Clouds Media watapotea sokoni kama Sahara Media

Clouds Media watapotea sokoni kama Sahara Media

Mi nlikua mpenzi mkubwa wa Power breakfast,lakini baada ya kuondoka PJ na GH,namimi na familia yangu tumeamua kuacha kuskiliza PB ya clouds fm.
 
Nilikuwa nasikiliza Clouds kuanzia saa moja na nusu asubuhi hadi arround mbili na nusu hivi ili nimsikilize PJ akisoma magazeti. Alipoondoka siwezi tena ku tune huko
 
Clouds media walikuwa wanakuja vizuri sana TZ na East Afrca katika soko la media,tatizo la kufukuza fukuza watu na bifu zisizo na msingi watapotea kama Sahara Media walivyopotea sasahivi.
Wapotee mara ngapi mkuu??
 
Clouds media walikuwa wanakuja vizuri sana TZ na East Afrca katika soko la media,tatizo la kufukuza fukuza watu na bifu zisizo na msingi watapotea kama Sahara Media walivyopotea sasahivi.
You wish.
Kila chombo cha habari kina target yake.
Na kila kipindi kina aina ya wasikilizaji wake.
Ukiona chombo cha habari au kipindi fulani ukielewi, ujue si kwa ajili yako.

Nikweli power breakfast ya Clouds imebadilika na imebadilika kwa makusudi.
Ukisikiliza njinsi Masoud anavyo jadili mambo kwa mtazamo wa ndani kidogo.
Ili kuelewa,inakubidi na wewe msikilizaji uwe na uwelewa wa mambo.Nitofauti na wakati wa Hando na PJ,walikuwa wana chekesha na kufurahisha tu.
 
Clouds itakuja kupotea lakini siyo kwa hizo sababu ulizozitaja.
 
Wote hawa walikuwa vinara wa kumtukana lowassa,sahara sasa hivi ameshusha ving'amuzi vyake kwa Zaidi ya asilimia 30 lakini hakuna mtu ananunua...Bado clouds,imekuwa ya ccm na magufuli
 
kuna kipindi chao cha asubui . kinamjumuisha brother k. kusema kweli kinaboa. utoto mwingi
 
Utoto wao na kuniana kumezidi redio ina mabifu na kusutana tu.
 
kweli mkuu nakumbuka mwaka 2007 kiss fm ilikuwa inasikilizwa hadi nchi jirani eg zambia,kenya,ug,rwanda kwA sabab ya communication media i.e English language.sahv vjana wa shule za kikwete wameharibu vipind wanaongea kiswanglsh had unachkia ukiwasklza
Ndio hiyo channel kuna dogo anajiita MABELE aka maziwa?tozi flan dot.com,nimesahau kipindi kinaitwaje.
 
KP masoud yuko poa sana studio, Jana aliniacha hoi upuuzi wake.

KP Ana IQ kubwa sana, sisi wajuzi wa kupima tunajua. wanaomlalamikia ruge kwa kumwondoa hando Gerald hawajui kitu
 
Utoto wao na kuniana kumezidi redio ina mabifu na kusutana tu.
Kiukweli huwa sisikilizi kabisa hii redio lakini kuna mazingira let's say kwenye daladala unakuta dereeevaa ndio kipindi chake , yanayoongelewa humo ni utoto na upuuzi mtupu
Kusaga alitaka awaachie vijana waonyeshe vipaji vyao sasa wanavionyesha hasa
 
Kwangu mimi walishapotea mda sana maana sijawasikiliza mwaka wa pili sasa kwa sababu ya mambo yao ya kuwapa promo watu wao (tht) ilihali wakiwanyonya tu. Bifu dhidi ya wasanii wengine pia.
Hata hapa umeamua kuwapa promo tu
 
Back
Top Bottom