COTECNA na TISCAN: IPTL nyingine?

FairPlayer

JF-Expert Member
Feb 27, 2006
4,145
716
Bandugu, Nimesoma kwenye gazeti la This day nikaona ni share na nyinyi:

Pata habari,

 
Duuuhh

Hewala, sisi ndio wajinga waliwao. Mzee FD, ukichunguza zaidi utakuja jua kuna watu kama akina siye tuliowahi kuishi nje na sasa tuko seriaklini TZ tumo kwenye "payroll", utashangaa tuwatu wana-Swap tu vi credit card vyao kufanya transfers, hii haitofautiani sana na NetGroup Sln
 
Ogah,

naomba kuelimishwa, mikataba ya mashirika ya umma yanaingiwa na nani? sio mkurugenzi/kamishna mkuu? sasa hili linalohusisha utendaji wa TRA kwanini imesainiwa na Kamishna wa customs tu? halafu kwanini wateja walikuwa wanalipia mashine ambayo haikuwepo? huu si ni wizi?

TUAMKENI, HIVI VI NGO VILIVYOJAA TELE MJINI VINAFANYA NINI? KUTAFUNA FEDHA ZA SERIKALI???!!! Kamata hawa peleka mahakamani!
 
FD,

Kuna kitu huitwa "delegation of power" huwa vinakuwa defined kwenye Contracts, zaidi kuna definitions ya nani ni "Client" and nani ni "Contractor", kwa case ya hao jamaa, sijui hivyo vitu vimekuwa defined vipi. wakati mwingine nasikia huwa wanasaini "dummy contracts" prior to original contract yenyewe ambayo lazima wakuu ndio wasaini.

Ni muhimu kujua structure/framework nzima ya hio mkataba

Wizi kupitia mikataba utaendelea kuwepo, mpaka pale tu serikali itapoamua kuweka wazi hiyo mikataba kwa wadau wote. kwani kuna kitu gani ambacho Cotecna wanafanya WATZ hatuwezi???, ndio maana wataalamu wetu wengi tu mko nje, tumewasomesha wenyewe lakini hatutaki kuwatumia kwa ajili ya CHOYO walizonazo baadhi ya viongozi wetu.
 
Ogah,

Hilo nalo ni tatizo linalotakiwa tulijadili humu, kwanini wabongo walio nje wanafanya vizuri (wasomi) wakati wakiwa hapa nchini michango yao haithaminiwi?!!, hao wageni wameajiri wabongo, wapo kwenye uongozi ngazi za juu tu, sisi tunashindwaje? hapo ndio naungana na JK kuhusu KUWEZESHWA, serikali ituwezeshe sisi wabongo kufanya kazi kama hizi za Tiscan.
 
Mambo yanaendelea.....

 
Fikiraduni,'
Kuna rafiki yangu mmoja alishawahi kusema kuwa viongozi wetu ni Pimbi wababaishaji na Mbilikimo wa mawazo. Hao ndio walipotufikisha huko. :x
 
FD, Jasusi,

Ama kweli hawa ni mapimbi,, yaani hii mikataba tunanza kuisikia ikishaanza kuwaendea vibaya

Huyo Kitillya anajikosha tu, hana lolote la maana, wao wamekaribisha wezi nyumbani kwao, na huku wakijua kabisa (wamesaini wenyewe huo mkataba feki) huyu ni mwizi, sasa mwizi anaendeleza wizi wake, eti ndio unakuja kutueleza eti huyu ni mwizi!!!, hell NO na Kitillya achia ngazi mara moja, from the very begining kwenye huo mkataba mlitakiwa kuweka vipengele ambavyo vitahakikisha huyo mwizi awe responsible ( hata sijuikama hilo linawezekana.........maana hawa ni wezi tu)
 
Tuko katika awamu ya pili ya ku-recolonise Afrika. Kibaya zaidi awamu hii wanashiriki wale tunaowaita eti ni viongozi.
 
Huyu Mzee Karimagi,

Ni mzee wa macontena, yaani mfanya biashara za kuyasafirisha makontena toka bandarini mpaka sehemu mbali mbali yanakotakiwa na customers,

pia ni mwanamtandao halisi, nafikiri katika list ya mtandao kuna JK, RA, EL, Kingunge, Sitta, Karimagi, Diallo, Nchimbi, .........na kuendelea kwa hiyo ni mtu muhimu sana kwenye power yetu,

kazi kubwa aliyoifanya kwenye uchaguzi, ni yeye na Diallo walilipia sana shughuli za kampeni, locally na ninaamini kuwa kwa pamoja walilipia at least shillingi BLLIONI 5 mpaka 10 ikiwa ni pamoja na mzee Kamalla & Masha,

Hawa ni watu waliokuwa wakipiga kampeni ya ubunge na kuwaambia wananchi kuwa watakuwa mawaziri, kwani walishaahidiwa mapema haikuwa siri,

Now kuhusu hayo aliyoyasema, ndio exactly JK anavyotaka viongozi wanaofikisha ujumbe kama alivyosema kwenye vikao vyao vya siri ambavyo hufanyika kila siku usiku baada ya vikao vya bunge, JK hawezi kukataa kuwa huyu jamaa amesema ambayo hakuyasema au kuyapitisha, ndio maana JK amewachagua kina Makamba ni kwa ajili ya kupitisha kila analosema bila ya kuuliza wala kubisha!
 
Mzee ES,
Basi kuna kazi. Sasa hayo mamilioni waliyotoa watarudishaje kama si kufanya mambo ambayo yatakuwa na madhara kwa nchi? Ndiyo maana nimesema huu ni ukoloni namba 2. Wakoloni wa kwanza walikuwa watoka nje na hawa ilikuwa rahisi kuwatambua na kuwatimua. Hawa wakoloni wa sasa wamo ndani kabisa kama vile chawa. Watatumia nafasi zao katika uongozi kujitanua. Hakuna conflict of interest, hakuna national interest ni personal interest peke yake.
 
Na kinachoudhi... chombo pekee ambacho kingeweza kuchunguza na kuwaambia wananchi nacho kiko kimya..!! Bado ni wapinzani ndo wanaonyesha uchungu zaidi na nchi kuliko chama CHAWALA! Hakuna mwaandishi ambaye yuko tayari kuwabana na kuwahoji maswali na kuwaweka kwenye rekodi! Hakuna mtu ambaye yuko tayari kwenda mahakamani kudai habari fulani zihusuzo jamaa zitolewe hadharani!! Watu tunakwenda mzoba mzoba tu!!!
 
Nchi imetafunwa sana na awamu ya tatu! bado tena tuna mawaziri wa amamu ya nee ambao tena wanatakata kututafuna!!

huyu Karamagi mbunge wa huko kigoma labda ni mrundi kwa kwa maana mtanzania asilia anapaswa kuwa na hurumu tumekamuliwa sana na akina Sumaye sasa wameona aibu hadi kukimbia nchi!


Sasa huyu Karamagi na Masha tena JK anataka kuwatumia kutumaliza kabisa!!!!!!!!!!!


beating a dead snake again!!

JAMANI KAMA JK UNASOMA HAPA TUNAOMBA UTUHURUMIE SANA WATANZANIA TULIWEKA MATUMAINI MAKUBWA KWAKO!!

TAFADHALI JK MUONGE MUNGU!!! WATANZANIA WANA MAISHA MAGUMU SANA WALIKUPA ASILIMIA 80% KWA IMANI KUBWA LEO HATA MWAKA MMOJA HAUJAISHA UMEANZA KUSAHAU!

UKIJISAHAU KABISA TUTAOMBA AKINA KONY WA TANZANIA WA TANZANIA WAJITOKEZE HAKUNA HAJA YA KUNYONYWA NA KINA KONY WAKO KAMARAGI NA MASHA.

FUATILIA MASUALA YA MERERARI KAMA ULIVYOAHIDI!

JK MUOGOPE MUNGU ATAKULAANI SANA KAMA UTASAHU IMANI YA WATANZANIA KWAKO!
 
More of Karimagi......,

Huyu mzee Karimagi ni juzi tu amefanya maajabu makubwa kwa kumnyang'anya mke wa mwanamtandao mweziwe, mzee P. Mongella, mjube wa NEC ya CCM na ambaye juzi alizawadiwa u-DC,

Mke wa mzee Patrick Mongella, ambaye ana watoto watatu naye, alikwenda India kwa scholarship ya miaka miwili, kumbe haikuwa ya kweli zilikuwa njama za huyu mzee Karimagi, ambaye alikuwa akijimwaga huko mara kwa mara kujirusha naye, wiki mbili zilizopita mke alirudi, sasa mzee P, na familia yake walikwenda kumpokea Airport, walipofika tu nyumbani mama akamwambia mzee P, kuwa it is over na kwamba "amechoka na umasikini wa Patrick" anaondoka,

kutoka pale akahamia kwenye apartment ya kifahari aliyokuwa ametayarishiwa na huyu mzee Karimagi, huko Obey na kumuacha mzee Patrick na watoto watatu, lakini mzee JK akampoza na u-DC,

now hawa ndio viongozi wetu wa awamu ya nne, ambao hawana aibu wala utu kwa viongozi wenzao, sasa vipi sisi wananchi wasiotuona wala kutujua? Mzee Jasusi, you got it right tena huu sio ukoloni ila ni ujambazi bro!

Pole pole wananchi wataanza kuyaona tuliyoyasema wakati wa uchaguzi kuwa Mungu hatamsamehe Mkapa kwa mambo aliyotufanyia watanzania na hii "Suprise!", ndio maana hawa kina Karimagi na the likes kina Masha, na Diallo wamepewa wizara za mlo na bila manaibu wawili ili warudishe hela zao za kampeni, that is all guys!
 
Mzee ES, hizi ni habari nzito tena kubwa na za kutisha!! Kesho nitapata nafasi ya kuwauliza hawa waandishi wetu ni kitu gani kinachowafanya kuogopa kuuliza maswali yenye kina na badala yake wamebakia kuwafuatilia watu wachache usiku kucha!! Ila hili la waziri kumzidi kete jamaa nalo ni kali kama nini....

Tatizo ni kuwa watanzania tumezoea viongozi uchwara, na hatuko tayari kuwawekea kiwango cha juu cha utendaji. Mediocrity is being toleraed while incompetence is rewarded! Nchi ya namna hiyo haitafika mbali... Mzee ES nipe data na zitawekwa hadharani bwana....
 
Mzee Mwanakijiji,

Kama unataka kujua ni kwa nini waandishi wa habari wanacheza dana dana, kwanza fuatlia ma-DC waliochaguliwa, kuna waandishi waliopewa u-DC, na kuna wanaosubiri ahadi zao kina Salva Rweyemamu,

leo ukiona waandishi wanamuandama kiongozi yoyote wa awamu hiii, ujue huyo sio mtandao, sasa hata wasiokuwa mtandao wamejifunza na wameanza kuwalipa waandishi wetu mbuzi,

Habari kama hizi za Karimagi zilipaswa kuwa kichwa cha habari hasa kufuatilia hizo kauli za kipumbavu alizozitoa kuhusu JK, lakini kimyaaaaaaaa!
 
Mzee Es
Habari hizi zimenfanay chai imeshindwa kupita na hata akili kuwaza imeisha kabisa .Mimi nilisema nyuma kwamba JK hana nidhamu na mwil na hata ndoa yake analala hovyo na wanawake hawezi kuwa kiongozi wetu safi watu wakasema ana sura nzuri na tabasamu kubwa iko kazi sasa .

Kuna mambo nafuatilia naona magazeti yako kimya na JK yuko kimya .Uranium imekamatwa TZ ikiwa inaelekea Iran kivipi? Jk unataka kutupeleka pabaya ndugu .Kitendo cha media kuwa kimya na wapinzani kubanwa kinaleta hisia mbaya sana .Bora Mkapa alikuwa mbabe lakinij baadhi ya habari zilisikika na akaonyesha ubabe wazi wazi kuliko huyu anayetumia kila aina ya njia kuziba ukweli .

JK kweli umeamua kuwa betray wapiga kura wako na watanzania ambao walifikia kukuita wewe ni Nabii kuna nini ? Mimi nilisema CCM haina maana hata JK hana maana ni mtu wa humo ndani miaka yote watu wakadhani nina roho mbaya .Nilikuwa kwenye kibanda nanyoa nywele baarabara hii Arusha Nairobi hapa wanapo osha magari .Akaja mzee mmoja yeye alikuwa ni mtu Ntagazwa akasema yeye kakaa sana kwenye system na alifanya kazi na Mwalimu na hadi anafanya kazi kwenye system aliahidi kutomchagua muhuni .Akiwa na maana ya JK alisema uchafu wa Dodoma wote na akasema hana uhakika kama miaka 5 ya kwanza itakuwa salaam maana Nchi uongozi umepatikana ma udhalimu na pesa na uganga wa kienyeji.Sasa haya ni maneno ya mzee leo kuna Kirimagi kuchukua mke wa mtu na JK anatoa baraka za kumpa u DC shame on your JK na unafiki wako .
 
Mwanakijiji,
Waandishi wa Bongo hawawezi kusema chochote. Wameshanunuliwa. Rai lilikuwa gazeti makini na independent lakini nasikia Rostum ameshalinunua na kuungwa mkono na Salva
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…