Dada amwaga matusi hadharani

Dada amwaga matusi hadharani

Idhae

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2014
Posts
609
Reaction score
277
Nilikuwa baa moja hivi napata kinywaji baridi, jirani nami alikuwepo jamaa mmoja na binti mrembo.

Mara wakaingia jamaa wawili wakaelekea kwenye ile meza ya yule bwana na yule binti, kisha jamaa akafanya utambulisho...huyu ndiyo DEMU wangu.

Binti alimwaga mitusi hadi aibu kisa? Hataki kuitwa demu.

Nawashauri wale wenye tabia ya kuwaita wachumba zao MADEMU waache mara moja wasije yakawakuta kama huyo bwana...kwani nimegundua baadhi ya mabinti hawapendi itwa mademu
 
demu inatokana na neno dame ambalo ni neno la heshima in english
 
Nilikuwa baa moja hivi napata kinywaji baridi, jirani nami alikuwepo jamaa mmoja na binti mrembo.
Mara wakaingia jamaa wawili wakaelekea kwenye ile meza ya yule bwana na yule binti, kisha jamaa akafanya utambulisho...huyu ndiyo DEMU wangu. Binti alimwaga mitusi hadi aibu...kisa? Hataki kuitwa demu.
Nawashauri wale wenye tabia ya kuwaita wachumba zao MADEMU waache mara moja wasije yakawakuta kama huyo bwana...kwani nimegundua baadhi ya mabinti hawapendi itwa mademu

wewe demu?
 
ni kweli kabisa hawapendi maana nilimtania wife tukiwa chumban akamaindi sana hata....... haikutekelezwa hahahahaaaaaa
 
Huyo demu hajielewi? bangi na viroba zimemuchanganya demu wa watu.
 
Aiseee, mi hata classmate wangu tulikua tunafight kuniita au kuita mdichana yeyote. Nkisikia tuu, moto wake ni sheeedrah, ni zuri japo tumezoea vibaya kwamba anaeitwa ivo huwa ni part time, (get n use) hadi saizi silitaki na silipendi
 
Dem ni kibint cha o level kuanzia form 2 hadi 4
 
Back
Top Bottom