Consigliere
Platinum Member
- Sep 9, 2010
- 12,689
- 26,568
Mkuu Consigliere unakumbuka ule uzi wako kuhusu Korea Kaskazini ?
Uchina , Korea Kaskazini na Urusi wanataka wawaweke Korea Kusini na Marekani kwenye kikaango,
Huku akijua kabisa Marekani atafanya kila namna kujaribu kufanyia figisu Korea Kaskazini tena, hapo atapata kisingizio kwamba yeye alikubali mazungumzo na pila alikubali kwenye kwenye michezo ya Olympiki: Ana nia njema kabisa ya kumaliza huu mgogoro lakini Marekani hataki. Hii lazima itazua taharuki kwa wananchi kwa Korea Kusini kwasababu Marekani ataoneka dhahiri kabisa kwamba hataki suluhisho na anahatarisha maisha yao.
Huu mchezo wa Divide et Impera (Iron Wedge Diplomacy) ameitumia sana Urusi Barani Ulaya,
Kawafanyia Vurugu kule Ukraine na kajibebea Crimea lakini kwenye Minsk Agreement akaenda vizuri tu huku akisema yeye Wayukreini ni ndugu (Brethren) hivyo anapenda wakae chini wayamalize. Hapa Marekani alitengwa kabisa wakenda Maraisi wa Ufaransa, Belarus, Ukraine na Ujerumani. Mwisho wa siku Marekani juzi amekubali kuuizia silaha nzito (Lethal Weapons) nchi ya Ukraine kinyume kabisa na makubaliano ya Minsk na leo hii Marekani anaonekana Mkorofi mbela ya Jumuiya ya Kimataifa. (Very Clever Move; Exceptionally Clever)
Leo hii Bunge la Ulaya wanasema Marekani anahatarisha Usalama wa Ulaya kwa kumchokoza Urusi,
Marekani haaminiki sana Ulaya kama ilivyokuwa zamani na anaendelea kutengwa kila siku,
Nigel Farage juzi akasema ndani ya Bunge la Ulaya kwamba "When you poke the Russian Bear expect the reaction"
Sasa Korea Kaskazini kaiga huo mchezo,
Lakini mimi nagopa sana kwasababu tofauti kabisa na nchi ya Ukraine Marekani ana maslahi makubwa sana pale,
Ndiyo maana nikasema hayo mazungumzo yatamalizika vizuri endapo wahusika wakubwa (Uchina, Japan, Urusi na Marekani) Mbali na Korea zote kuhusishwa. Ufaransa, Ujerumani na Belarus walihusishwa kwenye Minsk Accord kwasababu wao wana maslahi ya moja kwa moja nchini Ukraine tofauti na Marekani.
NB: Korea Kusini na Japan ni masoko makubwa sana ya kibiashara ya Marekani pia ni eneo la kimkakati kwa Marekani kulinda The Western Hemisphere: Vivyo hivyo Uchina na Urusi wana maslahi ya moja kwa moja nchini Korea Kaskazini ndiyo maana nasema ili kuwe na amani pale kwenye Korean Peninsula ni lazima kuwe na Bilateral Agreement ambayo itahusisha minimum support or supervision kutoka nchi nyingine husika....
Mkuu Malcom Lumumba ndiyo maana mimi siku zote nimekuwa nikiamini kwamba South and North Korea ni projects zilizosukwa kimkakati. They agreed/decided to divide in order to advance and contain.
Haya mataifa yenye umri mkubwa (1000+ years) huwa wana akili zilizo beba maono ya mbali sana. Na mikakati yao ni kuvivusha na kuvijenga vizazi vyao siyo class fulani. Hivyo mataifa kama China, Korea kusini na Kaskazini wanaweza kufanya lolote kwa ajili ya vizazi vyao.
Kuna series niliwahi pata kuiangalia kuna kakipande kadogo mno kwenye moja ya Episode kanaonyesha namna usiri mkuu uliopo baina ya mataifa haya ukikaangalia kwa akili nzuri utaona kuna mikakati ilishatengenezwa kabla hata hawajafarakana ni namna gani watakuja kuungana huko mbele. Na kuna watu wanahakikisha mgogoro unakua mkubwa kwa gharama yoyote ile lakini hii yote ni mbinu tu.
Korea Kaskazini ni mbeba msalaba lakini lastly hawa kuna kitu wanamchota mzungu.