Uonevu ni kitu kibaya sana, binafsi nawapongeza sana clouds kwakuwa creative na kuusogeza muziki na radio yao mahali vilipo sasa, hata wao clouds wanafahamu fika ni kazi za wasanii nikimaanisha nyimbo zilizowafikisha hapo. tujikumbushe kidogo nyuma, clouds walikuwa maDJ wanapiga madisko sehemu mbalimbali wakitegemea viingilio kama kipato chao, baadae akina sugu, J, na hatimae kina Juma Nature walipoibuka na midundo mikali ikawakuna watu, clouds wakaisense hiyo opportunity ya kuwakutanisha wasanii na mashabiki wao, ndo ma summer jam then fiesta ambayo yakawapatia udhamini na kuanza kutengeneza pesa mbali na viingilio, then wakaexpand na kufungua redio ambayo ukiacha nyimbo za nje mtaji mkubwa ulikuwa ni bongo fleva songs unakumbuka ile smooth vibes project? mara jina likawa kubwa na station ya kusikiliza nyimbo mpya za bongo ikawa clouds, Wasikilizaji hasa vijana wakawa wengi, nakumbuka kipindi kile hata mzee wangu akikukuta unasikiliza clouds alikuwa anakasirika sana, ghafla wasanii wakaanza kuleta nyimbo zenye kugusa, nyimbpo zikakubalika na hatimae segments za wasikilizaji zikaongezeka, radio ikakua na kupata sponsors kibao ambao wamewapa hela nyingi na sasa wameshalewa. Kumbuka kipindi kile cha nyuma kuimba ilikuwa njia ya kupatia madem. Radio imekuwa na wasanii wameongezeka, clouds wanadivide na kurule, wasanii wakongwe wanaojua haki zao wanapotezwa na kuibuliwa wapya ambao bado wanataka kutoka ili biashara iendelee.
Ushauri wangu, in business kila mara lazima ufanye SWOT analyisis, yaan Streghth, Weakness, Opportunities na Threats ili biashara iendelee. Kama wanafikiri bado wako powerful watakuwa wanajidanganya, sumu ya kuchukiwa imeenea sana na kama umefuatilia msiba wa Ngwair utanielewa, ni turning point tu imebaki wenye nguvu warudishiwe stahiki yao. There is no clouds without bongo fleva but there will always be bongofleva without clouds. Ukijikwaa amka tazama ulipojikwaa ili kesho usijikwae tena ili tusonge mbele,. Niwapongeza Clouds kwa juhudi zao zilizoifikisha bongo fleva sehemu ilipo leo na pia mafanikio yao katika media zao. Kuna vipindi kama amplifier na sports kinabamba sana, pb na jahazi zamani ilikuwa kweli ila baada ya kujivika mbeleko ya CCM mmetupoteza wengi wapenda kusikia yote, mema na mabaya. Kaeni na wasanii na msitengeneze maskini wenye majina makubwa kama mmoja wao alivyoimba na pia hata kama mna interest na chama fulani basi kama ni magazeti someni yote sisi hatutaki kujua CDM au CCM wamesema nini, tunachotaka kujua ni je magazeti ya leo yanasemaje? uhondo huo tunaupata times fm na si kwenu tena kama zamani. Change or Die(i mean zorota), mark my words!