NAMKWAKWA
Member
- May 16, 2013
- 43
- 38
Kampuni ya Clouds media kupitia makampuni yake ya clouds f.m na clouds Tv wamebuni mbinu ya kuwaibia watanzania ambao wengi hawana uwelewa mkubwa wa matumizi ya teknolojia ya mawasiliano kwani wanakutumia ujumbe mfupi unaohusu shughuli za burudani wanazozifanya kisha wanakukata hela,pasipo wewe mpokea ujumbe wa simu kujiunga na huduma hizo kiasi wanachokata ni Tsh 150.Hili suala ni very sensitive kwani nimejaribu kuwapigia simu watu wa huduma kwa wateja na kuwalalamikia wao wamesema hawajui kitu zaidi ya kunishauri nitume neno STOP kwenda number 15556 Ili kusitisha ujumbe huo ambao unaiba pesa za watanzania,suala la kujiuliza hapa ni kuwa mimi ni mwelewa wa mabo ya mawasiliano je kwa mjomba wangu aliyepo kule kijijini Lukuredi kama atakuwa anatumiwa ujumbe na hawa watu kila siku na anakatwa hela pasipo ridhaa yake hawa watu watakuwa wanatengeneza mabilioni mangapi ya pesa?.Hata hao watu wa huduma kwa wateja kwenye makampuni ya simu kwa majibu yao wanaonekana wameelekezwa na maboss wao kuwa mtu akihoji hili suala umwambie ulijiunga mwenyewe atume neno ONDOA kWENDA NUMBER 15556,hIvi mtu mzima na akili zako unaweza jiunga kwenye huduma za kitoto za matukio ya fiesta?.
Ufuatao ni copy ya ujumbe mfupi ambao hii kampuni inautuma ovyo kwa watanzania na kuwakata hela bila ridhaa yao
"CLOUDS TV:Angalia mkali wa ngolongolo Diamond Platnumz akiwasha moto Fiesta 2012.Diamond amewakilisha Tabora, Dodoma.SIMU.TV;Bofya; http://db.tt/CXiJhfHZ "
Nakala
i)Joseph Kusaga (Clouds media Group)
ii) Makamba J (Naibu waziri)
Ufuatao ni copy ya ujumbe mfupi ambao hii kampuni inautuma ovyo kwa watanzania na kuwakata hela bila ridhaa yao
"CLOUDS TV:Angalia mkali wa ngolongolo Diamond Platnumz akiwasha moto Fiesta 2012.Diamond amewakilisha Tabora, Dodoma.SIMU.TV;Bofya; http://db.tt/CXiJhfHZ "
Nakala
i)Joseph Kusaga (Clouds media Group)
ii) Makamba J (Naibu waziri)