VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Tunakaribia. Tunafika mwishoni. Tunafika pa kumaliza utata. Siku ya kupiga kura imegonga hodi. Zimebaki siku 12 za kampeni na moja ya kupiga kura. Mikutano ya kampeni inaendelea. Inazizima kutoka Dodoma hadi Ruvuma; Mbeya hadi Musoma. Mwanza nayo haiko nyuma. Lowassa na Dr. Magufuli. Historia inakwenda kuandikwa na mmoja wao. Anakwenda kuwa Rais wa Tano wa Tanzania.
Mmoja wao anajiunga kwenye daftari la kumbukumbu lenye majina ya Hayati Mwalimu Nyerere, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mzee Benjamin Mkapa na Rais Kikwete. Mmoja wao atapigiwa kura za ushindi hapo Oktoba 25 mwaka huu. Tangu kampeni zianze, Lowassa na Dr. Magufuli wanachuana kwelikweli. Wanapiga kampeni za kusheheni sera, kuomba kura na mwitiko wa vituko. Hakika, ni mpambano wa kukata na shoka.
Kwa mara ya kwanza, CCM haina uhakika wa ushindi. Si Urais, Ubunge wala Udiwani. Kwa mara ya kwanza, CCM inatumia kila mbinu lakini wapinzani wanazing'amua na kushambulia. Ni piga-nikupige; fanya nikuige. Ni mwendo wa kupita nifute; umati wako si kama wangu. Uchaguzi wa maamuzi. Tanzania mpya yaja. Ni kwa mara ya kwanza, wanawake na wazee nao wanatamani kuwapigia kura wapinzani. Wananchi hawatishiki kirahisi.
Kadiri tunavyosogelea na kukaribia Oktoba 25, ndivyo homa ya mabadiliko yao au yetu inavyozidi kupanda. Hata maji yaliyokuwa ya moto sasa yameganda. Aliyekuwa njia nyoofu sasa yuko njia panda. Hapatoshi. Mpira unachezwa Muheza, washangiliaji wako hadi Mwanza. Pwani,Tabora, Ruvuma,Morogoro,Dodoma,Rukwa,Tanga na Mtwara mbioni kuonja Wabunge wa upinzani.
Binafsi, natabiri kuwepo kwa Serikali ya mseto kwakuwa hakuna dalili zozote za chama kimoja hapa Tanzania kupata Urais, wingi wa Ubunge na Udiwani. Tanzania mpya imefika!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Mmoja wao anajiunga kwenye daftari la kumbukumbu lenye majina ya Hayati Mwalimu Nyerere, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mzee Benjamin Mkapa na Rais Kikwete. Mmoja wao atapigiwa kura za ushindi hapo Oktoba 25 mwaka huu. Tangu kampeni zianze, Lowassa na Dr. Magufuli wanachuana kwelikweli. Wanapiga kampeni za kusheheni sera, kuomba kura na mwitiko wa vituko. Hakika, ni mpambano wa kukata na shoka.
Kwa mara ya kwanza, CCM haina uhakika wa ushindi. Si Urais, Ubunge wala Udiwani. Kwa mara ya kwanza, CCM inatumia kila mbinu lakini wapinzani wanazing'amua na kushambulia. Ni piga-nikupige; fanya nikuige. Ni mwendo wa kupita nifute; umati wako si kama wangu. Uchaguzi wa maamuzi. Tanzania mpya yaja. Ni kwa mara ya kwanza, wanawake na wazee nao wanatamani kuwapigia kura wapinzani. Wananchi hawatishiki kirahisi.
Kadiri tunavyosogelea na kukaribia Oktoba 25, ndivyo homa ya mabadiliko yao au yetu inavyozidi kupanda. Hata maji yaliyokuwa ya moto sasa yameganda. Aliyekuwa njia nyoofu sasa yuko njia panda. Hapatoshi. Mpira unachezwa Muheza, washangiliaji wako hadi Mwanza. Pwani,Tabora, Ruvuma,Morogoro,Dodoma,Rukwa,Tanga na Mtwara mbioni kuonja Wabunge wa upinzani.
Binafsi, natabiri kuwepo kwa Serikali ya mseto kwakuwa hakuna dalili zozote za chama kimoja hapa Tanzania kupata Urais, wingi wa Ubunge na Udiwani. Tanzania mpya imefika!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam