Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Naona Dogo wanamchanganya sana watu hapa, masikini weee. Imebidi nirudi nimsaidie.
Kijana, kwenye haya madudu, mie si mtaalam sana ila nafahamu mgawanyiko wake ulivyo.
Kwenye Computer kuna Hardware na Software.
Hardware: Hii hujumlisha wale watu wanaunda Computer (Assemble) na ku-design vitu hizo Integrated parts za Computer kama CPU, RAM, Graphic cards etc. Hizi wala usipoteze muda kuzisoma maana milele hutakuja ukae uwe mtengenezaji. Wamezishika sana watu kama akina Intel, AMD, ASSUS, nk. Sanasana wee utabaki kuwa MUUNDAJI tu. Kwa nchi duniani, ni USA, Taiwan, Malaysia, Thailand, Hong Kong na wengine kadhaa ila mama lao ni Thaiwan.
Software: Hizi nazo zimegawanyika kwenye sehemu kama TATU hivi ingawa kuna kitengo zinakuwa kama mbili-
1. Watengeneza Programing na baadaye kuziuza program zao. Hawa ndiyo watu kama akina Oracle, Microsoft, Norton nk.
2. Wanaosomea hizo program zilizonunuliwa hapo juu na kufundisha watu wengine. Wakati mwingine wanatumia utundu wao wa kuzaliwa na kuleta matumizi fulani ya hizo program ambayo hata wale jamaa wa juu hawakufikiria.
3. Watumiaji wa kawaida ambao inabidi wafundishwe na watu wa pili au wa kwanza kwa ajili ya kazi zao.
Mtu wa pili na wa kwanza wanaweza wote kuwa wamesomea IT. Anaweza kuwa mtu yuleyule kaandika program na kuwafundisha watu jinsi inavyofanya kazi. Katika hizo program, zinapishana sana na kuna zile rahisi ambayo hata wewe leo hii unatakiwa kuwa unaweza kuifanya. Kwa mfano unatengeneza kiprogram cha ku-solve quadratic equation.
Umuhimu wa watu waliosomea IT ni kuwa wanakuwa wameshaweka Msahafu wa Computer kichwani na hii inawasaidia kuwa flexible kwenye field tofauti. Kwa mfano, wanakuja watu wa Muhimbili wanataka kutengeneza kifaa cha kipimo fulani na jamaa wanakaa na Madaktari, kusikia jinsi utaratibu ulivyo na wanatoka na kifaa kilichokuwa na program ya kufanya hivyo. Kesho watakuja watu wa madini wanataka kifaa cha kupimia udongo wenye dhahabu/almasi nk. Wanakaa nao na kujadili jinsi utaratibu wao ulivyo na jamaa wanakuja na kifaa/program ya kupima.
Nilishashuhudia Prof. mmoja aliyekuwa amebobea kwenye somo la Theory of Elasticity and Plasticity alienda USA na kufanya kazi hospital pamja na Madktari na wakali wa IT. Wali-design taya la binadamu bandia. Hapa, Madaktari walianza kwa kuweka jinsi taya linavyofanya kazi. Prof. huyo juu alikuja na kuweka Model nzima ya taya na kutafuta kila sehemu ya taya iwe na Strength kubwa kiasi gani. Watu wa IT ndipo wakaingia sasa na kuchanganya walivyosema Madaktari na huyu Prof. mhandisi. Mwisho wakaja na taya zima lililotengenezwa kwa ushirikiano wao wote.
Ukisomea IT unakuwa kama Mpishi mzuri sana anayejua kupika karibu vyakula vyote duniani. Utaweza kupika chakula kizuri popote pale duniani hata kama huna baadhi ya viungo au vyakula.
Baadhi ya vyuo wanadanganya kuwa wanafundisha hiki au kile ila ukweli wanafundisha kitu kilekile na wengi wao kwa ufupi wanafundisha ELECTRONICS ambayo inahusisha hivi vitu vyote.
Ndiyo maana nikasema hakuna kitu kama Computer Engineering. Wewe kama wataka kuwa Mchezea pote, basi soma Electronics Engineer maana utakuwa na uelewa kila sehemu kidogo. Ukitaka kuwa mtengeneza program basi nenda kwenye IT ila huko, unaweza kujifunza kuunda Computer kwa muda wako maana hakuna mtu atakufundisha. Ila kuna baadhi ya shule sasa wanafundisha baadhi ya field moja kwa moja na IT yake. Kwa mfano unaweza ukasomea kitu kinaitwa Computerised Economics ambapo unasoma Uchumi na IT. Nafikiri pia kuwa ujenzi na IT, Uganga na IT, nk na hawa wanakuwa wakali wa IT ila wamebobea kwenye field zao moja kwa moja yaani anakuwa Mhandisi na mtu mwenye ujuzi wa IT au Mganga na ujuzi wa IT.
Telecominication ni somo lenye future nzuri sana maana kila siku vifaa vinakuwa vingi sana na sidhani itafika sehemu watu wakose kazi. Hili halihitaji sana maelezo.
Jambo la muhimu ni kukumbuka kuwa ukiwa CHUO KIKUU, baadhi ya mambo jisomee mwenyewe na usisubiri mtu akufundishe. Usisome ili upass mitihani bali soma ili yakusaidie huko mbele ya safari au kwa faida yako mwenyewe. Kuandika ukurasa wa WWW, hakuna atakayefundisha ila kama umesoma IT, basi utajisomea wewe mwenyewe na maadam una msingi mzuri, utaelewa na kuwa na uwezowa kutengeneza WWW yako mwenyewe. Computer ikiharibika, kubadili RAM, HDD, sijui CPU, utajifunza mwenyewe na mwisho unakuja kuweka data sawa kwenye BIOS na mtambo unafana kazi.
KILA LA KHERI.
Kijana, kwenye haya madudu, mie si mtaalam sana ila nafahamu mgawanyiko wake ulivyo.
Kwenye Computer kuna Hardware na Software.
Hardware: Hii hujumlisha wale watu wanaunda Computer (Assemble) na ku-design vitu hizo Integrated parts za Computer kama CPU, RAM, Graphic cards etc. Hizi wala usipoteze muda kuzisoma maana milele hutakuja ukae uwe mtengenezaji. Wamezishika sana watu kama akina Intel, AMD, ASSUS, nk. Sanasana wee utabaki kuwa MUUNDAJI tu. Kwa nchi duniani, ni USA, Taiwan, Malaysia, Thailand, Hong Kong na wengine kadhaa ila mama lao ni Thaiwan.
Software: Hizi nazo zimegawanyika kwenye sehemu kama TATU hivi ingawa kuna kitengo zinakuwa kama mbili-
1. Watengeneza Programing na baadaye kuziuza program zao. Hawa ndiyo watu kama akina Oracle, Microsoft, Norton nk.
2. Wanaosomea hizo program zilizonunuliwa hapo juu na kufundisha watu wengine. Wakati mwingine wanatumia utundu wao wa kuzaliwa na kuleta matumizi fulani ya hizo program ambayo hata wale jamaa wa juu hawakufikiria.
3. Watumiaji wa kawaida ambao inabidi wafundishwe na watu wa pili au wa kwanza kwa ajili ya kazi zao.
Mtu wa pili na wa kwanza wanaweza wote kuwa wamesomea IT. Anaweza kuwa mtu yuleyule kaandika program na kuwafundisha watu jinsi inavyofanya kazi. Katika hizo program, zinapishana sana na kuna zile rahisi ambayo hata wewe leo hii unatakiwa kuwa unaweza kuifanya. Kwa mfano unatengeneza kiprogram cha ku-solve quadratic equation.
Umuhimu wa watu waliosomea IT ni kuwa wanakuwa wameshaweka Msahafu wa Computer kichwani na hii inawasaidia kuwa flexible kwenye field tofauti. Kwa mfano, wanakuja watu wa Muhimbili wanataka kutengeneza kifaa cha kipimo fulani na jamaa wanakaa na Madaktari, kusikia jinsi utaratibu ulivyo na wanatoka na kifaa kilichokuwa na program ya kufanya hivyo. Kesho watakuja watu wa madini wanataka kifaa cha kupimia udongo wenye dhahabu/almasi nk. Wanakaa nao na kujadili jinsi utaratibu wao ulivyo na jamaa wanakuja na kifaa/program ya kupima.
Nilishashuhudia Prof. mmoja aliyekuwa amebobea kwenye somo la Theory of Elasticity and Plasticity alienda USA na kufanya kazi hospital pamja na Madktari na wakali wa IT. Wali-design taya la binadamu bandia. Hapa, Madaktari walianza kwa kuweka jinsi taya linavyofanya kazi. Prof. huyo juu alikuja na kuweka Model nzima ya taya na kutafuta kila sehemu ya taya iwe na Strength kubwa kiasi gani. Watu wa IT ndipo wakaingia sasa na kuchanganya walivyosema Madaktari na huyu Prof. mhandisi. Mwisho wakaja na taya zima lililotengenezwa kwa ushirikiano wao wote.
Ukisomea IT unakuwa kama Mpishi mzuri sana anayejua kupika karibu vyakula vyote duniani. Utaweza kupika chakula kizuri popote pale duniani hata kama huna baadhi ya viungo au vyakula.
Baadhi ya vyuo wanadanganya kuwa wanafundisha hiki au kile ila ukweli wanafundisha kitu kilekile na wengi wao kwa ufupi wanafundisha ELECTRONICS ambayo inahusisha hivi vitu vyote.
Ndiyo maana nikasema hakuna kitu kama Computer Engineering. Wewe kama wataka kuwa Mchezea pote, basi soma Electronics Engineer maana utakuwa na uelewa kila sehemu kidogo. Ukitaka kuwa mtengeneza program basi nenda kwenye IT ila huko, unaweza kujifunza kuunda Computer kwa muda wako maana hakuna mtu atakufundisha. Ila kuna baadhi ya shule sasa wanafundisha baadhi ya field moja kwa moja na IT yake. Kwa mfano unaweza ukasomea kitu kinaitwa Computerised Economics ambapo unasoma Uchumi na IT. Nafikiri pia kuwa ujenzi na IT, Uganga na IT, nk na hawa wanakuwa wakali wa IT ila wamebobea kwenye field zao moja kwa moja yaani anakuwa Mhandisi na mtu mwenye ujuzi wa IT au Mganga na ujuzi wa IT.
Telecominication ni somo lenye future nzuri sana maana kila siku vifaa vinakuwa vingi sana na sidhani itafika sehemu watu wakose kazi. Hili halihitaji sana maelezo.
Jambo la muhimu ni kukumbuka kuwa ukiwa CHUO KIKUU, baadhi ya mambo jisomee mwenyewe na usisubiri mtu akufundishe. Usisome ili upass mitihani bali soma ili yakusaidie huko mbele ya safari au kwa faida yako mwenyewe. Kuandika ukurasa wa WWW, hakuna atakayefundisha ila kama umesoma IT, basi utajisomea wewe mwenyewe na maadam una msingi mzuri, utaelewa na kuwa na uwezowa kutengeneza WWW yako mwenyewe. Computer ikiharibika, kubadili RAM, HDD, sijui CPU, utajifunza mwenyewe na mwisho unakuja kuweka data sawa kwenye BIOS na mtambo unafana kazi.
KILA LA KHERI.
Mkuu umeua hapa