Mkuu
Consigliere unakumbuka ule uzi wako kuhusu Korea Kaskazini ?
Uchina , Korea Kaskazini na Urusi wanataka wawaweke Korea Kusini na Marekani kwenye kikaango,
Huku akijua kabisa Marekani atafanya kila namna kujaribu kufanyia figisu Korea Kaskazini tena, hapo atapata kisingizio kwamba yeye alikubali mazungumzo na pila alikubali kwenye kwenye michezo ya Olympiki: Ana nia njema kabisa ya kumaliza huu mgogoro lakini Marekani hataki. Hii lazima itazua taharuki kwa wananchi kwa Korea Kusini kwasababu Marekani ataoneka dhahiri kabisa kwamba hataki suluhisho na anahatarisha maisha yao.
Huu mchezo wa
Divide et Impera (Iron Wedge Diplomacy) ameitumia sana Urusi Barani Ulaya,
Kawafanyia Vurugu kule Ukraine na kajibebea Crimea lakini kwenye
Minsk Agreement akaenda vizuri tu huku akisema yeye Wayukreini ni ndugu (Brethren) hivyo anapenda wakae chini wayamalize. Hapa Marekani alitengwa kabisa wakenda Maraisi wa Ufaransa, Belarus, Ukraine na Ujerumani. Mwisho wa siku Marekani juzi amekubali kuuizia silaha nzito (Lethal Weapons) nchi ya Ukraine kinyume kabisa na makubaliano ya Minsk na leo hii Marekani anaonekana Mkorofi mbela ya Jumuiya ya Kimataifa. (Very Clever Move; Exceptionally Clever)
Leo hii Bunge la Ulaya wanasema Marekani anahatarisha Usalama wa Ulaya kwa kumchokoza Urusi,
Marekani haaminiki sana Ulaya kama ilivyokuwa zamani na anaendelea kutengwa kila siku,
Nigel Farage juzi akasema ndani ya Bunge la Ulaya kwamba "When you poke the Russian Bear expect the reaction"
Sasa Korea Kaskazini kaiga huo mchezo,
Lakini mimi nagopa sana kwasababu tofauti kabisa na nchi ya Ukraine Marekani ana maslahi makubwa sana pale,
Ndiyo maana nikasema hayo mazungumzo yatamalizika vizuri endapo wahusika wakubwa (Uchina, Japan, Urusi na Marekani) Mbali na Korea zote kuhusishwa. Ufaransa, Ujerumani na Belarus walihusishwa kwenye Minsk Accord kwasababu wao wana maslahi ya moja kwa moja nchini Ukraine tofauti na Marekani.
NB: Korea Kusini na Japan ni masoko makubwa sana ya kibiashara ya Marekani pia ni eneo la kimkakati kwa Marekani kulinda The Western Hemisphere: Vivyo hivyo Uchina na Urusi wana maslahi ya moja kwa moja nchini Korea Kaskazini ndiyo maana nasema ili kuwe na amani pale kwenye Korean Peninsula ni lazima kuwe na Bilateral Agreement ambayo itahusisha minimum support or supervision kutoka nchi nyingine husika....
Marekani anapeleka Masilaha kule Ukraine kuwakomesha Ulaya na Urusi kwa kutotaka kumhusisha kwenye Mkataba wa Minsk anatuma ujumbe kwamba huwezi kupata suluhisho la amani bila yeye kuwepo.
Mfano mwingine hai kabisa,
Hata kule nchini Syria kama unakumbuka kwenye
Astana Peace Talks walikaa Uturuki, Urusi na Iran halafu USA na Israel wakapigwa kapuni lakini mwisho wa siku umeona sasa Urusi na Syria wameshinda vita lakini Marekani na Isreal wamekataa kutoka nchini Syria na naskia wana mpango wa kukata kipande cha Syria na kutengeneza Kurdish State (Another USA client state in the middle east). Mpaka leo asubuhi nasikia U.S.A amepanga kutengeneza kikosi cha Wanajeshi 30000 wa Kikurdi ambao wengi wao ni wastaafu wa jeshi la Syria. Juzi wametuma drones zimelipua kambi ya Warusi, leo wanaweka wanajeshi kama 30000 kwenye mpaka wa Uturuki ambapo humo ndani kutakuwa na majamaa ya IDF, SIS, NAVY SEALS na Mercenaries wengine wenye silaha nzito.
Hivyo basi,
Tukiangalia haya mambo in a Realistic Point of view,
Huwezi kupata suluhisho la kisiasa la kudumu hapa duniani bila kuhusisha Urusi,USA na Uchina (Kwenye issue ya Korea) Hawa wawili ndiyo chanzo cha hii migogoro yote na vurugu zinazoendelea hapa duniani. Endapo utaweza kuwaweka hawa Simba Dume wawili kwenye zizi moja basi utaona amani ya kudumu nchini Korea na kwingineko duniani.
Kama
CUBA mwaka
1962 na Ujerumani mwaka
1985 iliwezekana kwanini
Korea 2018 Ishindikane kama wakiamua ???