Mwanamaji
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 2,896
- 4,495
Usajili wowote ule ni kamali, hata kama mchezaji fulani kufeli kwenye klabu mpya hutokea kwa nadra sana, lakini itoshe tu kukubaliana kwamba huwa inatokea.Sikatai ni mzuri kibongobongo, nakataa thamani anayopewa. Ligi yetu hii ya bongo yenyewe viwanja vibovu na waamuzi wabovu kuna mchezaji wa 500m au 1b. Kuna ujanja ujanja wunafanywa na mawakala ili wapige pesa kupitia mchezaji. Nakwambia hata chama akiwemo ndani timu hiyo itafungwa TU. Mpira wetu unachezwa zaidi nje ya uwanja kuliko ndani ya uwanja. Hivi kazidi sana thamani yake ni 200ml.
Huwezi kusema dereva wa Corolla akipewa Carina hawezi kuendesha. Chama na Makambo wacheze vizuri Tanzania lakini wakose namba kwenye timu zao mpya. Hiyo inatokea kwa nadra sana.
Ni kweli Chama sio BIMA kwa timu ambayo yupo kwamba isifungwe. Na hakuna mchezaji duniani ambaye uwepo wake kwenye timu yako unakuhakikishia kwamba hautafungwa.
Kuhusu bei, hilo ni suala la "negotiations" hakunaga bei elekezi za wachezaji.
Hiyo milioni 200 inaweza ikatosha, au ikawa kubwa sana au ndogo sana kulingana na namna mtakavyo negotiate mezani baina ya pande zote husika.
Mawakala hiyo ndio kazi yao, ni kazi halali, hata Ulaya akina Mino Raiola wanafanya hivyo hivyo. Inabidi tuzoee.