Kitombise
JF-Expert Member
- Sep 24, 2013
- 8,287
- 24,318
Cristiano Ronaldo amewashinda wachezaji
Antoine Griezman na Gareth Bale na kutwaa tuzo
ya mchezaji bora wa Ulaya kwa upande wa
wanaume. Ushindi huu umetokana na mafanikio
yake msimu uliokwisha huku akiwa ametwaa
vikombe vikubwa vya ulaya kwa maana klabu
bingwa ulaya na kombe la mataifa ya Ulaya.
Ronaldo pia alikuwa mfungaji bora wa Ulaya
huku akiwa wa pili kwa ufungaji katika ligi kuu
ya nchini Hispania. Ikumbukwe pia, Ronaldo
alifika fainali hizi huku mpinzani wake akiwa ni
Antoine Griezman na kumshinda kote ijapokuwa
kwenye fainali ambayo Ureno walitwaa ubingwa
aliumia mapema sana.
Ronaldo alifunga mabao 51 kwenye mechi 48
msimu uliopita huku akifunga mabao 3 pekee
kwenye mashindano ya mataifa ya Ulaya
ambapo mchezaji Antoine Griezman alikuwa
mfungaji bora.
Antoine Griezman na Gareth Bale na kutwaa tuzo
ya mchezaji bora wa Ulaya kwa upande wa
wanaume. Ushindi huu umetokana na mafanikio
yake msimu uliokwisha huku akiwa ametwaa
vikombe vikubwa vya ulaya kwa maana klabu
bingwa ulaya na kombe la mataifa ya Ulaya.
Ronaldo pia alikuwa mfungaji bora wa Ulaya
huku akiwa wa pili kwa ufungaji katika ligi kuu
ya nchini Hispania. Ikumbukwe pia, Ronaldo
alifika fainali hizi huku mpinzani wake akiwa ni
Antoine Griezman na kumshinda kote ijapokuwa
kwenye fainali ambayo Ureno walitwaa ubingwa
aliumia mapema sana.
Ronaldo alifunga mabao 51 kwenye mechi 48
msimu uliopita huku akifunga mabao 3 pekee
kwenye mashindano ya mataifa ya Ulaya
ambapo mchezaji Antoine Griezman alikuwa
mfungaji bora.