Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,027
- 20,411
CUTHBERT SWAI NDANI YA MTEGO WA LEMA NA MBOWE
Nitangulize kusema kuwa Mimi nimekuwa ndani ya Chadema kwa Miaka Mingi sana, Nimeshiriki katika Ujenzi wa Chama na kusimamia operesheni kadhaa za Chama ikiwemo Mipango Ovu ya Chama huku ikiratibiwa na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.
Mbowe ni Kiongozi mwenye kisasi na akidhamiria jambo lake lazima alitimize kwa njia yeyote ile. Wakati Sabaya anateuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya pale Hai nilijisemea peke yangu Sabaya anaenda katika vita vya Maisha Yake. Ashinde Aheshimike au Ashindwe na ndoto zake katika Uongozi ziishe. Ila toka Ameteuliwa Mpaka sasa Sabaya ndiye Mshindi anaongoza dhidi ya Mbowe na Sasa Mbowe anataka kulipa Kisasi.
Sasa kisasi kinalipwa kupitia Mfanyabiashara Cuthbert Swai, Huyu Swai namfahamu Miaka Mingi ni Mfanyabiashara ambaye amekisaidia chama cha Chadema sana, Operesheni nyingi za Vijana za kujenga chama zilifadhiliwa na huyu bwana naweza sema ni mmoja wa vijana wenye roho ngumu sana wapo Tayari kumaliza mtu yeyote ili kulinda Maslahi yao. Mbowe, Cuthbert na Lema hawa wote ni Wachaga wa Machame wameungana kupambana na kijana wa Kimasai Lengai Ole Sabaya.
Sasa hivi Sabaya amekua Ajenda ya Chama, Chama sasa kinatumia Akaunti zao za Twiter, Facebook na Istagram huku baadhi ya viongozi waandamizi wafuasi wa Mbowe na Lema kama Twaha Mwaipaja na Kumbusho Dawson wakipokea fungu kutoka kwa Cuthbert ili kuchafua Image ya Sabaya.
Sabaya kuwa Serikalini ni Tatizo kubwa kwa Upinzani wa nchi hii, Kumbuka huyu ndiye amemuangusha Mbowe, Huyu ndiye kafanya Hai imetulia na sio uchochoro wa uhalifu tena, Dawa za kulevya, Noti feki, Uhalifu, Dhuluma sasa haviwezi fanyika tena Hai. Mbowe sasa anataka kulinda Genge lake la wafanyabiashara ambao si rafiki kwa Serikali yetu.
Sasa Cuthbert amesahau Uhuni wake katika Biashara, Dhuluma zake kwa Wapagazi katika Kampuni yake, Dhuluma zake za Ardhi kwa wananchi na Amesahau kuwa hata hapo Jipe anapoishi sasa Ardhi anayokaa inasomeka amepewa na wanakijiji bila kujua Mchezo mchafu anaochezaga wa kujimilikisha Ardhi kwa Kisingizio cha kupewa na wanakijijiji vinajulikana. Aasa kaingizwa kwenye Ngoma ya Mbowe na Lema na yeye anacheza huku akiambiwa ndivyo atasaidika. Nachomwambia Swai yeye anajiitaga Muhuni ila Lema na Mbowe ni Wahuni zaidi yake.
Wacha niwakumbushe jambo, Sabaya Aliteuliwa akitokea Arusha, Na aliteuliwa wakati wa Misukosuko, Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Waandamizi wakimpinga na kumshawishi Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa kuwa Sabaya Hafai, Ni baada ya kuamua kusimama kwa wanyonge na kutetea Maslahi yao ambayo Matajiri walikua wakiwanyonya bila huruma. Sabaya alibaki Peke yake, Bila Chama, Bila wafanyabiashara akabaki na Wananchi wanyonge. Pamoja na kumbambikia Kesi Mwishowe Rais Akamteua Nafasi aliye nayo sass hivi.
Mungu Humuinua katika Nyakati zenye kelele kama hizi, Hii ni ishara tosha kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kutazama file la Sabaya na kutambua Tunu kubwa aliyopata huyu kijana katika kusimamia misingi ya utawala bora na uongozi.
Kijana Mwenzangu Sabaya Huu ni wakati wako, Piga kazi, Usiwajibu wacha sisi tuwajibu hatukubali Wahuni watupangie nani wa kutuongoza.
Pia nishauri Diwani wa Arusha unayelalamika kupigwa na Sabaya mpango wenu unafahamika wewe na hao wafanyabiashara pamoja na kiongozi mmoja wa wilaya moja iliyo ndani ha Mkoa wa Kilimanjaro, Kiongozi huyo anafahamu uwepo wa Sabaya Hai utasababisha Hai iendelee kuongoza katika Ukusanyaji wa Mapato huku yeye akitaka ndiye aongoze kupitia wilaya anayofanya kazi. (Huyo kiongozi namuweka Kiporo)
Mimi kada Mtiifu wa Chama cha Mapinduzi, na Nitasimama katika Misingi ya Chama changu, Nitalinda kiapo changu ndani ya Chama, Nitasema Kweli Daima na Uongo kwangu ni Mwiko.
Nitangulize kusema kuwa Mimi nimekuwa ndani ya Chadema kwa Miaka Mingi sana, Nimeshiriki katika Ujenzi wa Chama na kusimamia operesheni kadhaa za Chama ikiwemo Mipango Ovu ya Chama huku ikiratibiwa na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.
Mbowe ni Kiongozi mwenye kisasi na akidhamiria jambo lake lazima alitimize kwa njia yeyote ile. Wakati Sabaya anateuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya pale Hai nilijisemea peke yangu Sabaya anaenda katika vita vya Maisha Yake. Ashinde Aheshimike au Ashindwe na ndoto zake katika Uongozi ziishe. Ila toka Ameteuliwa Mpaka sasa Sabaya ndiye Mshindi anaongoza dhidi ya Mbowe na Sasa Mbowe anataka kulipa Kisasi.
Sasa kisasi kinalipwa kupitia Mfanyabiashara Cuthbert Swai, Huyu Swai namfahamu Miaka Mingi ni Mfanyabiashara ambaye amekisaidia chama cha Chadema sana, Operesheni nyingi za Vijana za kujenga chama zilifadhiliwa na huyu bwana naweza sema ni mmoja wa vijana wenye roho ngumu sana wapo Tayari kumaliza mtu yeyote ili kulinda Maslahi yao. Mbowe, Cuthbert na Lema hawa wote ni Wachaga wa Machame wameungana kupambana na kijana wa Kimasai Lengai Ole Sabaya.
Sasa hivi Sabaya amekua Ajenda ya Chama, Chama sasa kinatumia Akaunti zao za Twiter, Facebook na Istagram huku baadhi ya viongozi waandamizi wafuasi wa Mbowe na Lema kama Twaha Mwaipaja na Kumbusho Dawson wakipokea fungu kutoka kwa Cuthbert ili kuchafua Image ya Sabaya.
Sabaya kuwa Serikalini ni Tatizo kubwa kwa Upinzani wa nchi hii, Kumbuka huyu ndiye amemuangusha Mbowe, Huyu ndiye kafanya Hai imetulia na sio uchochoro wa uhalifu tena, Dawa za kulevya, Noti feki, Uhalifu, Dhuluma sasa haviwezi fanyika tena Hai. Mbowe sasa anataka kulinda Genge lake la wafanyabiashara ambao si rafiki kwa Serikali yetu.
Sasa Cuthbert amesahau Uhuni wake katika Biashara, Dhuluma zake kwa Wapagazi katika Kampuni yake, Dhuluma zake za Ardhi kwa wananchi na Amesahau kuwa hata hapo Jipe anapoishi sasa Ardhi anayokaa inasomeka amepewa na wanakijiji bila kujua Mchezo mchafu anaochezaga wa kujimilikisha Ardhi kwa Kisingizio cha kupewa na wanakijijiji vinajulikana. Aasa kaingizwa kwenye Ngoma ya Mbowe na Lema na yeye anacheza huku akiambiwa ndivyo atasaidika. Nachomwambia Swai yeye anajiitaga Muhuni ila Lema na Mbowe ni Wahuni zaidi yake.
Wacha niwakumbushe jambo, Sabaya Aliteuliwa akitokea Arusha, Na aliteuliwa wakati wa Misukosuko, Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Waandamizi wakimpinga na kumshawishi Rais ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa kuwa Sabaya Hafai, Ni baada ya kuamua kusimama kwa wanyonge na kutetea Maslahi yao ambayo Matajiri walikua wakiwanyonya bila huruma. Sabaya alibaki Peke yake, Bila Chama, Bila wafanyabiashara akabaki na Wananchi wanyonge. Pamoja na kumbambikia Kesi Mwishowe Rais Akamteua Nafasi aliye nayo sass hivi.
Mungu Humuinua katika Nyakati zenye kelele kama hizi, Hii ni ishara tosha kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kutazama file la Sabaya na kutambua Tunu kubwa aliyopata huyu kijana katika kusimamia misingi ya utawala bora na uongozi.
Kijana Mwenzangu Sabaya Huu ni wakati wako, Piga kazi, Usiwajibu wacha sisi tuwajibu hatukubali Wahuni watupangie nani wa kutuongoza.
Pia nishauri Diwani wa Arusha unayelalamika kupigwa na Sabaya mpango wenu unafahamika wewe na hao wafanyabiashara pamoja na kiongozi mmoja wa wilaya moja iliyo ndani ha Mkoa wa Kilimanjaro, Kiongozi huyo anafahamu uwepo wa Sabaya Hai utasababisha Hai iendelee kuongoza katika Ukusanyaji wa Mapato huku yeye akitaka ndiye aongoze kupitia wilaya anayofanya kazi. (Huyo kiongozi namuweka Kiporo)
Mimi kada Mtiifu wa Chama cha Mapinduzi, na Nitasimama katika Misingi ya Chama changu, Nitalinda kiapo changu ndani ya Chama, Nitasema Kweli Daima na Uongo kwangu ni Mwiko.

