britanicca
JF-Expert Member
- May 20, 2015
- 15,636
- 30,004
Taarifa kwa Umma
Kumekuwa na taarifa ya akaunti ya kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) inayosambaa mitandaoni ikionyesha miamala iliyofanywa kwenye akaunti yake ya benki.
Tunapenda kujulisha umma kuwa taarifa hiyo ya akaunti ambayo imeihusisha Benki yetu ya CRDB si ya kweli na kuendelea kuisambaza ni kosa la jinai.
Benki yetu imeshairipoti kwa vyombo husika vya dola ili uchunguzi wa kina ufanyike na hatua stahiki zichukuliwe dhidi wote wanaohusika na kitendo hiki.
Benki ya CRDB inapenda kuwakumbusha wateja wake na umma kuwa Benki inaendeshwa kwa misingi ya kanuni na sheria na siku zote taarifa za mteja zitabaki kuwa kati ya mteja na Benki.
Imetolewa na Idara ya Mawasiliano na Uhusiano
Benki ya CRDB