george aloyce
JF-Expert Member
- Aug 22, 2017
- 1,177
- 1,827
Naomba nisaidie, sijui nafanya nini Kaka, mtoto wangu ni mbaya, ana miaka miwili halafu ni wa kike, yaani kafanana na baba yake kila kitu, mpaka naona aibu hata marafiki zangu kuja kunisalimia, mbali na kumpost.
Natamani hata nimwachie bibi yake, nikazae mwingine na mwanaume mwingine huko, ila si mume wangu. Ninapiga sindano za uzazi wa mpango, wakati nikihangaika kutafuta mwanaume mwingine wa kuzaa naye, siwezi kuzaa tena na huyu mume wangu.
Shida ni kwamba baba yake anampenda mtoto wake hivyo hivyo, nikimuambia ishu ya kumpeleka kwa bibi yake, mpaka tunagombana, kwani hakuna sababu yoyote ile, nisiaidie nimuambieje ili akubali nimuondoe huyu mtoto hapa.
Nikiona marafiki zangu wakipost watoto wao mitandaoni, najikuta nakuwa na hasira, namfokea mwanangu, sijawahi kumpiga, ila najisikia vibaya ninavyomkasirikia. Mtoto hataki hata kunisogelea, nakuwa mkali, kana kwamba ananiogopa, anakua na amani baba yake tu akiwa nyumbani.
NB: Nachukia kuandika hizi stori, lakini zimekuwa nyingi, kama uko kama huyu Mama, tafuta msaada, haiuko sawa kabisa!
Natamani hata nimwachie bibi yake, nikazae mwingine na mwanaume mwingine huko, ila si mume wangu. Ninapiga sindano za uzazi wa mpango, wakati nikihangaika kutafuta mwanaume mwingine wa kuzaa naye, siwezi kuzaa tena na huyu mume wangu.
Shida ni kwamba baba yake anampenda mtoto wake hivyo hivyo, nikimuambia ishu ya kumpeleka kwa bibi yake, mpaka tunagombana, kwani hakuna sababu yoyote ile, nisiaidie nimuambieje ili akubali nimuondoe huyu mtoto hapa.
Nikiona marafiki zangu wakipost watoto wao mitandaoni, najikuta nakuwa na hasira, namfokea mwanangu, sijawahi kumpiga, ila najisikia vibaya ninavyomkasirikia. Mtoto hataki hata kunisogelea, nakuwa mkali, kana kwamba ananiogopa, anakua na amani baba yake tu akiwa nyumbani.
NB: Nachukia kuandika hizi stori, lakini zimekuwa nyingi, kama uko kama huyu Mama, tafuta msaada, haiuko sawa kabisa!