CUF kumuunga mkono mgombea wa CCM Mbeya, et tu Brutus ?

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Mbeya Mjini, Yasin Mrotwa amesema hivi sasa wanaendelea na mazungumzo na mmoja wa wanachama wa CCM, Prince Mwaihojo kumuomba ili asimame kugombea ubunge wa Mbeya Mjini kwa niaba ya vyama hivyo.

Naona CUF yazidi kumeremeta katika ndoa yake na CCM - ndoa yazidi kunoga !
 
mbona hilo liko Waazi, ila Mbeya Mjini na Vijijini hata wafanyaje CCM WANADONDOKA, WAOMBE NGUVU HATA YA MREMA, MTIKILA, WAHARIRI WA HABARI COOPERATION, na wajinga wengine.
 
mbona hilo liko Waazi, ila Mbeya Mjini na Vijijini hata wafanyaje CCM WANADONDOKA, WAOMBE NGUVU HATA YA MREMA, MTIKILA, WAHARIRI WA HABARI COOPERATION, na wajinga wengine.

Habari ndiyo hii hapa !

Vyama saba vya upinzani vimeamua kuunda ushirikiano na kumsimamisha mgombea ubunge mmoja katika Jimbo la Mbeya Mjini huku vikitangaza kuwaunga mkono wagombea wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika majimbo mawili ya Rungwe Mashariki linalogombewa na Profesa Mark Mwandosya na Kyela linalowaniwa na Dk Harrison Mwakyembe.

Akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari jijini Mbeya, Mwenyekiti wa umoja huo ambaye pia ni Mwenyekiti APPT Maendeleo wilaya ya Mbeya Mjini, Godfrey Devis alisema wameamua kusimamisha mgombea mmoja atakaye pambambana na mgombea wa CCM, kwa lengo la kuweka mbele maslahi ya wananchi wa Mbeya.

Alisema kaulimbiu ya umoja huo ni 'Mbeya kwanza, vyama baadaye' na ndio sababu wanaangalia zaidi uwezo wa mgombea, dhamira ikiwa ni kuwatumikia wananchi wa Mbeya ili kuwaletea maendeleo.
Vyama hivyo vilivyoamua kushirikiana kusimamisha mgombea mmoja wa ubunge katika jimbo la Mbeya Mjini ni Chama cha Wananchi (CUF), NCCR- Mageuzi, UDP, TADEA, SAU, APPT- Maendeleo na TLP.


Devis alisema kwa vile kaulimbiu yao ni Mbeya kwanza na vyama baadaye, wanaamini Dk. Mwakyembe na Profesa Mwandosya ni watu wenye uwezo mkubwa wa kuwaletea wana-Mbeya maendeleo na ni wapambanaji wa vita dhidi ya ufisadi ambao umelitafuna taifa, ndio sababu wamekubaliana kwa kauli moja kuwaunga mkono.

"Tumeamua kwa dhati kushirikiana vyama hivi vyote saba kusimamisha mgombea mmoja mwenye uwezo na nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo," alisema Devis.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Mbeya Mjini, Yasin Mrotwa alisema hivi sasa wanaendelea na mazungumzo na mmoja wa wanachama wa CCM, Prince Mwaihojo kumuomba ili asimame kugombea ubunge wa Mbeya Mjini kwa niaba ya vyama hivyo.

Alisema utafiti wao unaonyesha kuwa Mwaihojo ambaye pia ni mwenyekiti wa mtandao wa wasomi wa Mkoa wa Mbeya anakubalika na umma wa wananchi wa Mbeya hivyo endapo atakubali ombi lao atakuwa ni mtu sahihi wanayeamini kuwa anastaihili kupewa ridhaa ya kuliongoza jimbo la Mbeya Mjini.

Kuhusiana na nafasi za madiwani, Mrotwa alisema wagombea wote watachukua fomu ndani ya vyama vyao na baada ya utafiti watakaofanya, watakuwa wakimuachia mgombea wa chama kinachokubalika zaidi katika kila kata.

Naye Mwenyekiti wa Mipango na Uchumi wa NCCR Mageuzi, Agabo Mwakatobe alisema ushirikiano wa vyama waliouanzisha Mbeya, utakuwa mfano wa kuigwa nchini, kwa sababu kwa mara ya kwanza Mbeya itakuwa na mbunge wa kitaifa anayeungwa mkono na vyama saba.

Mwakatobe alisema wanachama wa vyama vya CCM na Chadema wenye nia ya dhati ya kujikomboa kiuchumi na kimaendeleo pia wanakaribishwa kuingia kwenye ushirikiano huo ili kuongoze nguvu itakayofanya apatikane mbunge wanayemtaka na anayekubalika na wanachi.


CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Habari ndiyo hii hapa !

Vyama saba vya upinzani vimeamua kuunda ushirikiano na kumsimamisha mgombea ubunge mmoja katika Jimbo la Mbeya Mjini huku vikitangaza kuwaunga mkono wagombea wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika majimbo mawili ya Rungwe Mashariki linalogombewa na Profesa Mark Mwandosya na Kyela linalowaniwa na Dk Harrison Mwakyembe.
Akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari jijini Mbeya, Mwenyekiti wa umoja huo ambaye pia ni Mwenyekiti APPT Maendeleo wilaya ya Mbeya Mjini, Godfrey Devis alisema wameamua kusimamisha mgombea mmoja atakaye pambambana na mgombea wa CCM, kwa lengo la kuweka mbele maslahi ya wananchi wa Mbeya.
Alisema kaulimbiu ya umoja huo ni 'Mbeya kwanza, vyama baadaye' na ndio sababu wanaangalia zaidi uwezo wa mgombea, dhamira ikiwa ni kuwatumikia wananchi wa Mbeya ili kuwaletea maendeleo.
Vyama hivyo vilivyoamua kushirikiana kusimamisha mgombea mmoja wa ubunge katika jimbo la Mbeya Mjini ni Chama cha Wananchi (CUF), NCCR- Mageuzi, UDP, TADEA, SAU, APPT- Maendeleo na TLP.
Devis alisema kwa vile kaulimbiu yao ni Mbeya kwanza na vyama baadaye, wanaamini Dk. Mwakyembe na Profesa Mwandosya ni watu wenye uwezo mkubwa wa kuwaletea wana-Mbeya maendeleo na ni wapambanaji wa vita dhidi ya ufisadi ambao umelitafuna taifa, ndio sababu wamekubaliana kwa kauli moja kuwaunga mkono.
"Tumeamua kwa dhati kushirikiana vyama hivi vyote saba kusimamisha mgombea mmoja mwenye uwezo na nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo," alisema Devis.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Mbeya Mjini, Yasin Mrotwa alisema hivi sasa wanaendelea na mazungumzo na mmoja wa wanachama wa CCM, Prince Mwaihojo kumuomba ili asimame kugombea ubunge wa Mbeya Mjini kwa niaba ya vyama hivyo.
Alisema utafiti wao unaonyesha kuwa Mwaihojo ambaye pia ni mwenyekiti wa mtandao wa wasomi wa Mkoa wa Mbeya anakubalika na umma wa wananchi wa Mbeya hivyo endapo atakubali ombi lao atakuwa ni mtu sahihi wanayeamini kuwa anastaihili kupewa ridhaa ya kuliongoza jimbo la Mbeya Mjini.
Kuhusiana na nafasi za madiwani, Mrotwa alisema wagombea wote watachukua fomu ndani ya vyama vyao na baada ya utafiti watakaofanya, watakuwa wakimuachia mgombea wa chama kinachokubalika zaidi katika kila kata.
Naye Mwenyekiti wa Mipango na Uchumi wa NCCR Mageuzi, Agabo Mwakatobe alisema ushirikiano wa vyama waliouanzisha Mbeya, utakuwa mfano wa kuigwa nchini, kwa sababu kwa mara ya kwanza Mbeya itakuwa na mbunge wa kitaifa anayeungwa mkono na vyama saba.
Mwakatobe alisema wanachama wa vyama vya CCM na Chadema wenye nia ya dhati ya kujikomboa kiuchumi na kimaendeleo pia wanakaribishwa kuingia kwenye ushirikiano huo ili kuongoze nguvu itakayofanya apatikane mbunge wanayemtaka na anayekubalika na wanachi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI


Sijawahi kusikia nonsense kama hii kutoka kwa baadhi ya Watanzania. Hivyo vyama vyote vilivyotajwa ni CCM-B, vionatumiwa na chama tawala -- kwa pesa of course -- kudhoofisha dhoruba tarajiwa la Chadema! Na mbinu hizi tutazisikia sana katika uchaguzi huu. Nashangaa DP ya Mtikila haimo katika umoja huo -- nadhani kasahauliwa tu kutajwa. Juzi juzi alilipiwa deni na CCM ili asiende jela -- na sasa hivi keshaanza kazi ya kurudisha fadhila kwa chama hicho -- kupiga vita upinzani na lengo hasa ni Chadema.
 
Sijawahi kusikia nonsense kama hii kutoka kwa baadhi ya Watanzania. Hivyo vyama vyote vilivyotajwa ni CCM-B, vionatumiwa na chama tawala -- kwa pesa of course -- kudhoofisha dhoruba tarajiwa la Chadema! Na mbinu hizi tutazisikia sana katika uchaguzi huu. Nashangaa DP ya Mtikila haimo katika umoja huo -- nadhani kasahauliwa tu kutajwa. Juzi juzi alilipiwa deni na CCM ili asiende jela -- na sasa hivi keshaanza kazi ya kurudisha fadhila kwa chama hicho -- kupiga vita upinzani na lengo hasa ni Chadema.

Mtikila safari hii kamkubali Dr. P. W. Slaa na kawaomba Watanzania wamuunge mkono kuung'oa huo zizi wa fitina - big up Mtikila, saa ya ukombozi ni sasa !
 
Sijawahi kusikia nonsense kama hii kutoka kwa baadhi ya Watanzania. Hivyo vyama vyote vilivyotajwa ni CCM-B, vionatumiwa na chama tawala -- kwa pesa of course -- kudhoofisha dhoruba tarajiwa la Chadema! Na mbinu hizi tutazisikia sana katika uchaguzi huu. Nashangaa DP ya Mtikila haimo katika umoja huo -- nadhani kasahauliwa tu kutajwa. Juzi juzi alilipiwa deni na CCM ili asiende jela -- na sasa hivi keshaanza kazi ya kurudisha fadhila kwa chama hicho -- kupiga vita upinzani na lengo hasa ni Chadema.

kwanza ni vyama vinavyosubiri uchaguzi, hatusikii harakati zozote baada ya uchaguzi, unaungana na TLP ya Mrema kutafuta nini ? CUF ndo hao waliomwekea kauzibe Mgombea wa CHADEMA uchaguzi ule wa Mbeya vijijini, ambapo CUF iliumbuka vibaya.
Binafsi hivyo ni vyama vinavyokufa, vinavyosubiri huruma ya ccm KUWEZA KUISHI.
 
Hivi wanataka huyo Prince awakilishe chama kipi? Atagombea kama chaguo la shirikisho la vyama vya upinzani ambaye bado ni mwanachama hai wa CCM?

Amandla.......
 
Hiyo habari haijakaa sawa,ina mgongano ndani ya habari yenyewe,ieke sawa kwanza,maana naona Cuf wamo ktk sehemu mbili kutokana na maelezo yako,au wewe ndo ktk wale wale?
 
mbona hilo liko Waazi, ila Mbeya Mjini na Vijijini hata wafanyaje CCM WANADONDOKA, WAOMBE NGUVU HATA YA MREMA, MTIKILA, WAHARIRI WA HABARI COOPERATION, na wajinga wengine.

Ukiangalia vizuri demographic ya jimbo la Mbeya Mjini utajua jinsi ilivyo vigumu kumshinda Mwl. Benson Mpesya kutokana na kabila lake lakini pia ukizingatia kuwa Prof. Mwandosya na Dr. Mwakyembe watakuwa pamoja nae.
 
Halafu kuna watu hapa kila siku wanatoa pumba (mimi naziita propaganda za ccm) kuwa wapinzani waungane. HIvi ukiungana na wanafiki kama hawa ndio utategemea kushinda kweli?
 
Halafu kuna watu hapa kila siku wanatoa pumba (mimi naziita propaganda za ccm) kuwa wapinzani waungane. HIvi ukiungana na wanafiki kama hawa ndio utategemea kushinda kweli?

Kweli Mkuu, CUF iungane na Chadema wakati huo huo imeshachagua mwenza CCM, hao mafahali wawili watawezaje kuishi kwenye zizi moja ! Wakati Chadema wanajipanga kuung'oa utawala wa kifisadi wa CCM, CUF wanajipanga kushirikiana nao ! Hapana Chadema, CUF ni ya kuogopwa kama ukoma.
 
hongera mbeya......ningekuwa huko you could count my vote on your side!.........hawa wengine wasioonyesha dalili za umoja waacheni wagalagazwe.......nawaombeeni ushindi na ushindi huo nitasherehekea nanyi......huku wasikoungana nitashirikiana na waliowashinda kuwazomea.........UCHU WA MADARAKA UNAWALA.........MBEYA KWANZA VYAMA BAADAYE.......TANZANIA KWANZA VYAMA BAADAYE...!
 
Back
Top Bottom