Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Kama hii habari ni kweli basi tukae mkao wa kula kwa CUF kuingia madarakani 2010.
Ni matumaini ya kila Mtanzania kuwa endapo vigogo hao ambao wameonekana kuwa mstari wa mbele katika kukinzana na wenzao na pia kuonekana kujitenga kwa kukemea mambo ambayo hayaendani na taratibu za Chama chao cha CCM ,kujiunga na upinzani ni mwanzo wa kuigawa hadharani CCM.
Kuna fununu kuwa baadhi ya viongozi wa juu wastaafu wa serikali zilizopita za CCM huenda wakajiunga na Chama Cha Wananchi (CUF) ili kukipa tafu chama hicho baada ya kuchoshwa na matatizo yanayoibuka kila siku yanayokikumba chama tawala CCM,pia baadhi yao wamesikika wakisema wanafikiria kujiunga na vyama vingine lakini bado hawajaamua kutokana na migongano inayoibuka ndani ya vyama hivyo tofauti na CUF ambacho kimeonekana kutulia kabisa na hakina usongo na viongozi wanaohama au kuhamia,jambo ambalo limewafanya vigogo hao kuifanya CUF kuwa ndio chaguo lao.
Ingawa CUF imewataka vigogo hao kutulia huko waliko mpaka wakati muafaka utakapofika ndipo watangaze rasmi kuachana na CCM na UCCM ,hali sivyo ilivyo kwa wateja hao ambao hamu ya kubwaga manyanga ya Uccm imewazidi na kuona kama wanadhulumiwa kuambiwa wakati wa kujiunga haujaiva ,inaonyesha subira itawashinda.
Nawapa hongera wale wote ambao wameanza kuona mwanga na kuona ubovu na uzembe bila ya kusahau ubaya wa CCM ambao leo hii hauhitaji mistari mingi kuelezewa mwananchi , wala haihitajiki kamati kuchunguza sera mbovu za CCM ambazo zimeshindwa kutekelezeka na kubaki kuwa ni mikakati ambayo kila siku inapangiwa miyaka ,eti mkakati baada ya miaka mia !!!
Ni matumaini ya kila Mtanzania kuwa endapo vigogo hao ambao wameonekana kuwa mstari wa mbele katika kukinzana na wenzao na pia kuonekana kujitenga kwa kukemea mambo ambayo hayaendani na taratibu za Chama chao cha CCM ,kujiunga na upinzani ni mwanzo wa kuigawa hadharani CCM.
Kuna fununu kuwa baadhi ya viongozi wa juu wastaafu wa serikali zilizopita za CCM huenda wakajiunga na Chama Cha Wananchi (CUF) ili kukipa tafu chama hicho baada ya kuchoshwa na matatizo yanayoibuka kila siku yanayokikumba chama tawala CCM,pia baadhi yao wamesikika wakisema wanafikiria kujiunga na vyama vingine lakini bado hawajaamua kutokana na migongano inayoibuka ndani ya vyama hivyo tofauti na CUF ambacho kimeonekana kutulia kabisa na hakina usongo na viongozi wanaohama au kuhamia,jambo ambalo limewafanya vigogo hao kuifanya CUF kuwa ndio chaguo lao.
Ingawa CUF imewataka vigogo hao kutulia huko waliko mpaka wakati muafaka utakapofika ndipo watangaze rasmi kuachana na CCM na UCCM ,hali sivyo ilivyo kwa wateja hao ambao hamu ya kubwaga manyanga ya Uccm imewazidi na kuona kama wanadhulumiwa kuambiwa wakati wa kujiunga haujaiva ,inaonyesha subira itawashinda.
Nawapa hongera wale wote ambao wameanza kuona mwanga na kuona ubovu na uzembe bila ya kusahau ubaya wa CCM ambao leo hii hauhitaji mistari mingi kuelezewa mwananchi , wala haihitajiki kamati kuchunguza sera mbovu za CCM ambazo zimeshindwa kutekelezeka na kubaki kuwa ni mikakati ambayo kila siku inapangiwa miyaka ,eti mkakati baada ya miaka mia !!!