Hello Jff,
Siku za hivi karibuni kumekuwa na upungufu mkubwa wa vizuo vya maambukizi ya magonjwa ya zinaa na mimba zembe.Kwa utafiti mdogo niliofanyanya kwenye mitaa ya dar wa salaam bidhaa hii imekuwa adimu na ikiwa inapatikana kwenye maduka machache na kwa bei ya juu kwa paketi moja kuunzwa kati shilingi 700 mpaka 1000.kwenye maduka machache ya madawa bidhaa hizi zipo ila nyingi zinaanzia shilingi 2000 na kuendelea,ambayo mtu wa hali ya chini hawezi kumudu.
Jambo la kushangaza hata wasambazaji kwenye maduka ya jumla wamekuwa wakilalamika ufinyu wa upatikanaji wa hii bidhaa.
Hii ni hali inayolikumba jiji la dar es salaam ambapo tunaamini asasi nyingi za afya ya uzazi ndipo zilipojikita na bado usambazaji umekuwa changamoto ukiachilia mbali mikoani (mafinga,njombe na kadhalika) ambako hii bidhaa haipatikani kabisa.Hii hali inatia hofu sana na ukizingatia takwimu za maambukizi ya VVU/UKIMWI bado zipo juu.
Sijasikia wizara ya afya ikitoa neno lolote kuhusu hii hali na namna wamejipanga kulitatua kabla madhara makubwa hayajatokea.
Swali.. Kama taifa tunaelekea wapi?