ofisi na Kabati la vitabu kwaajili ya mkuu wa shule vyenye thamani ya 1.2mil kama Mkurugenzi Mtendaji wa Furniture Designer
💁Marafiki wa faida walionisindikiza ikiwemo Maheshi Dhondri- Rais wa Lions Club International- Mwanza (kushoto kwangu), Mrs. Chegeni- Mkurugenzi Mtendaji wa Isamilo Lodge- Mwanza, Mrs. Zongii -Mkurugenzi Mtendaji wa Zongii Molders na dada yangu kipenzi Beatrice Samson Ngwalida walinisaidia kusapoti meza 5 za walimu na kuendelea kuichangia shule ktt changamoto mbalimbali zinazoikabili.
💁Asanteni sana Desk and Chair Foundation kwa kusapoti ujenzi wa vyoo vya walimu na wanafunzi. Vyoo 10 vya kike, 10 vya kiume na 5 vya walimu.
💁Unapokuwa na mapenzi ya dhati na nchi yako na unajua unao wajibu kama mwananchi (si lazima uwe mwanasiasa). Unajitoa kwa hali na mali kuisapoti jamii yako.
💁Mafanikio ya watoto wote ni faida kwa jamii nzima. Wakiwa wazuri tutanufaika wote, tukiwaacha waangamie au wakose elimu bora tutakuja kuumia wote. Tutekeleze wajibu wetu kwa pamoja.
🙋🙋🙋🙋TUSHIRIKIANE KUIJENGA NCHI YETU NA JAMII YETU KWA HALI NA MALI. TUWEKE KIPAUMBELE CHA KUWAINUA WATOTO WOTE.
💁MIMI NI SHUHUDA, WALIONIPA MSAADA WA KUSOMA SIO NDUGU ZANGU WALA SINA UKOO NAO. ILA WALIJUA MANUFAA YAKE NI KWANGU, NDUGU, JAMAA NA TAIFA LANGU KWA UJUMLA.
4040
11 C