Kaamua kumtumikia shetani
Mwenzake yupo kijitonyama kajificha anachungulia lipumbaa anavyo teswa na usalitiLipumba Ni yuda iskarioti
Professor ndio ana njaa ya kuzidihivi kati ya lipumba na wewe nani ananjaa jamani ..kuwa muwazi
Kwa wana lumumba lazima mumchukie maalimKwa hii fukuzafukuza Maalim amekurupuka, angetumia hekima na busara katika kuumaliza mgogoro. Na hapa badala ya kuutatua mgogoro ndio ameuchochea. Ametengeneza mgogoro na CUF Bara. Sipati picha jinsi Wabunge wa Bara na Visiwani watakavyoweza kuishi ndani ya Bunge. Sipati picha jinsi dhana ya UKAWA itakavyoweza kutekelezwa ndani ya Bunge wakati mshirika mwenza amejigawanya. Hapa kutakuwa na hali ya kutokuaminiana kati ya Wabunge wa Chama kimoja. Je CDM atashirikiana na CUF Zanzibar au CUF Bara? Ni ngumu kumeza! Kwa ujumla Maalim ametibua badala ya kujenga Umoja ndani ya CUF.
Na huo ndio muarobaini wa kushindana na siasa za maji taka kwani ccm watashindwa kujipenyeza kwenye huo muungano wa chama kimojaNa kwa kufanya hivyo kwa maoni yangu atafanikiwa kutimiza lengo la kuidhoofisha CUF na pia UKAWA. CHADEMA na CUF wasiotumika na maccm au ambao si mamluki watafanya jambo la maana sana kuamua kuungana na vyama vyote ndani ya UKAWA na hivyo kuunda chama kimoja chenye nguvu bila kuchelewa. Wakiweza kufanya hivyo lengo la Lipumba na waliomtumia ndani ya CCM litakuwa limeshindwa vibaya sana.
Kwa hili napingana nawe kwa asilimia mia mojaKinachokiua Cuf bara ni ubaguzi wa Maalim Seif na Chadema wanachochea kwa kutaka wao ndio waonekane chama pekee cha upinzani chenye nguvu wameshakiua Nccr na sasa wanakishughulikia Cuf
Hii project nzima inadhaminiwa na kitengo kwa ujanja sana huku kikijitahidi kutaka kukipaka CHADEMA matope lakini mwisho wa siku ukweli utatamalaki kwakuwa siku zote kitu cha kupanga huacha alama za makosa zisizofutikaKwa wana lumumba lazima mumchukie maalim
Si amefurahi kutupiliwa mbali mahasim wakeKwa maana ipi
Siwezi kuliona lakini wewe umeliona!Kuhusu Ubaguzi wa Maalim hiyo ni dhairi kabisa wala halihitaji tochi kwani hata hiyo Cuf kuwa bara ni kwa vile tu sheria ya usajili wa vyama vya siasa inalazimisha chama kuwa katika sura ya muungano maana hata kwenye uchaguzi nguvu kubwa imeelekezwa Zanzibar ikiwa ni pamoja na bajeti kubwa inatengwa huko kuliko bara hivyo maalim Seif haoni hasara Cuf bara ikafa na hilo lingine ni jambo linafanywa kimkakati zaidi kijuu juu huwezi kuona
Ccm inajua wazi nguvu ya CUF visiwani na nguvu ya CHADEMA bara ! Kushamiri kwa hivi vyama kila upande kwa vyovyote vile sio habari njema kwa ccmCUF inahitaji mtu kama Maalim Seif siyo pr njaa, kuendesha upinzani Afrika siyo kazi nyepesi ati. Tatizo huwa chama tawala kuweka mapandikizi.Viva Seif, viva UKAWA.
Ndomana mnaishia kuwashika akili wenye njaa ya pesa na akili..mmchukue Lipumba mmpe usajili si ndo mnamwaminisha anawezaNdiyo cdm walilipia ukumbi wa mkutano wa cuf na kumfadhili pesa wapambe wa seif
Naona fikra kiduchu ndizo zinazokuhangaisha. Kama ungekuwa na upeo thabiti ungaliona jinsi katiba inavyonyong'onywezwa na kufinyangwa. Mwanzoni mlinyanyasa sana Mzee James Mapalala mpaka akakata tamaa na akaamua kuondoka, lakini kwa huu mziki ulivyo mnene, HATOKI MTU!Upeo wako ni mdogo., siku zote ni bora chama kuliko yooote hayo uliyoeleza, chama kibaki hai na salama kisiasa ndio kitu nyeti tunachoangalia.,
Tanzania ni kubwa, wasomi wapo wengi, there are so many Prof.Lipumba, hao kina Sekaya ndo kabisa, ni bora kujenga chama kikawa imara zaidi. Lipumba aanzishe chama chake na taasisi yake huko Bara, ukitaka kujuwa kilichomkuta HR Lipumba ni zaidi. HR alitarajiwa kuwa mrithi wa maalim seif leo Zanzibar ukimtaja HR hakuna anayemjuwa ni kwa sababu chama kilifanya maamuzi magumu na kuijenga CUF ya sasa.
CUF tokea imeanzishwa ni chama pekee cha upinzani Tz kilicho madhubuti na kinazidi kupiga hatua kila uchao. Katika taasisi hakuna mtu mkubwa zaidi kuliko taasisi, Lipumba alihisi CUF ni yeye na yeye ndo CUF. mwache ajifunze aendako.