Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Watangazaji wa Clouds Fm, Kibonde na Gadner wamemshukia mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa CHADEMA John Mnyika na kueleza kwamba anachanganya mambo. Wanahabari hao waliyasema hayo katika kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo hicho.
Jambo hilo lilijitokeza wakati wakisoma magazeti katika kipindi hicho ambapo Kibonde aliamua kumpuuza na kupuuza kuisoma habari iliyokuwa ukurasa wa mbele wa gazeti la Dar Leo.
Gazeti hilo lilinukuu kauli ya Mnyika kuhusu ripoti ya Umoja wa Mataifa(UN) inayohusisha Tanzania na tuhuma za uuzaji na silaha.
Kibonde alisema kuwa kitendo cha Mnyika kutaja suala la dhahabu na Kampuni ya Meremeta, na madini na ripoti ya UN inayohusu silaha ni kuchanganya mambo kwa lengo la ubunge wa ubungo mwaka 2010.
Hivyo, Kibonde aliacha kuisoma habari hiyo hewani kwa kauli ambayo iluungwa mkono na Gadner.
Kwa tukio hilo Clouds Fm imeweza kumuumbua vizuri Mnyika kwa kuwa redio hiyo ni kipenzi cha vijana kote Dar es salaam ikiwemo katika jimbo la Ubungo.
Tukio hilo ni dalili ya wanahabari kuwa makini katika kuchambua mambo na hivyo kuepuka propaganda chafu za wanasiasa dhidi ya CCM na serikali yake
........ndiyohiyo
Jambo hilo lilijitokeza wakati wakisoma magazeti katika kipindi hicho ambapo Kibonde aliamua kumpuuza na kupuuza kuisoma habari iliyokuwa ukurasa wa mbele wa gazeti la Dar Leo.
Gazeti hilo lilinukuu kauli ya Mnyika kuhusu ripoti ya Umoja wa Mataifa(UN) inayohusisha Tanzania na tuhuma za uuzaji na silaha.
Kibonde alisema kuwa kitendo cha Mnyika kutaja suala la dhahabu na Kampuni ya Meremeta, na madini na ripoti ya UN inayohusu silaha ni kuchanganya mambo kwa lengo la ubunge wa ubungo mwaka 2010.
Hivyo, Kibonde aliacha kuisoma habari hiyo hewani kwa kauli ambayo iluungwa mkono na Gadner.
Kwa tukio hilo Clouds Fm imeweza kumuumbua vizuri Mnyika kwa kuwa redio hiyo ni kipenzi cha vijana kote Dar es salaam ikiwemo katika jimbo la Ubungo.
Tukio hilo ni dalili ya wanahabari kuwa makini katika kuchambua mambo na hivyo kuepuka propaganda chafu za wanasiasa dhidi ya CCM na serikali yake
........ndiyohiyo