Confessions: Nilimfukuza kaka yangu kichawi

Confessions: Nilimfukuza kaka yangu kichawi

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
19,349
Reaction score
36,303
Habari zenu wakuu!Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu. First of all,let me refresh your memories.Mwaka jana niliandika uzi kuhusu kukerwa kwangu na kaka yangu wa damu,kutokana na tabia zake ambazo kusema ukweli zilikuwa a disgrace for our family.

Kwa ufupi jamaa alikuwa amejiingiza kwenye ulevi wa pombe kali za kienyeji, uvutaji wa bangi ulio kithiri na kujiunga kwenye makundi ya fujo na vurugu.

Tabia na mwenendo wake vilikuwa a disgrace (fedheha)to our family. Tulijaribu kumshauri na kumsihi kwa kila namna lakini hakubadilika. Tukamtafutia kozi mbalimbali za kusoma,alakini where( wapi )..Akapewa mtaji wa biashara,wapi...Akatafutiwa kazi,wapi..!

Yeye anachokitaka ni ulevi,bangi, na utemi...


Nikaona isiwe tabu...
Wazigua wana uchawi wao fulani hivi,unaitwa SUNKHWA . Yaani maana yake fukuza. Hii inaitwa 'SPIRITUAL EXILE ". Unamfukuza mtu asiye faa kwa kutumia uchawi..

Wazee wa kimbulu, wana uchawi wao pia, unao fanana na sunkhwa. Huutumia uchawi huu,mkuwafaukuza watoto wenye tabia zinazo dhalilisha na kufedhehesha familia.

Ukifanyiwa uchawi huu, utaondoka kwenu na kwenda mahali utakapo pachagua wewe. Hutorudi tena nyumbani kwenu.Hutopakumbuka nyumbani kwenu ukiwa unaishi. Utakumbuka nyumbani kwenu siku utakayo kuwa kaburini...


So personally, nikaamua kumpiga sunkhwa huyu jamaa. Aliondoka siku moja,tangu tambiko hilo lilipo fanyika.

Kwa sasa sijui yupo wapi na sitaki kujua yupo wapi.Alinifanya nikufuru Mungu kwa kumwambia,kwanini umetupa ndugu asiye faa....

NIMEMTOSA BAHARINI, SAMAKI WAKE ATAMMEZA HUKO..................
 
Wewe hata Mungu atachukua muda sana kukusamehe kwa kumfanyia ndugu yako wa damu kitu kibaya kama hicho ,usipotubu subiri balaa lake.Wewe ungemleta kwa Yesu angeshafunguliwa hayo maroho machafu na akawa mtu mzuri kwenye jamii yake
 
Wewe hata Mungu atachukua muda sana kukusamehe kwa kumfanyia ndugu yako wa damu kitu kibaya kama hicho ,usipotubu subiri balaa lake.Wewe ungemleta kwa Yesu angeshafunguliwa hayo maroho machafu na akawa mtu mzuri kwenye jamii yake


Ndo maana nikasema, NIMEMTOSA BAHARINI,SAMAKI WAKE ATAMMEZA HUKO.....
 
Nimekuelewa unajipigia promo ya biashara kistaarabu,

Hongera, watakuja wengi we subiri tu!

Buhahahahahahaha! umewaza mbali sana! siwezi kufanya biashara ya uchawi hata siku moja!!!
 
Kama una uwezo huo basi badala kufanya uchawi wa kumfukuza kwanin basi usingefanya uchawi wa kumbadilisha tabia awe mtu mzuri?

It was not about him. It was about me and other good members of our family.
 
Sijakuelewa.Hivi sasa unajuta au unaturingishia au unajivuna au unatufundisha au unadeka kwa mikogo ya ufukuzaji wa nduguyo?Au ni nini hasa mkuu?

Nawafahamisha kuhusu njia nzuri na salama ya kudeal na mtu anayekuletea usumbufu katika maisha yako.Badala ya kumuua au kumfunga,we mpige sunkhwa tu.U know kuna wengine wanawaua kabisa!!!
 
It was not about him. It was about me and other good members of our family.

Thats my question.Uliona anakuhaibisha na kuaibishs familia na uchawi wewe unaoweza; kwanin kwa kutumia huo uchawi hukumbadili tabia awe na sifa nzuri na tabia ambayo familia ingejivunia?

Ndio maana nimeuliza au uchawi hauwezi kufanya kitu positive?kama hicho cha kumbadili tabia awe mtu mwema?
 
Hukumsoma Nyambare Nyagwine au Michael Kadege ? Hiyo inaitwa "CODE SWITCHING" or " CODE MIXING". Matter fact, English is our official language
nyambare nyangwine ni nani au ni mmoja wa magaidi walioshikwa?
 
sasa hili ni swali, hoja, maoni, tangazo la biashara au nini?
 
Sikubaliani na hiyo falsafa yako ya "....total destruction is the only solution..." mkuu.
 
Thats my question.Uliona anakuhaibisha na kuaibishs familia na uchawi wewe unaoweza; kwanin kwa kutumia huo uchawi hukumbadili tabia awe na sifa nzuri na tabua ambayo familia ingejivunia?

Ndio maana nimeuliza au uchawi hauwezi kufanya kitu positive?kama hicho cha kumbadili tabia awe mtu mwema?

Why did i not think of that??!!!. Anyways, kama ningetakiwa kufanya hivyo,ningefanya hivi. Ningechukua jini mmoja (Jina kapuni ),nikamuweka ndani ya nafsi ya huyo jamaa.Tabia za huyo jini ndo zingekuwa tabia za huyo jamaa. Meaning,jamaaangekuwa kama msukule vile na angekuwa dizaini kama zezeta vile. Kwa maana nyingine, tungekuwa tunaishi na jini na sio mtu. Pili gharama za uchawi huo ni kubwa sana ikilingwanishwa na gharama za sunkhwa. Tabia ni kama ngozi, huwezi kuibadili.Alichagua maisha hayo. Alitufanyia usumbufu mkubwa. So let him leave our presence
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom