CPA siku hizi bado ina advantage?

CPA siku hizi bado ina advantage?

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,302
Habari za saa wakuu mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa pili nasomea accounting and finance, nawaza sana kuhusu ajira baada ya kutoka hapa, nilikua na wazo la kwenda kuchukua CPA baada ya kumaliza chuo mwakani, lakini nasikia siku hizi watu wanaziponda hadi mwenyewe naanza kua na wasiwasi kuhusu umuhimu nwake siku hizi, vp, bado zina dili?
 
Jiulize kwanza wanaoponda wanazo? CPA inamata milele but they don't reward they award so don't say ngoja nikuchukue sema nkatafute
 
Notes za cpa zinafungiwa Chapati na maandazi uswahilini changanya akili zako na za darasani utaelewa
 
Cpa ni leseni inayokuwezesha kufanya kazi za kihasibu ambazo haziwezi kufanywa na mtu yeyote yule hata kama ni profesa wa akaunts.
Ni kwamba kama unataka kuuza profesional yako kama wanavyofanya madaktari na wanasheria ni lazima uwe na cpa...pia mtu mwenye cpa hawezi kulipwa pesa ndogo kuliko amb ambaye hana hiyo cpa kwa taasisi ambazo zipo huru.
 
Cpa ni leseni inayokuwezesha kufanya kazi za kihasibu ambazo haziwezi kufanywa na mtu yeyote yule hata kama ni profesa wa akaunts. Ni kwamba kama unataka kuuza profesional yako kama wanavyofanya madaktari na wanasheria ni lazima uwe na cpa...pia mtu mwenye cpa hawezi kulipwa pesa ndogo kuliko amb ambaye hana hiyo cpa kwa taasisi ambazo zipo huru.
Mkuu upo sahihi na mifano yako inatosha hata kum-elekeza Kipofu. CPA Professional Degree hiyo anayosomea ni Academic Degree hivyo hauwezi kutambulika kimataifa au kitaifa kama wewe ni Mhasibu mpaka pale utapokua na CPA kwa maana uhasibu unaundwa ktk Misingi ya International standards hivyo kama unatamani kuwa Mhasibu na sio Mhasibu msaidizi basi CPA ndio jibu.
 
Kweli vijana kazi ipo! Kuna kazi bila kuwa CPA Holder huwezi kufanya kisheria,Kama wewe ni mhasibu na ndoto zako ni kuwa mhasibu na si karani wa uhasibu CPA/ACCA/ACA haikwepeki!
 
If u will have enough money kasome ACCA,its more marketable.
 
If u will have enough money kasome ACCA,its more marketable.

Siku hizi watu wanaangalia uwezo sio aina ya cheti hayo ya ACCA kufagiliwa sana ilikuwa enzi zile NBAA wanatumia TFAS while ulimwengu ulikuwa ktk IFRS! Kwasasa NBAA inatambulika IFAC ambao ni shirikisho la bodi za uhasibu ulimwenguni na hawa wakikutambua kila mwanachama wake lazima akutambue na uweze kufanya kazi popote walipo wanachama wake (ingawa huwezi kuzuia upendeleo kwa nchi husika).

Zamani Foreigners wengi walikuwa wanaogopa watu wa CPA sababu mitaala ilikuwa ni local.Ingawa ukweli unabaki kuwa ACCA ni bodi kubwa zaidi na ya kisasa lakini ule umuhimu uliokuwa unawapa credit over CPAs haupo kwa sasa imebaki mazoea tu.

Jitahidini kusoma vizuri na kupata uzoefu ndio ngao kwenu na si kusoma sijui ACCA,ACA n.k!
 
Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa pili nachukua accounting and finance, nawza sana kuhusu ajira baada ya kumaliza chuo mwakani, ningependa mnisaidie kunijulisha hivi siku hizi mtu ukiwa na cpa bado inasaidia au ni useless maana nataka nikishamaliza masomo yangu nikachukue na cpa lakini nasikia watu wanaziponda hadi naanza kua na wasiwasi kwamba ni bure tu siku hizi, naomba majibu wadau

Acha mawazo ya kizamani wewe...... Kumbe pamoja na usomi wooote huo bado unamawazo ya enzi za kuajiriwa!!!!! Unasoma ili ukaajiriwe na "wahindi......." Wakunyonye mshahara ndo utachekelea? Badala ya kusoma ili uelewe mambo kisha ukajiajiri wewe unataka CPA ili ukaajiriwe..... Ili upate mshahara wa nusu milioni kwa mwezi....wakati kumbe unao uwezo wa kupata milioni 20 kwa mwezi!!!! Acha unyonge wewe.....
Sasa nakupa ushauri:
1). Soma digrii yako ya accounting and finance
2). Kisha soma CPA
Halafu baada ya kuhitimu USIAJIRIWE KABISA!!! Tena hata ile ajira ya "kujishikiza usijaribu, acha....
Nenda Mamlaka ya Mapato Tanzania ukajisajili kama Tax Consultant. Kwa mujibu wa maelezo yako, wewe uko elligible kusajiliwa kama tax consultant chini ya kifungu cha 134 na regulation 37 ya sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004. Fanya kazi kama tax consultant miaka mitatu kisha nenda NBAA (assuming tayari una CPA) wao watakusajili kama certified public accountant. Utakuwa unatengeneza mahesabu ya watu na pia kuwafanyia ushauri wa masuala ya kodi.
Nakuhakikishia hutatamani tena kuajiriwa..... Pesa utakayoipata kwa kipindi cha miaka ya mwanzo (miaka mitano mpaka kumi hivi) ni pesa ambayo hutakuja uipate kwa kuajiriwa hata kama utafanya kazi miaka sabini!!!! Amini nikuambiayo mimi.
Kama haitoshi naomba uni PM nikuelekeze zaidi....
 
Niko bize kidogo ,
Naweza kukutuma unichukulie na Mimi? ?
 
Ha ha ha ha oh my lord.hoya CPA siyo unaitafuta kama pipi,eti nikachukue,tuliyoifanya tunajua,huipati kiboyaboya.na weka akilin bila CPA hutambulik as profesional mhasibu,mbona hata CAG wako alitamka hicho kitu ludovic,wasio na CPA hawatambuliki,soma na magazeti sio uje kutuchosha.
 
CPA sio mat.ako kila mtu anakuwa nayo by default.
 
mdau nenda kachukue...! ukiona haikusaidii unaitupa...! ha ha ha ha ha!!!! dogo anachekesha, mbona anawaza ajira kivile... watu kama hawa ndo wanasuguaga bench hadi wakome...!
 
Hata ukiwa na PHD ya accounts without CPA you are nothing
 
Back
Top Bottom