Shule ni kitu muhimu, waliogopa umande ndio walikosa elimu wakasingizia ukoloni. Wameishiwa hata kupatariziki ya kutia tonge kinywani basi inatokana na fitina. Bila fitina hawali.
Choyo na kijicho ndio sera zao na kushinda kutwa kwenye maskani. Upuuzi wa mtoa mada hapo juu unatokana na wale watu waliokimbia umande na kutoroka shule. Halaiki na chipukizi ndivyo alivyotumia ujana wake na ndio shule yake.
Ni wazi CUF haiwezi kupambana na dola lisioheshimu utu na haki. Lakini ni ujinga usiopingika kuwa huwezi kumkuta CCM Mzanzibari mshirazi ambae hakuchanganya damu na mfuasi wa CUF. Kwa hiyo hakuna mtu atakaeisoma namba zaidi ya CCM WAKATA MAJI.
Wakati wa kukipachika chama cha CUF kuwa ni chama cha kigaidi zimepitwa na wakati. Ulimwengu umeshaelewa nani gaidi Zanzibar, Janjaweed, Mazombie au Mabarkowa!
Uchaguzi wa Oktoba 2015 umepeleka ujumbe mzito kwa nchi za nje hali halisi ya siasa za Zanzibar na hawawababahwi tena. Hakuna mtu mwenye uthubutu wa kukifuta chama cha CUF , na kwa kosa gani? la kuismbaratisha CCM Zanzibar kwenye uchaguzi? huo ndio ugaidi kwenye kamusi ya CCM?