Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,786
- 1,710
Tumesikia kauli ya mufti nanukuu, (maneno yote hapa ni ya Mufti si yangu):
"Nawatahadharisha Waislamu wote nchini kwamba Ponda Issa Ponda si mwanazuoni, si Sheikh, hakusoma elimu ya msingi ya kidunia wala ya kidini, hata Qur'an hajui kusoma. Anajaribu kuwatumia Waislamu kwa manufaa yake binafsi. Hatujawahi kushuhudia kutoka Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania jambo lolote la maendeleo zaidi ya ghasia za maandamano, kupora misikiti na kudandia matukio na kuwachangisha Waislamu fedha, mwishoni mwa maandamano hayo huishia kuwatapeli waumini fedha zao ambazo huishia mifukoni mwa Ponda na wenzake."
"Ni kigenge cha watu wachache wenye kufuata madhehebu ya Mawahabi ambao kwa mujibu wa itikadi yao wanaamini kwamba Muislamu yeyote asiyefuata itikadi yao basi huyo siyo Muislamu na hafai kuwa kiongozi kwa ngazi yoyote ile"
"Vurugu, chokochoko na ghasia za uvamizi hazikuanzia Bakwata, wamekuwa wakifanya hivyo sehemu mbalimbali mikoani kwa kuvamia na kuteka misikiti na kuwaondoa viongozi waliochaguliwa kihalali kwa nguvu na udhalilishaji mkubwa na hatimaye kupora na kuhodhi rasilimali za misikiti hiyo."
"Wamekuwa wakiendesha mafunzo ya karate kwenye misikiti hiyo waliyoiteka na kuikalia kimabavu ili waweze kuendeleza dhuluma yao ya uporaji wa Misikiti na vituo vingine vya Kiislamu."
"Ni vitendo vinavyokiuka maadili ya Uislamu. Kwa sababu hiyo nawaonya na kuwatahadharisha Waislamu wa madhehebu yote kuepuka vitendo vya uvunjaji wa sheria unaofanywa na kikundi hiki cha watu wachache."
Source: Mwananchi 21.09.2012
Mimi najaribu kutafuta ukweli katika haya anayosema mufti. Naombeni wanaofahamu vizuri CV ya Ponda watuwekee hapa.
"Nawatahadharisha Waislamu wote nchini kwamba Ponda Issa Ponda si mwanazuoni, si Sheikh, hakusoma elimu ya msingi ya kidunia wala ya kidini, hata Qur'an hajui kusoma. Anajaribu kuwatumia Waislamu kwa manufaa yake binafsi. Hatujawahi kushuhudia kutoka Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania jambo lolote la maendeleo zaidi ya ghasia za maandamano, kupora misikiti na kudandia matukio na kuwachangisha Waislamu fedha, mwishoni mwa maandamano hayo huishia kuwatapeli waumini fedha zao ambazo huishia mifukoni mwa Ponda na wenzake."
"Ni kigenge cha watu wachache wenye kufuata madhehebu ya Mawahabi ambao kwa mujibu wa itikadi yao wanaamini kwamba Muislamu yeyote asiyefuata itikadi yao basi huyo siyo Muislamu na hafai kuwa kiongozi kwa ngazi yoyote ile"
"Vurugu, chokochoko na ghasia za uvamizi hazikuanzia Bakwata, wamekuwa wakifanya hivyo sehemu mbalimbali mikoani kwa kuvamia na kuteka misikiti na kuwaondoa viongozi waliochaguliwa kihalali kwa nguvu na udhalilishaji mkubwa na hatimaye kupora na kuhodhi rasilimali za misikiti hiyo."
"Wamekuwa wakiendesha mafunzo ya karate kwenye misikiti hiyo waliyoiteka na kuikalia kimabavu ili waweze kuendeleza dhuluma yao ya uporaji wa Misikiti na vituo vingine vya Kiislamu."
"Ni vitendo vinavyokiuka maadili ya Uislamu. Kwa sababu hiyo nawaonya na kuwatahadharisha Waislamu wa madhehebu yote kuepuka vitendo vya uvunjaji wa sheria unaofanywa na kikundi hiki cha watu wachache."
Source: Mwananchi 21.09.2012
Mimi najaribu kutafuta ukweli katika haya anayosema mufti. Naombeni wanaofahamu vizuri CV ya Ponda watuwekee hapa.