Sidhani kama watakuwa wanamlipa maana inaweza kuzuka scandal. Nasema sidhani kwa sababu sijawahi kuona RAIS akitangaza bidhaa za biashara. Ina maana kwa kuvaa kwake nguo na akalipwa, atakuwa anatangaza biashara za watu na hiyo nafikiri nchi nyingi wanaipiga marufuku.
Ndiyo maana kuna balozi mmoja wa Tanzania alifungua Bar huko Sweden na wakampiga STOP. Wakamwambia au aache Ubalozi awe mfanya biashara au afunge biashara. Nafikiri ukishakuwa na cheo fulani, basi baadhi ya vitu huruhusiwi kufanya. Sasa hebu fikiria kama Obama mwenyewe angelikuwa anashonewa nguo na akina Prado na wanamlipa, si Mafisadi wangelikuwa wanaingia Jumba Jeupe kila siku na masanduku ya Fedha/Nguo....
Nafikiri sanasana anakuwa anashonewa nguo na watu fulani. Ingawa ninavyofahamu, ni kuwa huwa anaingia dukani mwenyewe na kujichaguliwa randomly. Ila tu hapa washauri watakuwa sanasana wanamwambia kwenda kwenye maduka ambayo OWNER ni wananchi wa USA. Ukishaona Mama Obama kavaa nguo yako, sanasana unaweza kwenda kusaidia pesa kwenye foundation yake kama ASANTE.
Papa ninavyofahamu, ana washonaje wake wa nguo na viatu. Kwa miaka mingi sana zimekuwa ni familia fulani tu wanafanya hiyo kazi. Ila mara nyingi wanakuwa wamefungwa kwa mikataba kuwa hawatashonea watu wengine nguo.