Clouds FM kufungiwa?

Clouds FM kufungiwa?

Wanajamvi Clounds ina identity yake ndio maana imefanikiwa pamoja na mapungufu kibao.

Tusitake kuona clouds inakuwa too much official kama TBC. Wengine watakuja wanasema hapa inaboa na hakuna ubunifu. May be watangazaji wa Clouds wana uhuru zaidi kuliko vituo vingine. Kuna faida na hasara zake but tusisahau every decision ina compromise.

katika kuwin market ya bidhaa yoyote identity ni kitu muhimu kitu ambacho kwenye media radio Clouds wana identityyao japo kuna mapungufu.

naamina makapuni mengi yakitakiwa kupunguza bajeti zao za promo radioni watakoanza kukosa wateja ni Radio One, RFA, etc. clouds itakuwa ya mwisho kutoswa

nakumbuka lile tangazo lao la
"baba naniiiiiiii usiiitoe hapo ilipoooooo ndo mahala pake"

Teh teh
 
Clouds waseme sababu ya kuandaa birthday ya jk ilikua ni nini?pesa zimewazidi au kuwa karibu na mheshimiwa ili wapate tenda zaidi za malaria haikubaliki kwa chandarua na muziki au?
 
Kuna habari kuwa Clouds fm inaweza kufungiwa au wafanyakazi wake kufungiwa kutangaza Radioni maana wananchi wametoa malalamiko yao kwa TCRA kuwa watangazaji wake wanaporomosha matusi na kuzalilisha watu kwa maneno ya binafsi wakiwa wanatangaza

TCRA watakuwa wanawaonea?

Source: Majira

TCRA hawawezi kuifungia clouds fm hasa ukizingatia hiyo ni toto ya uhuru fm kwa yule mama mdogo 'ufisadi'
so how this can be? Kikwete and his CCM mate thy know it
 
mkuu punguza jazba, inachofanya clouds ni sawa na magazeti ya uhuru, tanzania daima nk,
na humu jf wengi mnatatizwa na kipindi kimoja tu ambacho ni jahazi
kama unasikiliza asubuhi wana power break fast, humo nikukosoa serikali kwa kwenda mbele.
Kuna leo tena, karibu 80% ya wanawake hapa dar wanasikiliza.
Kisha kuna xxl, vijana karibu wote town hii ndio kipindi yao,
sasa kuna jahazi, hapa ndipo jf wanapochefuka simple kwasababu ya mtu mmoja tu, kibonde.
Kisha vipindi vinavyofuata ni miziki na michezo.
Jf kama great thinker sioni mantiki ya kila siku kupost mambo ya clouds na kuyapa kipaumbele utadhani issue ya maana, hii ni radio ya burudani siasa ni by the way.
Hakuna ubaya wowote kwa wao kuegemea ccm kama ilivyo sahihi kwa tanzania daima kuegemea chadema,
naomba niwe mkweli napenda kusikiliza clauds kama kituo cha burudani na nina hakika wengi wetu humu ndani niwasikilizaji wazuri wa clouds thats why chochote kitakacho jiri clouds utakikuta humu jf.
Na kama unajidanganya kuwa haipendwi jaribu kufanya jautafiti kadogo, pita uswahilini, panda madaladala utapata majib
u

Hapo pekundu.

Kwa bahati mbaya kupendwa kwa kitu hakuashirii ubora/umaana wa kitu hicho kinachopendwa. Kwa mfano ukikuta mhubiri (awe muislamu/mkristo n.k) anatoa neno watu wengi watapita tu bila hata kujihangaisha kumsikiliza. Subiri mtu aanze kumwaga mitusi hapo hapo uone watu watakavyojazana kusikiliza!!

Ndio maana magazeti ya udaku yananunuliwa sana kuliko Business Times
 
haifai kuwa redio ya kusikiliza bali inatakiwa iwe kijarida cha kitchen part tu................akina kibonde wanaharibu sana redio na mimi niliishaacha kusikiliza tangu niliipoona kuwa wamenunuliwa na mafisadi na ccm wakati wa uchaguzi............wamefulia........
CLOUDS HAWANA VIPINDI VYA KUELEIMISHA NA WALA HAWANA UWEZO WA KUELIMISHA....REDIO YAO IFUNGIWE KWANI HAPO BAADAE WANAWEZA KUWA WACHOCHEZI HASA MTU KM KIBONDE...........NOT WANTED IN MEDIA AENDE AKAGANGE NJAA CCM

Kipindi cha michezo kinalipa mimi huwa nasikiliza
 
Ni ajabu kuona namna baadhi ya Watanzania wasivyoelewa maana ya umuhimu wa vyombo vya habari. CLOUDS FM inaweza kuwa na matatizo yake ( na awali ya yote ni nani asiye na matatizo yake) lakin i kwa sasa ni redio ambayo inaongoza kwa kuwa na 'wateja' (wasikilizaji) wengi, ingawa utafiti wa kina bado haujafanyika.

Baadhi yetu sisi wana-JF tunavyozidi kuichukia na kuanzisha mjadala wa kuijadili ndivyo tunavyozidi kuipa ,chati' redio hii. Hata tv yao nayo ni kiboko. Hii ni redio ambayo siyo ya mafisadi ni ya watanzania wenzatu waliojaa ubunifu na kuthubutu kuanzisha kitu cha maana. Isipokuwa sisi baadhi ya watanzania tulivyo na wivu ndio maana sishangai kuona kuwa baadhi ywetu tumeanza kuichukia clouds ambayo hata ukichukia namna gani haisaidii.

Hilo lakuwa nawateja wengi,ubunifu wao sio tatizo kwetu ila shida ni huyu mtu wakujipendekeza KIBONDE ukimtoa huyu Clouds FM Saaaaaaaaaa...fiiii.
 
Back
Top Bottom