CRDB wakataa fedha za mteja!

Mwitongo

JF-Expert Member
Jan 30, 2009
312
360
Ndugu zangu, katika hali isiyo ya kawaida, leo nimeshuhudia tukio la kusikitisha. Nilikuwa katika Benki ya CRDB, Tawi la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam; nimeshuhudia mhudumu wa dirisha namba 2 akikataa kupokea fedha za mteja mmoja kijana. Kisa ni kwamnba kijana huyo alikuwa na fedha nyingi za Sh 50, 100 na 200 ambazo kwa kawaida ni sarafu. Mhudumu amekataa kuzipokea kwa maelezo kwamba hawapokei "masimbi". Akamtaka kijana huyo azipeleke kwa makondakta wa daladala, azibadili ili wampe noti, au masimbi hayo ayapeleke BoT. Kukawa na vuta nikuvute, mwisho yule kijana akaondoka bila kuweza fedha kwenye akaunti.

Hoja: Hii ni sahihi kwa benki kukataa kupokea sarafu? Je, sarafu hazitambuliwi kama fedha halali hapa nchini? Naomba wadau tulijadili suala hili.

Nawasilisha.
 
Ndugu zangu, katika hali isiyo ya kawaida, leo nimeshuhudia tukio la kusikitisha. Nilikuwa katika Benki ya CRDB, Tawi la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam; nimeshuhudia mhudumu wa dirisha namba 2 akikataa kupokea fedha za mteja mmoja kijana. Kisa ni kwamnba kijana huyo alikuwa na fedha nyingi za Sh 50, 100 na 200 ambazo kwa kawaida ni sarafu. Mhudumu amekataa kuzipokea kwa maelezo kwamba hawapokei "masimbi". Akamtaka kijana huyo azipeleke kwa makondakta wa daladala, azibadili ili wampe noti, au masimbi hayo ayapeleke BoT. Kukawa na vuta nikuvute, mwisho yule kijana akaondoka bila kuweza fedha kwenye akaunti.

Hoja: Hii ni sahihi kwa benki kukataa kupokea sarafu? Je, sarafu hazitambuliwi kama fedha halali hapa nchini? Naomba wadau tulijadili suala hili.

Nawasilisha.

Angeenda kwa meneja sidhani kama kuna policy ya benk ya kukataa sarafu
 
Kwani wewe unazijua haki zako ukiwa kama customer wa bank? Ukizijua hapo itakuwa rahisi kudeal na hiyo issue
 
hakuna mtu yeyote mwenye mamlaka ya kukataa hela kwani hela ni mali ya serikali na ni malipo halali kwa huduma itolewayo kwa wakati huo hivyo huyo muhudumu wa bank amekosea sana

Hoja: Hii ni sahihi kwa benki kukataa kupokea sarafu? Je, sarafu hazitambuliwi kama fedha halali hapa nchini? Naomba wadau tulijadili suala hili.

Nawasilisha.[/QUOTE]
 
Sio halali kukataa fedha za sarafu, alichotakiwa ni kupokea alafu kumshauri kwamba siku nyingine kama ataweza awe anawapa watu chenji kwa kuwa hizo fedha za sarafu huwa zinatumika sana kwenye mzunguuko wa fedha wa kila siku (though si lazima azipeleke huko)
 
Ni fedha halali na bank hawatakiwi kukurudisha kisa coin
tena wao ndo inabidi wazichukue na kuzipeleka BOT
 
Tatizo ni incompetency ya hawa wahudumu wa benki, ukichunguza kwa undani utashangaa huyo kasomea ualimu grade A au kitu kingine na kwakuwa ana refa basi kapata kazi Benki na kapewa siku mbili za training na sasa anapiga mzigo. Hawezi kuwa anayajua maadili ya kibenki mhudumu kama huyo!!!!
A%20S%20angry.gif
 
Ndugu zangu, katika hali isiyo ya kawaida, leo nimeshuhudia tukio la kusikitisha. Nilikuwa katika Benki ya CRDB, Tawi la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam; nimeshuhudia mhudumu wa dirisha namba 2 akikataa kupokea fedha za mteja mmoja kijana. Kisa ni kwamnba kijana huyo alikuwa na fedha nyingi za Sh 50, 100 na 200 ambazo kwa kawaida ni sarafu. Mhudumu amekataa kuzipokea kwa maelezo kwamba hawapokei "masimbi". Akamtaka kijana huyo azipeleke kwa makondakta wa daladala, azibadili ili wampe noti, au masimbi hayo ayapeleke BoT. Kukawa na vuta nikuvute, mwisho yule kijana akaondoka bila kuweza fedha kwenye akaunti.

Hoja: Hii ni sahihi kwa benki kukataa kupokea sarafu? Je, sarafu hazitambuliwi kama fedha halali hapa nchini? Naomba wadau tulijadili suala hili.

Nawasilisha.

Haya ndio matokeo ya output za kutoka UDOM. Tutashuhudia mengi.
 
Daah! hii ni mbaya sana hasa kwenye ushindani huu wa biashara. Huyo teller hajafanya vizuri hasa kwa kubishana na mteja dirishani hadi wateja wengine waliokaa nyuma wamejua nini kimeendelea. Tatizo ajira za sikuhizi ni kwa kujuana na vimemo kwa sana matokeo yake customer care hakuna na wala hawajali as wanajua wana god father anawalinda na ajira hata akimjibu mteja vibaya hawezi kupoteza ajira.
Makeshia au staff kwa ujumla wanaajiriwa bila kufanyiwa training hivyo hawajui wajibu wao kwa mteja, inawezekana ukaongea na mteja kwa lugha ambayo yeye mwenyewe anakubali kupeleka fedha hizo benki kuu bila kulalama ila makeshia wengi wamekuwa na kauli chafu na hii kufanya wateja kuchukia na kukimbia benki.
Kwa ufahamu wangu mimi mdogo kuhusu benki kutokana na elimu yangu ya awali, benki inawajibui wa kupokea fedha halali kutoka kwa mteja iwapo mteja huyo amefungua akaunti na benki husika, ikiwa si mteja kuna masharti yanatakiwa kufuatwa. Benki itakataa kupokea fedha isiyo halali au fedha feki tu kutoka kwa mteja bila kuwa na kosa ila kukataa kupokea fedha kutoka kwa mteja kwa sababu ni coins hilo ni kosa kubwa.
Kingine ninachofahamu kuhusu cash ni kuwa keshia anapofunga jioni anatakiwa kurudhisha fedha strong room kwenye bandles la kuanzia 10,000/=, milioni kumi 5,000/= milioni tano 2,000/= milioni mbili 1,000/= milioni moja 500/= laki tano hivyo ikifika jioni kama keshia ana noti yoyote ambayo haijafikia bandle kama nilivonyambulisha hapo juu anatakiwa kubaki nazo kama cash on hand na kesho anaanza nazo biashara na kwenye coin ili ziingie strong room anatakiwa 200 ziwe laki 2, 100 ziwe laki 1 50 ziwe elf 50, 20 ziwe elf 20 na 10 ziwe elf kumi ndo wnapokea sasa hawa makeshia wanakataa kupokea coin ambazo hazijatimia kwenye mafungu kwani wanajikuta wanakaa nazo mda mrefu kama cash on hand na hivo kupata audit query. Good customer care kama mteja anaakaunti na benki hiyo keshia alitakiwa kuzipokea na kinyume chake mteja unaweza kuishitaki benki. Kama mteja hauna akaunti unamuwekea mtu mwingine kuna charge utachajiwa na fedha zinatakiwa kupokelewa, labda kama alikuwa anataka abadilishiwe kutoka kwenye koin kwenda kwenye noti hilo ni suala lingine ambalo ni sawa na kuchange dola to tsh.
Ila lugha nzuri ikitumika kumuelewesha haya mteja hatalalamika na tena alitakiwa amuite pembeni na si kubishana nae akiwa dirishani.
Nawakilisha.
Ever remeining,
Ever loving,
Sakapal
 
Ndio Customer Care ya Taasisi zetu. Mara narudisha Bidhaa sina Chenji, mara sipokei Sarafu!
 
Siungemwambia /ungemsaidia kwa meneja? Ndo masuala ya kuajiri watu wasio na uhusika wa kazi.
 
Kiukweli ukilinganisha na mibank mingi, CRDB ni Bank inayomsikiliza mteja. Siku zote kwenye msafara wa mamba na kenge wamo. Kwa hiki kilichotokea, itabidi wafanyakazi wote wapigwe msasa.
 
Watanzania ushirikiano ni zero kabisa wewe umeshindwa nini kumshauri pamoja na wenzio angalau amuone hata meneja muhusika kuliko kumuacha akaondoka bila kupata huduma?
 
Back
Top Bottom